KERO Treni ya mchongoko Dar-Dodoma imeharibika porini toka saa 2 asubuhi kati ya eneo la Pugu na Soga

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Mungu ajaalie "mifumo ya uendeshaji" ndege zetu isitokee.

Watanzania ni bogus sana, utakuta maereva waliamka na pombe, wa kichwa cha mbele anaenda Dodoma wa kichwa cha nyuma anaenda Dar.

Hakuna cha "hitilafu" wala nini kwenye mifumo ya uendeshaji, ni uzembe tu.
 
Chombo ni kipya, mitambo ya umeme ni mipya, na umeme upo. Nadhani juzi TANESCO walisema tunakimbia na ziada, na maji pia, kama ilivyosemwa na DAWASCO siku tatu zilizopita. Lakini leo, Jumapili, maji yamekata!😂
 
Mwanzo ni mgumu ndugu zangu! Tuwe wavumilivu kila kitu kitakaa sawa. Kumbukeni hatujwahi kuwa nazo treni hizi kabla.
Serikali isingekua na nia ya kuwasaidia wasafiri hasa katika upunguzaji wa ghalama, wasingejenga hii reli. Miundombinu yoyote inayojengwa hailengi kumkomoa mwananchi bali kumsaidia.
Ni vyema kutoa mawazo chanya kuliko kupopoa. Kumbukeni ni mali zetu wenyewe
 
Marekebisho ya kiufundi ?

Kifaa kipya!

Ufundi wa nini ???

Niliishi Brooklyn, New York. Subway lao limejengwa mwaka wa 1904.

Sijawahi kuona limekata moto.

La kwetu lina miezi miwili unusu. Kila siku linakata moto porini.

Tatizo nini ????
 
Haya ndio madhara ya kufunga ndoa na mwanamke mwenye mtoto!

Madhara ya kujimilikisha Mali chakavu!
 
Binafsi sina lawama hata kidogo na SGR nasafiri kibos sana dar dom

Hayo ni makosa tu ya kibinadamu.
Mimi nasafairi sana na ndege lakini juzi dakika za mwisho nikaambiwa badala ya kuondoka mchana itakuwa jioni sababu ya kiufundi ni kweli unakuwa unakasirika kidogo lakini mwisho wa siku usalama na yanatokea haya lakini ukiuuliza % ngapi inatokea utakuta sio issue kabisa. Tuache kukuza mambo.
 
= gharama

Hivi hizo shule mlienda kusomea ujinga?
 
Kama Boeing 737 max haina mwaka ilianguka Ethiopia,cha kushangaza nini,wanaojua maswala ya mechanics wanalijua hili,a machine is working to include an error.Vipi wale wanaokwenda kwenye anga za juu,chombo ni kipya na siku ya kulunch kinalipuka hewani!tuwe na subira kila kitu kitakaa sawa...
 
Je, inashindikana Nini hilo treni kuvutwa na treni nyingine iliyo nzima ili iweze kufika stesheni na kuruhusu safari zingine za treni kuendelea na shughuli zake kwa mujibu wa ratiba zake? What's wrong about this?
Je, hao Watawala wa huko TRC wanahitaji kuwa na degree ngapi za chuo kikuu ili waweze kulitambua suala hili????
 
Hivi haya matreni yanavyobuma kila siku haiwezekani siku moja yakagongana?
Yani ilo swala nimeshajiuliza mara elf 1...maana inaonesha bado uendeshaji haujakaa sawa.
Hatuombei lakn inatia shaka ipo siku yataleta majanga
 


Nimependa neno “Mchongoko”
 
Yani ilo swala nimeshajiuliza mara elf 1...maana inaonesha bado uendeshaji haujakaa sawa.
Hatuombei lakn inatia shaka ipo siku yataleta majanga
Naam.

Na mimi ni kama wewe. Siombei iwe hivyo, ila najiuliza tu kwa ufanisi huu mbaya, haiwezekani siku signal processing zikaharibika treni lisionekane kwenye system na lingine likaja kwa kasi likaligonga?

Hatuombei, tunafikiria tu.
 
No, ndege ya Boeing 737 Max wakati ilipoanguka huko Ethiopia ilikuwa na umri wa zaidi ya mwaka mmoja, ndege hiyo ilinunuliwa mwaka 2017 na ilianguka mwaka 2019.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…