KERO Treni ya mchongoko Dar-Dodoma imeharibika porini toka saa 2 asubuhi kati ya eneo la Pugu na Soga

KERO Treni ya mchongoko Dar-Dodoma imeharibika porini toka saa 2 asubuhi kati ya eneo la Pugu na Soga

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
Shida ni treni jipya limekwama porini.

Kwa nini mitambo mipya inaharibika haribika ovyo ?

Limekuwa gari la mkaa ?

Hata lori la mkaa halikati moto porini likiwa jipya.

Tulinunua mitambo chakavu ? Kwa nini ma VX yao mapya hayakati moto porini ?
Nani alikuwambia trend ni jipya
 
Imetoka Dodoma saa 12 kamili asubuhi.

Tangu saa mbili asubuhi, treni imekwama. Sasa inaenda saa 7 mchana, na hakuna matumaini ya kuendelea.

Treni iko kilomita 45 kutoka Dar, porini. Wengine wanashuka na kupanda boda; wanaenda wapi, sijui. Tangazo la TRC linasema mafundi wapo kazini.

Chombo ni kipya, mitambo ya umeme ni mipya, na umeme upo. Nadhani juzi TANESCO walisema tunakimbia na ziada, na maji pia, kama ilivyosemwa na DAWASCO siku tatu zilizopita. Lakini leo, Jumapili, maji yamekata!

Abiria wapo, hivyo operesheni na mtaji wa matengenezo vipo.

Tatizo nini?

Wazalendo ndani ya TRC, tafadhali tujulishe kupitia njia zetu za kujuzana. Viongozi watatudanganya. Hawana dini. Waliwahi kusema Rais ametingwa na kazi Ikulu, kumbe ameshanyooka. Na waliongelea msikitini. Astakafullulilah Ladhim.

=====
Ufafanuzi wa TRC soma hapa: TRC yaomba radhi Treni ya Mchongoko Dar-Dodoma kusimama ghafla kati ya Pugu na Soga
Kama treni ni hovyo na mafundi watakuwa kama treni Yao na mkurugenzi wao
 
kama migahawa ya vyakula vya humo kwenye treni hawauzi vyakula kwa sababu ya treni kufika haraka safari yao, basi siombaya ikihalibika polini ili nao wapate riziki.
 
Treni limepona, limeondoka Soga 10 minutes ago.

Hii ni 11 jioni. Limebuma masaa 9, toka 2 asubuhi.

Magari ya mkaa yaliyogoma saa mbili asubuhi yalishaletewa spea kitambo, yameondoka, na yamesha deliver mikaa.

Waliposema itaondoka in one hour ilikuwa saa 7, some 4 hours ago. Walisema uongo!

Sishangai kuongopewa. Kuna siku walisema Rais hajambo kumbe kafa.
 
Mwanzo ni mgumu ndugu zangu! Tuwe wavumilivu kila kitu kitakaa sawa. Kumbukeni hatujwahi kuwa nazo treni hizi kabla.
Serikali isingekua na nia ya kuwasaidia wasafiri hasa katika upunguzaji wa ghalama, wasingejenga hii reli. Miundombinu yoyote inayojengwa hailengi kumkomoa mwananchi bali kumsaidia.
Ni vyema kutoa mawazo chanya kuliko kupopoa. Kumbukeni ni mali zetu wenyewe
Serikali haisaidii wasafiri au raia, inatimiza wajibu wake kwa kutumia kodi za raia kufanya biashara ya usafiri.
 
Mbona hata ma bus nayo huwa yanapata break down, vyombo vya moto kupata breakdown ni jambo la kawaida sana, kama wwe vile binaadamu kuumwa ni jambo la kawaida sana! Kanaumwa katoto kachanga ambako ndiyo binaadamu mpya huyo,itakua sembuse kitu cha mchongokoo!!
Treni sio sawa na bus.
 
Acha mawazo hasi mkuu....Wanawasiliana mara nyingi pale Gwara aliembele anamsubiri mwenzake apite kwanza
Haya si mawazo hasi, ni mawazo ya uhalisia. Watu kila siku chache treni linabuma, kwa nini kufikiri kuwa inawezekana siku treni zikagongana iwe ni mawazo hasi?
 
Wabongo tumejaa lawama sana;

Usafirishaji sio kitu perfect; inatokea kwenye Meli, kwenye ndege, kwenye mabasi n.k. Flights zinakuwa rescheduled kwa sababu mbali mbali mara kwa mara na maisha yanaendelea.

Nadhani Ingekuwa treni sio mali ya serikali wala usingelaumu. Shida ni kuwa ni ya serikali na waafrika wengi hawazipendi serikali zao.
 
Mkuu jikite kwenye hoja nini shida!!

Maana umeongea vitu vingi kwa wakati mmoja tukujibu kipi sasa,

Kilichokwamisha safari yako ni hiyo SGR lakini ni kama una mambo mengi kichwani, lawama ni nyingi kuliko kilichokukwamisha.
Kitu ambacho sijawahi kukielewa ni hii treni kuiita SGR ,ambayo ni kirefu cha Standard Gauge Rail... yaani hata media unasikia treni ya SGR yapata changamoto, really??
 
Back
Top Bottom