Treni ya Mizigo iliyobeba Kemikali yapinduka Morogoro

Treni ya Mizigo iliyobeba Kemikali yapinduka Morogoro

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1670169778505.png

Mabehewa 22 ya Shirika la Reli Tanzania na Zambia (TAZARA) yamedondoka mkoani Morogoro yakiwa na kemikali tani 1,099 za Sulphur Dioxide.

Wataalamu kutoka katika mamlaka mbalimbali za serikali wapo katika jitihada za kudhibiti madhara ya kemikali hizo kwa binadamu na wanyama baada ya treni hiyo kupata ajali katika eneo la Lumumwe, Halmashauri ya Mlimba wilayani Kilombero ikitokea Dar es Salaam kuelekea Zambia.

Mkuu wa kitengo cha Usalama Shirika la Reli Tazara nchini Tanzania anayesimamia Kituo cha Mlimba Amani Mboliko amesema ajali hiyo imetokea baada ya hitilafu katika mfumo wa breki, na hivyo injini ilishindwa kuvuta behewa zote na kuifanya irudi nyuma kwa zaidi ya kilometa nane na kusababisha mabehewa yote kuanguka.

Meneja Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali Kanda ya Kati, Gerald Merinyo anasema tayari jitihada za kuhakikisha kemikali yote iliyomwagika inaondolewa zinaendelea kufanyika kupitia wataalamu mbalimbali.

HABARI LEO
 
Moro
Mabehewa 22 ya Shirika la Reli Tanzania na Zambia (TAZARA) yamedondoka mkoani Morogoro yakiwa na kemikali tani 1,099 za Sulphur Dioxide.

Wataalamu kutoka katika mamlaka mbalimbali za serikali wapo katika jitihada za kudhibiti madhara ya kemikali hizo kwa binadamu na wanyama baada ya treni hiyo kupata ajali katika eneo la Lumumwe, Halmashauri ya Mlimba wilayani Kilombero ikitokea Dar es Salaam kuelekea Zambia.

Mkuu wa kitengo cha Usalama Shirika la Reli Tazara nchini Tanzania anayesimamia Kituo cha Mlimba Amani Mboliko amesema ajali hiyo imetokea baada ya hitilafu katika mfumo wa breki, na hivyo injini ilishindwa kuvuta behewa zote na kuifanya irudi nyuma kwa zaidi ya kilometa nane na kusababisha mabehewa yote kuanguka.

Meneja Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali Kanda ya Kati, Gerald Merinyo anasema tayari jitihada za kuhakikisha kemikali yote iliyomwagika inaondolewa zinaendelea kufanyika kupitia wataalamu mbalimbali.
View attachment 2435822
Morogoro again? Watz wangejua inakouzwa leo tena tungeshuhudia watu wakiungua sana.
 
Hii ni onyo na tahadhari kwenye SGR...mambo ya sijui vichwa vya mchongoko ni vya safari fupi na vya zamani full kazi ndoige mtu kazi tutakua kulaumiana huko baadae.
 
Poleni sana hiyo bara bara naijua ina matuta sana, nashauri shirika la reli wapunguze matuta
 
Sulphur Dioxide niliiona imemwagika kutoka kwenye Lori pale Chalinze pembeni yake akinamama lishe wakiendelea na shughuli zao kama kawaida.
 
Kwa Bei ya Jana tar 3/12/2022
KWA soko la hapa hapa tanzania

Kilo Moja ya sulphur dioxide
-ya unga- 236 USD= 545,000 TSH
-Ya mawe - 226 USD= 520,000 Tsh

Nawaza upotee na Lile pipa Moja tu la kilo 100 utakua Bei gan hapo ukiuza Bei ya hasara Chap chap[emoji848]
 
Kwa Bei ya Jana tar 3/12/2022
KWA soko la hapa hapa tanzania

Kilo Moja ya sulphur dioxide
-ya unga- 236 USD= 545,000 TSH
-Ya mawe - 226 USD= 520,000 Tsh

Nawaza upotee na Lile pipa Moja tu la kilo 100 utakua Bei gan hapo ukiuza Bei ya hasara Chap chap[emoji848]

Unamuuzia nani?
 
Haya mashirika watu wanapiga hadi wanajisahau.....reli service mbovu, treni zenyewe service mbovu......waafrika tumelaaniwa
Ndege ambazo zinabeba viongozi na wenye hela zimenunuliwa mpya.
Leo wananchi wanyonge wanaletewa treni mtumba. Nchi hii tajiri, treni mtumba?
Leo Mwigulu yupo singida kaenda kuzindua mradi wa maji halafu bado tunataka battle na wazungu. Tutauweza muziki wao?
Miaka 50+ ya uhuru tunahagaika na maji, madarasa, choo na umeme wa mgao halafu unasema nchi tajiri?
 
Back
Top Bottom