Treni za abiria hazina bima? Wahanga wa ajali ya Dodoma wanaweza idai serikali fidia?

Treni za abiria hazina bima? Wahanga wa ajali ya Dodoma wanaweza idai serikali fidia?

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Joined
Jan 31, 2021
Posts
9,189
Reaction score
16,128
Nimesikia wahanga wa ajali ya Precision Air watalipwa fidia, pesa nyingi. Nimekumbuka ajali ya treni Dodoma miaka ishirini iliyopita. Hivi treni huwa inakata bima? Wahanga wa ajali ile wanaweza dai fidia?
 
Nataka kujua kwanza kwani wanaolipa fidia ni serikali? Ajali ya ndege imetokea ila ni kampuni ya serikali? Au sijaelewa
Ina maana ingekuwa ni ndege ya ATCL kungekuwa hakuna fidia kwasababu ni ya serikali.?
Anataka kujua kama abiria wa ajali ya treni walilipwa fidia?
Mi naongezea na wale wa Meli zanzibar na MV bukoba ilikuaje?
 
Unakurupuka sana, mleta mada anaongelea malipo ya bima. Iwe chombo binafsi au cha serikali vyote hukatiwa bima
Sijakurupuka sasa hajaeleza specific ndio maana nikamuuliza afafanue. Rudi uangalie nilichouliza

Kwa ajali ya Dodoma 20 years ago, watu walipwe na nanI ? Serikali?
 
Ina maana ingekuwa ni ndege ya ATCL kungekuwa hakuna fidia kwasababu ni ya serikali.?
Anataka kujua kama abiria wa ajali ya treni walilipwa fidia?
Mi naongezea na wale wa Meli zanzibar na MV bukoba ilikuaje?
Demi I just asked a question, who is supposed to pay please stop jumping on me so hard😬

Hii ni elimu mpya kwetu.
 
13 November 2022
Songwe, Tanzania

AJALI SONGWE, GARI LAGONGA TRENI LA MIZIGO, ABIRIA WANUSURIKA KIFO..


Abiria kadhaa wamenusurika kifo, baada ya gari walilokuwa wakisafiria, lenye namba za usajili T388 DUS kuligonga treni la mizigo katika makutano ya Barabara Kuu ya Tanzania na Zambia (Tanzam) katika eneo la Songwe mkoani Songwe, tukio lililotokea jioni ya Novemba 13, 2022. Picha za video kutoka eneo la tukio, zinalionesha treni ya mizigo ikiwa imepinduka baadhi ya mabehewa na kufunga barabara hiyo
Source : Global TV Online
 
Hayana Bima ndio, lakini kuna utaratibu maalum wa kufuata linaposababisha hasara kwa maisha au mali, fungu hutoka hazina.
Ishu ni kwamba hayana bima na sivyo alphonce.NET alivyokoment kwenye post #4.
Pamoja na, utaratibu huo kuwepo sijawahi kusikia mfanyakazi wa serikali, au abiria aliyepata ajali kwenye gari ya serikali, amelipwa kama fidia kwa utaratibu huo
 
Nimesikia wahanga wa ajali ya Precision Air watalipwa fidia, pesa nyingi. Nimekumbuka ajali ya treni Dodoma miaka ishirini iliyopita. Hivi treni huwa inakata bima? Wahanga wa ajali ile wanaweza dai fidia?
Treni ni za serikali, serikali ililifilisi shirika lake la bima likabaki kama Kinyago, Magufuli akalipa mtaji.

Hadi leo nashangaa kwanini magari ya serikali hayakatiwi bima
 
Nataka kujua kwanza kwani wanaolipa fidia ni serikali? Ajali ya ndege imetokea ila ni kampuni ya serikali? Au sijaelewa
Vyombo vyote vinavyosafirisha abiria vinatakiwa kukata bima, vya serikali na vya watu binafsi. Juzi nimesikia ATCL wanalipa 5m dollars kama bima. Ninauliza kama treni hizi za serikali zinalipiwa bima na iwapo wale wahanga wa ajali ya treni ya Dodoma wanastahili kulipwa fidia?
 
Ina maana ingekuwa ni ndege ya ATCL kungekuwa hakuna fidia kwasababu ni ya serikali.?
Anataka kujua kama abiria wa ajali ya treni walilipwa fidia?
Mi naongezea na wale wa Meli zanzibar na MV bukoba ilikuaje?
Ahsante kwa kuongezea hapo.
 
Treni ni za serikali, serikali ililifilisi shirika lake la bima likabaki kama Kinyago, Magufuli akalipa mtaji.

Hadi leo nashangaa kwanini magari ya serikali hayakatiwi bima
Usikute wanadhani pesa za bima ni za kutafuna. Watu bwana. Treni za serikali kama hazina bima zisiruhusiwe kubeba abiria.
 
Back
Top Bottom