Tribute to Halima Mchuka: Alikuwa Mtu wa Watu!

Tribute to Halima Mchuka: Alikuwa Mtu wa Watu!

Pasco,

Pole kwa msiba wa Halima Mchuka, naamini kwa namna ulivyoishi naye umekuwa sehemu ya familia yao.

Mimi namkumbuka nikimsikia akirindima redioni RTD kwenye vipindi vya michezo na hatimaye akitangaza mpira wa miguu.

Ni mwanamke wa kwanza kupata kumsikia akiandaa vipindi vya michezo na kubwa kuliko yote alikuwa ni mwanamke pekee niliyepata kumsikia akitangaza mpira wa miguu "live" kutoka viwanjani. Mara ya mwisho kumsikia akitangaza mpira ilikuwa michuano ya kombe la tusker, wakati huo ikishirikisha vilabu vya Tanzania pekee.
Mwita Maranya, ni kweli nimetokea kuwa sehemu ya familia yao. Kiukweli enzi za RTD shift ngumu ilikuwa ni kupambazua, mtu wa kupambazua alifuatwa kwake saa 9 usiku, sasa inapotokea amekosekana, madereva humfuata Halima kwa vile kwake ni karibu na alishika shift za watu bika kinyongo wala kukereka na baada ya hapo aliendelea na kazi zake kama kawaida wakati ukipambazua unaondoka saa 4 asubuhi na kesho yake unakuwa off!.
 
Tujihadhari na ukimwi wakuu.

Mkuu mwita sentesi yako ni tata,sijaelewa hapa unatukumbusha kwamba tujiadhari na ukimwi kama ujumbe kwetu au inahusiana na mada hii inayochangiwa? Kama ni ujumbe kwetu kwanini usingeanzisha sredi yake mpake uiweke kwenye sredi ya pascal? Au kama inausiana na sredi hii kwanin usifunguke moja kwa moja? Hii ni mara ya pili unafanya hivyo ya kwanza ushawahi changia hivi kwenye sredi ya kifo cha mr.ebbo.
 
Nilisikiliza leo asubuhi Malin hassan akiongelea hilo swala na shaban kisu,simfahamu kwa sura but nakumbuka vipindi vyake
 
Pasco.

Pole kwa msiba mzito.Baada ya kusoma bandiko lako mara moja nikapata picha Halima Mchuka alikuwa mtu wa namna gani.

Sina uhakika sana ila nahisi Halima Mchuka na wewe hamtoki mkoa mmoja wala si waumini wa dini moja kama ndivyo basi shukrani za mwanzo ziende kwa Baba wa Taifa letu changa Mwl J K Nyerere ambaye alijitahidi katika uongozi wake wote kutufanya waTanzania wamoja.Alipiga vita ukabila,alipiga vita udini vitu hivi viwili alifanikiwa sana na pengine ndiyo maana Da Mwajuma alikuwa mwepesi sana kukukaribisha Ilala Flat bila kujali kabila lako au dini yako aliutazama uTanzania wako.

Mkuu Pasco nimeanza mbali kidogo si bahati mbaya ila nimeona niwakumbushe viongozi wetu hasa wanasiasa wanaotafuta madaraka kwa msingi wa ukabila ama udini waache mara moja watanzania tumeishi na tunaishi kwa upendo yamkini mfano wako unawakilisha mifano mingi jinsi wananchi tusivyo na huu upuuzi wa ubaguzi.


Mkuu Pasco pole sana hakika umeondokewa na mtu muhimu sana katika maisha yako.
Mkuu Ngongo ni kweli, ni kweli hatukua dini moja wala kabila moja na nilikaribishwa kwao.

Ni kweli heshima kwa Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere kuwezesha watu wa makabila tofauti kuishi pamoja kama ndugu na kusaidiana zaidi ya ndugu!.

Japo mimi ni Mkiristu wa RC, nilipokaribishwa nami nilimkaribisha rafiki Muislamu, Aboubakar Liongo na tuliishi kama ndugu. Wakati wa mwezi Mtukufu wenzangu walifunga, wakati wa kufuturu nilikaribishwa nikafikia wakati hata kula home naona noma mpaka nikaja kujikuta na mimi nafunga kiukweli na kufuturu kiukweli na hata mambo ya ujana kipindi cha mwezi Mtukufu ilikuwa no!.

Hawa wamekuwa nibzaidi ya ndugu, nilipopata ajali, Da Mwajuma alijitoa sana by then Halima alishapata stroke!.

Baada ya ajali yangu na matibabu ya Afrika Kusini na India kutoketa matokeo mazuri, Abou nae alinikaribisha Ujerumani kujaribu maana hao ni mabingwa wa tiba. Huu ni uthibitisho wa upendo wa dhati kwa sisi Watanzania bila kujali dini wala makabila yetu.

Asante Ngongo!.
 
Hakuna mwenye picha ya Halima kuwakumbusha watu? Mayalla bila shaka utabandika hapa. Japo umekataa RIP, wewe mwenyewe umesema RIP. Kumbe Rip haina hati miliki. Kwa kuwa Halima alikuwa mtu wa watu, usiwazuie watu wanapomtakia kheri mahali pema peponi yule mtu wao!

RIP Halima Mchuka.
 
Mkuu Pascal nakupa pole kwakuwa huu msiba ni wako.

Namkumbuka sana Marehemu akitanganza mpira enzi hizo. Nakumbuka nilimwona mara kwa mara akija Mwenge kijijini na watangazaji wenzake Eshe Muhidini na Nadhiri Mayoka kumtembelea rafiki yake Nadhir aitwaye Nuru. Enzi hizo kumwona mtangazaji ni sawa na kuuona Mwenge wa uhuru....adimu sana!........ Nakumbuka nawe mkuu ulikuwa unakatiza maeneo ya mwenge.... ikasemekana ulikuwa ukimchumbia binti mmoja hivi ambaye ana ndugu zake hapo Mwenge.....(sorry kwa hii ofu topiki)

Mungu aendelee kumweka mahali pema peponi Amen.
 
Nilishtuka sana leo asubuhi niliposikia habari za msiba wa Halima! Pascal Mayalla pole kwa huu msiba kutokana na hayo uliyoyasimulia hapa!
Nakumbuka nilimuona mara ya kwanza pale studio za RTD (wakati huo), 1995, nilienda kupeleka tangazo la kupotelewa na ndugu yangu! Alikuwa wameketi ofisini na Idd Rashid Mchatta (R.I.P. waliitana shemeji), nilipowaelezea tatizo lililonipeleka.

Kwa kweli walinisikitikia sana na pia kunisaidia kutoa tangazo lile! Lakini baada ya miaka kama 6, nilifahamiana na mzazi mwenzie (Baba Yekini), ambaye baadae kwenye 2005 au 2006 miezi michache kabla hajapata stroke tulikuwa namkakati wa kuanzisha NGO tukiwa wanne (Baba Yekini, Mimi, Halima na mtangazaji mwingine wa kike wa RTD, sikumbuki jina lake).

Bahati mbaya sana Halima akapata stroke, hivyo project yetu ikafa, maana yeye ndiye alikuwa muhusika mkuu! Niungane na wale wanaomfahamu/waliomfahamu kukumbuka umahiri wake kutangaza mpira na vipindi vingine vya redio.

Halafu nakumbuka Halima alipata stroke kipindi kama hiki (December) na amefariki December! Sijui alizaliwa na kuolewa December? Just thinking loudly!

Nimefahamishwa kuwa msiba upo Mbezi Beach kwa dada yake (Sina uhakika kama ni Da Mwajuma) karibu na flats za BOT. Mazishi ni kesho saa kumi jioni kwenye makaburi ya mamwinyi Msasani! Bwana alitoa na Bwana ametwaa,

Jina lake Lihimidiwe! Amen.
 
Halima , nilikutana nae mara ya kwanza baada ya kuacha kazi pale IFM na nilipoajiriwa na National Audit kama mkaguzi wa Nje nikawa attached pale RTD , kwakweli mimi ndio niliejigonga kwake, kwakua alikua bado binti na wakati huo alikua amejizolea sifa lukuki kama mtangazaji wa mpira wa kike, oooh Pumzika kwa Amani dada wa kutabasam , ulio waacha nyuma watakukumbuka kama ambavyo nakukumbuka.
400125_10150501978789233_791934232_8536867_2035417094_n.jpg
 
Update 1.
Msiba wa Halima Mchuka, upo nyumbani kwa dada yake mkubwa Mwajuma Mchuka, Mbezi Beach nyuma ya maghorofa ya BOT.

Mazishi ni kesho saa 5 asubuhi katika makaburi ya Msasani. Mwili utaswaliwa katika msikiti wa Msasani kabla ya swala ya Ijumaa.

Chanzo cha kifo ni shinikizo la damu. Jana mchana alitangaza kipindi cha salaam za mchana TBC-Taifa na inasemekana alitangaza vizuri ajabu!. Kitu cha ajabu jana aliwatumia sms wanae wawili waliopo nchini, na kuwaambia wamsikilize akitangaza akawaambia na muda. Masikini kumbe ndio kama kuwaaga kiaina kwa kuwaambia waisikilize sauti yake kwa mara ya mwisho!. Mara baada ya **** kipindi ndipo pressure ikampanda, akakimbizwa pale Dar Group na baadae Hospitali ya Taifa ya Muhimbili mauti yalipomkuta!.
 
Nilishtuka sana leo asubuhi niliposikia habari za msiba wa Halima! Pascal Mayalla pole kwa huu msiba kutokana na hayo uliyoyasimulia hapa!
Nakumbuka nilimuona mara ya kwanza pale studio za RTD (wakati huo), 1995, nilienda kupeleka tangazo la kupotelewa na ndugu yangu! Alikuwa wameketi ofisini na Idd Rashid Mchatta (R.I.P. waliitana shemeji), nilipowaelezea tatizo lililonipeleka. Kwa kweli walinisikitikia sana na pia kunisaidia kutoa tangazo lile!

Lakini baada ya miaka kama 6, nilifahamiana na mzazi mwenzie (Baba Yekini), ambaye baadae kwenye 2005 au 2006 miezi michache kabla hajapata stroke tulikuwa namkakati wa kuanzisha NGO tukiwa wanne (Baba Yekini, Mimi, Halima na mtangazaji mwingine wa kike wa RTD, sikumbuki jina lake).

Bahati mbaya sana Halima akapata stroke, hivyo project yetu ikafa, maana yeye ndiye alikuwa muhusika mkuu! Niungane na wale wanaomfahamu/waliomfahamu kukumbuka umahiri wake kutangaza mpira na vipindi vingine vya redio. Halafu nakumbuka Halima alipata stroke kipindi kama hiki (December) na amefariki December!

Sijui alizaliwa na kuolewa December? Just thinking loudly!

Nimefahamishwa kuwa msiba upo Mbezi Beach kwa dada yake (Sina uhakika kama ni Da Mwajuma) karibu na flats za BOT. Mazishi ni kesho saa kumi jioni kwenye makaburi ya mamwinyi Msasani! Bwana alitoa na Bwana ametwaa, Jina lake Lihimidiwe! Amen.
Asante zaratustra, pole na wewe!.

Hili na mazishi nadhani wamebadili muda, nimetoka hapo nyumbani saa 7 hii, mazishi ni kabla ya swala ya Ijumaa
 
Mkuu Pascal nakupa pole kwakuwa huu msiba ni wako.

Namkumbuka sana Marehemu akitanganza mpira enzi hizo. Nakumbuka nilimwona mara kwa mara akija Mwenge kijijini na watangazaji wenzake Eshe Muhidini na Nadhiri Mayoka kumtembelea rafiki yake Nadhir aitwaye Nuru. Enzi hizo kumwona mtangazaji ni sawa na kuuona Mwenge wa uhuru....adimu sana!........ Nakumbuka nawe mkuu ulikuwa unakatiza maeneo ya mwenge.... ikasemekana ulikuwa ukimchumbia binti mmoja hivi ambaye ana ndugu zake hapo Mwenge.....(sorry kwa hii ofu topiki)

Mungu aendelee kumweka mahali pema peponi Amen.
Asante Asprin, pole na wewe, Nadhir Mayoka ni RIP, Eshe Muhidin yuko Doha amejiunga na Aljazeera Swahili, na Nuru, mtoto wa Dr. Omar amehamia Marekani jumla na familia yake!.

Hayo mengine umenikumbusha mbali!, usijali.
 
Update 1.
Msiba wa Halima Mchuka, upo nyumbani kwa dada yake mkubwa Mwajuma Mchuka, Mbezi Beach nyuma ya maghorofa ya BOT.

Mazishi ni kesho saa 5 asubuhi katika makaburi ya Msasani. Mwili utaswaliwa katika msikiti wa Msasani kabla ya swala ya Ijumaa.

Chanzo cha kifo ni shinikizo la damu. Jana mchana alitangaza kipindi cha salaam za mchana TBC-Taifa na inasemekana alitangaza vizuri ajabu!. Kitu cha ajabu jana aliwatumia sms wanae wawili waliopo nchini, na kuwaambia wamsikilize akitangaza akawaambia na muda. Masikini kumbe ndio kama kuwaaga kiaina kwa kuwaambia waisikilize sauti yake kwa mara ya mwisho!. Mara baada ya **** kipindi ndipo pressure ikampanda, akakimbizwa pale Dar Group na baadae Hospitali ya Taifa ya Muhimbili mauti yalipomkuta!.

Duh! Mungu amlaze pema na awampe nguvu wote walioguswa na msiba huu.

Kifo cha ghafla hivi, kinahuzunisha mno
 
Ingawaje sijawahi kusikia hata saauti yake wakati wa kutangaza RTD, Jina lake si geni kwangu Mungu ametoa na Mungu ametwaa jinala la Bwana libarikiwe
poleni wote wafiwa Mungu awape faraja yake na nguvu pia
 
Mimi niliwahi kumsikia akitangaza mpira,kama jana alitangaza kwa kweli inauma sana.Halima tutakukumbuka kwa sauti uliotuachia
 
Inna Lillah Waina Illahi Rajoon


“Ewe Mwenyezi Mungu msamehe Halima Mchuka na ipandishe daraja yake katika walioongoka, na weka badili yake kwa aliyowacha nyuma na utusamehe sisi na yeye, ewe Mola wa viumbe vyote na umkunjulie yeye katika kaburi lake na umtilie mwangaza ndani yake”

“Sisi ni wa
Mwenyezi Mungu nasi Kwake tutarejea, Ee Mwenyezi Mungu Walipe wafiwa kwa msiba huu na uwape badili yake bora kuliko huo”
 
Ahsante marehemu halima kwa yote pia msiba wako kutudhihilishia kuwa Pasco ndio Pascal Mayalla!!
Bulesi, kumfananisha member yoyote wa jf na jina lolote ni kosa la name calling na adhabu yake ni ban!.
 
Back
Top Bottom