Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,872
- 34,363
Luhaga Mpina: Trilioni Zetu 360 Zipo Wapi? Bunge zima linapiga makofi kwa Trilioni 1.3.
"Tunazo trilioni 360 zimeshikiliwa na Mahakama uamuzi haujatoka, nilitegemea kwenye mpango hapa isemwe hela hizo ziko wapi. Leo bunge zima linapiga makofi kwa Trilioni 1.3 tulizopewa na IMF mpaka mikono inauma!
"Bunge halijaumia, Serikali haijaumia, kama tatizo ni Bodi za Rufaa za Kodi kukosa wataalamu, si waajiriwe wataalamu kutoka nje?
"Tuna kampuni 504 yenye miamala zaidi ya Trilioni 105 kwa mwaka, uwezo wa TRA kukagua makampuni haya ni 1% kwa mwaka, hawana wataamu wala fedha na hawezi kukagua, hivyo hatuwezi kupata kodi kwenye makampuni haya, fedha za Watanzania zinapotea.
"Haya yote hatuoni kama ni shida wala hatupati hasira katika hili, lakini tukiletewa hata bilioni 5 hapa tunafurahi kwelikweli. Nilitegema hata mikataba mibovu na ya kinyonyaji nchini kama ya TRA na SICPA ingezungumzwa Bungeni kuwa inaenda kufutwa mara moja na hivyo kusadia kupata mapato mengi ya serikali.
"TR anasimamaia Mashirika ya Umma 237 ambayo yanategemea ruzuku kutoka Serikalini, hayana mtaji na hayatekelezi majukumu yake sawa sawa. Kwanini mpango hauzungumzii juu ya kuyapatia mtaji mashirika haya ili yafanye biashara serikali iweze kupata gawio kubwa, hela zinazopelekwa kwa ajili ya ruzuku zifanye mambo mengine?
"Msajili wa Hazina anaweza kusimamia makapuni haya kwa 13% tu, hana fedha wala watalaamu, lakini sisi tunaona kukaa na kupanga ni sawa lakini hatufanyii kazi suluhisho la matatizo haya.
"Bado tuna maeneo mengi yenye utoroshaji mkubwa wa fedha, ukienda mipakani madini bado yanatoroshwa, mifugo, mazoa ya uvuvi, misitu na hata wanayama pori bado wanatoroshwa. Mpango unatueleza nini, unaenda kudhibiti vipi maeneo haya ili tuzidi kupata mapato?"
"Tunazo trilioni 360 zimeshikiliwa na Mahakama uamuzi haujatoka, nilitegemea kwenye mpango hapa isemwe hela hizo ziko wapi. Leo bunge zima linapiga makofi kwa Trilioni 1.3 tulizopewa na IMF mpaka mikono inauma!
"Bunge halijaumia, Serikali haijaumia, kama tatizo ni Bodi za Rufaa za Kodi kukosa wataalamu, si waajiriwe wataalamu kutoka nje?
"Tuna kampuni 504 yenye miamala zaidi ya Trilioni 105 kwa mwaka, uwezo wa TRA kukagua makampuni haya ni 1% kwa mwaka, hawana wataamu wala fedha na hawezi kukagua, hivyo hatuwezi kupata kodi kwenye makampuni haya, fedha za Watanzania zinapotea.
"Haya yote hatuoni kama ni shida wala hatupati hasira katika hili, lakini tukiletewa hata bilioni 5 hapa tunafurahi kwelikweli. Nilitegema hata mikataba mibovu na ya kinyonyaji nchini kama ya TRA na SICPA ingezungumzwa Bungeni kuwa inaenda kufutwa mara moja na hivyo kusadia kupata mapato mengi ya serikali.
"TR anasimamaia Mashirika ya Umma 237 ambayo yanategemea ruzuku kutoka Serikalini, hayana mtaji na hayatekelezi majukumu yake sawa sawa. Kwanini mpango hauzungumzii juu ya kuyapatia mtaji mashirika haya ili yafanye biashara serikali iweze kupata gawio kubwa, hela zinazopelekwa kwa ajili ya ruzuku zifanye mambo mengine?
"Msajili wa Hazina anaweza kusimamia makapuni haya kwa 13% tu, hana fedha wala watalaamu, lakini sisi tunaona kukaa na kupanga ni sawa lakini hatufanyii kazi suluhisho la matatizo haya.
"Bado tuna maeneo mengi yenye utoroshaji mkubwa wa fedha, ukienda mipakani madini bado yanatoroshwa, mifugo, mazoa ya uvuvi, misitu na hata wanayama pori bado wanatoroshwa. Mpango unatueleza nini, unaenda kudhibiti vipi maeneo haya ili tuzidi kupata mapato?"