Trucks and truckers special thread. Uzi maalum kwa wadau wa magari ya mizigo na wasafirishaji

Trucks and truckers special thread. Uzi maalum kwa wadau wa magari ya mizigo na wasafirishaji

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2009
Posts
76,107
Reaction score
160,001
1599480292338.png
Sekta ya usafirishaji wa mizigo kwa kutumia magari (malori) ni muhimu sana hapa nchini na duniani kwa ujumla. Magari ya mizigo yanafika jirani zaidi na mlaji wa mwisho au sokoni ambako meli, reli na ndege haviwezi kufika.

Uzi huu ni mahususi kwa kupeana taarifa mbalimbali kuanzia kwenye upatikanaji wa mizigo, mbinu za kukuza biashara, hali ya usalama barabarani na mengine mengi ya manufaa kwenye sekta hii adhimu.

Leo naomba niwapeni changamoto kidogo, ili tuweze kubadili our mindset. Hakuna prejudice kwa haya ninayoyasema lakini facts ziko wazi na kwa hizi facts tunaweza kujua tatizo liko wapi.

Kwa nini Tanzania some transporters wa kitanzania (wazungu, wahindi, waarabu, wasomali) wanafanya vizuri sana kwenye trucking business lakini indigenous Tanzanians wana struggle? Why GSM, TRH, AZAM, ZHP, ALISTAIR, ASAS, SIMBA TRUCKING etc wanafanya vizuri sana na wame-build fleet kubwa sana most of them up to 500 trucks and the others fail?

DISCIPLINE.
 
Ni kweli unayosema Displine, Displine kwenye transportation wamiliki wengi hawana. Unajua biashara ya gari ni kama kamari yani leo unapata nyingi na kesho inaweza ikachukua hela yote na ya akiba. Sasa wamiliki hawapendi na wakipata pesa hawaweki kwahiyo magari yanaharibika na tairi zinaisha, ikifika service mtu anashindwa kufanya hivyo hivyo mdogo mdogo gari linatembea kwa shida mpaka linakufa maana siku ukiamua kutengeneza huna pesa kabisa. Hao wenzetu usimamizi wa hali ya juu, madereva wapo well trained, magari yanatengenezwa wataacha kufanikiwa.

Kwa HansPop yenyewe ukiingia nae mkataba mpaka aipitishe gari yako yani uwe umefuzu vigezo vyote na hao madereva wako lazima wawe trained hata mwezi mzima mpaka waelewe. Haruhusiwi Dereva kuanza safari bila kuwa na uhakika yupo vizuri. Halafu gari linaenda kwa masaa, usiku hamna kutembea Dereva lazima alale, akitembea tu anapigiwa simu.

Sasa sisi waswahili hizo menejimenti tunaweza kweli? Kwanza Dereva ni mtoto wa kaka, mjomba, shangazi n.k yani hii shughuli ni ngumu ila Kilimanjaro naye anajitahidi mchaga mwenzetu jamani sa hivi anafikisha malori 120 na mabus 36. Kwahiyo tukiamua tunaweza na mdogo mdogo tutafika in shaa Allah. Cha muhimu kujifunza kupitia makosa. Akikosea mwenzio ndio darasa hilo.
 
Ni kweli unayosema Displine, Displine kwenye transportation wamiliki wengi hawana. Unajua biashara ya gari ni kama kamari yani leo unapata nyingi na kesho inaweza ikachukua hela yote na ya akiba. Sasa wamiliki hawapendi na wakipata pesa hawaweki kwahiyo magari yanaharibika na tairi zinaisha, ikifika service mtu anashindwa kufanya hivyo hivyo mdogo mdogo gari linatembea kwa shida mpaka linakufa maana siku ukiamua kutengeneza huna pesa kabisa...
Trucking industry is huge in the country with about 30,000 trucks doing local and cross border business na bado ni eneo ambalo still demand iko high.

If well managed ni moja ya maeneo ambayo investment yako haiwezi kupotea kamwe. Weka bima comprehensive na ya kutosha ; fanya scheduled services on time ; jitahidi upate madereva wazuri; andaa mikataba kwa kila kazi ; fahamu ofisi za watu wanaokodi gari zako ; tengeneza vitabu vya mahesabu na get a good person tu manage the trucks if you cant do it. You will be on course and see your fleet grow !
 
Bujibuji, What do you fore see as an impact of current Improvement of Railway System in Tanzania to Trucks Transport Sector ?
Complementary.
No way the new enhanced railway system will kill road transportation sector.

- Railway system is expensive to roll out everywhere
- There are areas which rail cannot reach
- Railway transport takes long and could be detrimental to some type of goods e.g perishables
- For those wishing quick turn around road is the choice
- Cargo transportation is still very high in demand so multimodal transportation (sea, rail, road) is still critical.

USA and Germany have the best railway systems in the world but trucking is still the highest earning sector in those countries.
 
Dada ambaye truck yake imezama Wami kafilisiwa na dereva, hakupata dereva mzuri
Mafunzo makubwa sana haya Kwenye maisha na bado wapo matransporter wengi hawakati insurance. Hata kazi za local naona ni biashara ngumu sana alikuwa analipwa mil 2 ukitoa mafuta, posho ya Dereva, dharura anaweza kubakiwa na laki tatu tu hapo sasa insurance kubwa atakataje😳 hapo tairi bado halijapasuka duuuh hamna kinachobaki
 
DHANA YA UBEBAJI MIZIGO KWA MUJIBU WA SHERIA ZA TANZANIA Je, sheria inasemaje kuhusu kubeba mizigo? Je, ni kosa kutumia gari langu kubeba mizigo? Kuna sheria mbili tutakazoziangalia hapa, nazo ni Sheria ya Usalama Barabarani sura ya 168 ya sheria za Tanzania, na kanuni za SUMATRA za usafirishaji mizigo za mwaka 2012 KANUNI ZA SUMATRA [TRANSPORT LICENSING (GOODS CARRYING VEHICLE) REGULATIONS 2012 Kifungu cha 2 cha kanuni kinatafsiri gari gari la kubebea mizigo (Goods carrying vehicle) kama gari ambalo limetengenezwa au kufanyiwa mabadiliko kwaajili ya kubebea bidhaa au lililotengenezwa au kurekebishwa kwaajili hiyo. Kanuni hazisemi nini maana ya mzigo.

Nadhani hii inaweza kuwa inatokana na dhana kwamba kila mtu anajua mzigo ni nini. Kwa mujbu wa kanuni ya 3 mtu yeyote mwenye gari ya mizigo kwaajili ya kufanya shughuli ya kubeba mizigo ni sharti awe na leseni ya kubebea mizigo. Kwa mujibu wa kanuni ya 4 leseni hiyo ataipata baada ya kuiomba kutoka SUMATRA.


Kanuni ya 4(2) inataja mahitaji ya vitu ambayo mwomba leseni anatakiwa kwenda navyo SUMATRA ili kupata leseni. Vitu hivyo ni pamoja na kadi ya gari,bima,ripoti ya ukaguzi, majina ya nakala za leseni ya madereva wa magari hayo,picha za mwenye gari, nakala ya mkataba wa dereva. Kwa mujibu wa kanuni ya 7 iwapo mamlaka itaridhika na nyaraka zilizowasilishwa basi itampa leseni mwomba leseni ya kusafirisha mizigo. Muda wa leseni ni mwaka mmoja na inaweza kuhuishwa (renewal) Kwa kuzingatia masharti ya kanuni ya 26, Mamlaka itatoa cheti cha ruhusa ya kuendesha gari kwa dereva atakayeendesha gari hilo.

Cheti hicho kitataja namba ya leseni ya dereva,TIN,tarehe ya kuzaliwa,picha ya dereva,jina na anwani ya dereva, jina la shule ya udereva aliyosomea. Masharti kwa dereva na matendo yaliyokatazwa Kwa mujibu wa kanuni ya 27 dereva atazingatia yafuatayo: (a) Kuendesha kwa spidi iliyokubaliwa; (b) Kutobeba abiria kwenye gari la mizigo; (c) Kutozidisha mizigo kinyume na uzito wa gari husika Kwa mujibu wa kanuni ya 28, dereva anakatazwa:

a) Kutumia lugha mbaya au za matusi kwa wateja (b) Kuwazuia wengine barabarani (c) Kuendesha akiwa na kilevi (d) Kuendesha kwa pupa na kutojali kinyume na sheria ya usalama barabarani (e) Kuegesha gari mahali pasiporuhusiwa (f) Kuendesha gari katika barabara ambazo uzito unaoruhusiwa ni wa chini kuliko ule wa gari (g) Kuwanyanyasa wateja (h) Kutumia simu wakati anaendesha Kushindwa kutekeleza masharti ya kanuni ya 27 na 28 kunaweza kupelekea dereva kupigwa faini ya shilingi laki moja au kifungo cha miezi mitano jela au vyote kwa pamoja.

Hitimisho Kwa ufupi sheria hii inawahusu Zaidi wale wanaomiliki magari kwaajili ya kufanya biashara au shughuli za ubebaji mizigo kwa kutumia magari yaliyotengenezwa maalumu kwaajili ya kubebea mizigo. Na hasa hasa wale wanaofanya bishara kwa kutumia magari hayo. Japokuwa sheria hapa imeweka masharti ya jumla bila kujali kwamba mwenye gari la mizigo anafanyia bishara au la. Kwa mujibu wa kanuni ya 35(1) polisi na maafisa wa SUMATRA wamepewa mamlaka ya kusimamisha magari haya ya mizigo na kukagua iwapo yanatimiza masharti ya kanuni hizi au kukagua leseni ama nyaraka nyingine inayotakiwa kuwemo kwenye gari.

Je, sheria hii inaelekeza lolote kuhusu namna ya kubeba mizigo au aina gani ya mizigo ibebwe? Je, sheria hii inakataza gari fulani kubeba mizigo? Jibu la maswali yote haya mawili ni hapana, sheria hii inajikita kwenye utoaji wa leseni tu au vibali kwaajili ya magari yanayobeba mizigo, na kwamba magari haya yanatakiwa kuzingatia sheria nyingine wakati wa kufanya kazi ya kubeba mizigo, mathalani sheria ya usalama barabarani, sheria ya ubebaji kemikali, nk. SHERIA YA USALAMA BARABARANI, SURA YA 168 (RTA,1973) Hii ndiyo sheria mama ya usalama barabarani.

Kwa mujibu wa kifungu cha 2 cha sheria hii tafsiri ya nini maana ya gari ya mizigo inafanana sana na ile iliyotolewa kwenye kanuni za SUMATRA za magari ya mizigo,2012. Kama zilivyo kanuini za SUMATRA sheria hii haitoa maana ya neno “mizigo au bidhaa” wala hakuna popote, kuanzia kifungu cha 1 hadi cha 118 inapokataza magari ya aina fulani kubeba mizigo.

Je, nini kinachokatazwa au kuelekezwa na sheria hii? [MAMBO AMBAYO DEREVA ALIYEBEBA MZIGO ANATAKIWA KUZINGATIA KWA MUJIBU WA SHERIA] 1. Sheria hii inataka gari lolote, likiwemo la mizigo au tela lake liwe zima, yaani linafaa kwa matumizi ya barabarani kwa mujibu wa kifungu cha 39(1) na (2) ili lisihatarishe maisha ya walimo kwenye gari na watumiaji wengine wa barabara. Kipimo cha ubovu wa gari kwa mujibu wa kifungu cha 39 ni sentensi hii “…not likely to be a danger to the persons travelling on the motor vehicle or trailer or to other users of the road.”

Yaani uendeshaji wa gari husika katika hali liliyopo usiweze kuwa hatari kwa watu wanaosafiri na gari hilo au watumiaji wengine wa barabara.” 2. Kifungu cha 39(3) kinapiga marufuku gari lolote au trela lake kutumika barabarani ikiwa mgawanyo, ufungaji, na urekebishaji wa mzigo uliobebwa unafana gari hilo kuwa hatari kwa watu wanaosafiri na gari hilo au watumiaji wengine wa barabara. [(3) No motor vehicle or trailer shall be used on a road if the distribution, packing and adjustment of the load carried is such as to make it a danger to persons travelling on the motor vehicle or trailer or to other users of the road.] 3. Kifungu cha 39(4) kinaeleza kwamba, kwa minajili ya kifungu kidogo cha 2 na cha 3 cha kifungu cha 39, watu wanaosafiri kwenye gari ni sehemu ya mzigo.

[travelling on a motor vehicle or trailer shall be deemed to be part of the load:] 4. Kifungu cha 39(2) kinapiga marufuku gari kubeba mzigo mkubwa zaidi ya uzito uliowekwa na mtengenezaji wa chesisi ya gari au kuzidisha uzito Zaidi ya ule uliotengenezwa kwa gari husika. Kifungu cha 39A(2), kinataka mzigo wowote uliopakiwa kwenye gari uwe umepangwa na kuzingirwa (secured) vizuri ili kuuzuia mzigo huo: (a) Kuwadhuru watu au kusababisha madhara kwa mali binafsi au ya umma na kuanguka au kuburuzika barabarani; (b) Kuzuia uoni wa dereva au kuathiri uwiano wa gari linapoendeshwa; (c) Kusababisha kelele, vumbi, au kusababisha kadhia nyingine zinazoweza kuepukwa (d) Kufunika taa,indiketa, viakisi mwanga(reflectors), sahani za namba, na alama za nchi ya usajili wa gari, au kuzuia kuonekana kwa alama yoyote inayotolewa kwa mkono.

5. Kifungu cha 39A(3) kila dereva atahakikisha kuwa viunganisha vyote kama vile minyororo,Kamba, waya, na bati zilizotumika kufunga au kuzingira mzigo zimefungwa thabiti kuweza kuushikilia mzigo. 6. Kifungu cha 39A(4) iwapo mzigo uliobebwa umetokeza nyuma au mbele kiasi cha kutoonekana na madereva wengine, dereva atahakikisha eneo hilo lililojitokeza linawekewa alama itakayofanya uonekane. [ hii ndio sababu watu huweka kitambaa chekundu au taa inayowaka na kuzima] 7. Kifungu cha 39A(5), dereva ambaye gari lake limetengenezwa mahsusi kwajili ya kubeba mizigo, anaweza katika mazingira fulani maalumu yaliyoelezwa na sheria hii, kubeba abiria kwenye nafasi iliyowekwa maalumu kwaajili ya mizigo.

[ Hata hivyo katika sheria mama mazingira hayo hayatajwi kinaganaga] Kwa maelezo haya, je gari ndogo za chini ya tani 3.5 ambazo hazikutengenezwa kwaajili ya kubeba mizigo mikubwa, kama vile, saloon, station wagon, nk, haziruhusiwi kubeba mizigo? JIBU ni hapana, hakuna popote kwenye sheria panapokataa gari hizo kubeba mizigo, ili mradi tu dereva atakuwa amezingatia msharti ya kifungu cha 39 na 39A cha sheria ya usalama barabarani.

Kwa mantiki hiyo madereva wanaopigwa faini kwa kubeba mizigo ndani ya siti za abiria wa gari ndogo, mfano umebeba boxi mbili zenye laptop kwenye saloon car seat za nyuma, je utakuwa umetenda kosa? Jibu ni hapana utakuwa hujatenda kosa, ili mradi tu mzigo huo umekaa salama kwenye siti husika kiasi kwamba hauwezi kusababisha uione mbele au nyuma kwa kutumia side mirror au driving mirror au windscreen.

Kwa hiyo hataukipigwa faini kosa pale sio kubeba mizigo kwenye gari isiyo ya mizigo bali kubeba mizigo kwa njia ya hatari. Na hatari yenye ni kule kubeba mzigo kiasi kwamba huwezi kuona kwa kutumia vioo vyako, au namba zimefichwa au taa zako zimefichwa au mzigo husika haujafungwa vizuri.

Hitimisho Kwa hiyo hakuna gari inayokatazwa kubeba mzigo ili mradi tu usalama umezingatiwa, kinachokatazwa ni KUBEBA MZIGO KWA NJA YA HATARI au kwa lugha nyingine KUHATARISHA WALIOMO KWENYE GARI AU WATUMIAJI WENGINE WA BARABARA. Ndio maana hizi gari ndogo zina buti au nafasi nyingine kwaajili ya kubebea mizigo. Zipo gari hazina buti ila kwa ndani sehemu ya siti imetengenzwa vizuri kiasi siti zinaweza kukunjwa ikapatikana nafasi ya kuweka mizigo
 
Naomba kuuliza:

Tandam ni nini, na
Kipisi ni nini.

Kwa kiswahili, kwa picha.
 
Tandam(Tandem) ni gari ambayo nyuma ina axle 2 waswahili tunasema double diff. Hill neno tandamu limekuwa likitumika kwenye fuso zile ndefu zenye diffu 2.

Kipisi- Ni gari yoyote ile iwe Scania/Man/Daf/Howo/Schackman yenye uwezo wa kubeba mzigo kuanzia tank 16. Pia kipisi unaweza ukaunga tela lingine(Mtoto) ikawa inavuta hapo tunaita Pulling.

Kiuhalisia ukitumia hata Scania kipisi ni tandamu kutokana na baadhi kuwa na double diff. Neno tandamu tumezoea kutumia kwa Fuso na Isuzu foward.

Picha watatuma wadau uzione
 
Kuna jamaa alinunua puling 2009 akiwa yeye mwenyewe ni dereva.alianza kwa ugumu sana.tairi ananunua za mabasi kisha anafunga nyuma.mafuta ananunua ya magendo. Mpaka sasa ana vipisi 2 na tandam moja na hiyo pulling aliyoanza nayo.ila akipokea simu za madereva ni matusi kwa kwenda mbele.

nilimuuliza kwa nini anatukana sana madereva lakini hawaondoki na hata wakiondoka fasta anapata wengine? Akanambia gari zake ni nzima sana anazingatia sana service na pia anawalipa vizuri madereva mpaka bonas huwa anawapa.
 
Anhaa, Tandamu inaweza kubeba tani 16

Na kipisi umesemq ni gari inayobeba tani 16 kuendelea

Kwa hiyo tandamu ni kipisi?
haaa,,,we jamaa unamaswali tata!!. imezoeleka fuso yenye diff mbili kuitwa tandam kama alivyokuelewesha jamaa hapo juu.

kipisi ni zile scania ambazo hazina tela. Pia kuna kipisi cha volvo,daff,actross n.k
 
Back
Top Bottom