Utam koleaTunasubiri utamu ukolee
Acha kumpamba hana anachojuaVuta pumzi ya kujipongeza mkuu tumetoka mbali sana.
story tellers wangu wa muda wote na wewe umo
cc UMUGHAKA SteveMollel JBourne59 et all
HahaaaaAcha kumpamba hana anachojua
127
Inuka uongeze mkaa kidogo, aliniamuru babu nami nikafanya kadri alivyoniamuru.
Kwahio hata bibi yako nae yupo chini ya amri ya huyu msichana? Sikujua kama huyu msichana ni hatari kiasi hicho na ukimwona huwezi ukamdhania kujihusisha na mambo hayo, nadhani ndio sababu bibi yako anampenda sana huyu mtoto kumbe wanashirikiana, aliongea mfululizo babu huku akionekana kuzama katika fikra nzito.
Ila naona anakupenda sana, kukuonesha siri zake tena za hatari namna ile pamoja na kuwatendea vile washirika wake ili wewe unusurike ni wazi anakupenda mno, alisema babu.
Nilimwuliza babu kuhusu ndoto yangu ya kupaa ambayo nilianza kuiota tangu utotoni, tena mara nyingi hunijia kwenye zile ndoto za kuogopesha sana.
Kabla hajajibu swali langu waliingia wale jamaa walokuwa wanalima, walikuja kujikinga mvua ambayo sasa ilikuwa inachapa vibaya mno.
Vipi rafiki yangu hongo (mapengo) kesho mtamaliza kulima yote? Babu Alimwuliza mmoja kati ya wale jamaa 6 waliokuwa wanalima.
Kesho zidhani babu, majaruba ni makubwa mno!
Mkuu samahani punguza shobo unaponiona.Acha kumpamba hana anachojua
Imeandikwa...waovu hukimbia pasipo kukimbizwa🤣131
Nilishangaa captain msaidizi akianza kuniita mimi upande wake hali iliyopelekea uzuke utani kwa juma kumwambia msaidizi wake kwamba amemuwahi kumwita okwi wake, huku yule msaidizi akisema huyu ni mrisho ngasa.
Baada ya timu kuwa tayari, tulianza kusakata kabumbu huku juma akiwa ameniazimia viatu kwa dogo mmoja aliyekosa namba na kubaki nje kungoja.
Baada ya zoezi tulikusanyika katikati ya uwanja na kupeana mawaidha kama ilivyo kawaida kwa timu za vijijini, nilishangaa kila mtu alikuwa ananitupia macho, wengine walikuwa wanaambizana kwamba huyu dogo akicheza mbele na joji, siku hiyo wale jamaa watakubali mziki.
Juma na wazee kadhaa walitutaka twende tukamwone yule mzee wa jirani na kiwanja kwani alikuwa anaumwa yu hoi kitandani, sikutaka kwenda pale kabisa kwani ni mimi ndio chanzo cha yeye kulala hoi kitandani.
Nilimwita juma pembeni na kumwomba radhi kwamba nisingeweza kwenda pale kwani usiku ulikuwa umeingia hivyo nilitakiwa niwahi nikakoke moto, juma hakuwa na noma aliniruhusu nikaondoka.
Mamaaa!
Kweli nimelala sana leo ngoja nisome😀
Kweli nimelala sana leo ngoja nisome😀