Sehemu ya pili
Nikajrnga ukaribu na majirani wa shangazi yangu na kisha hata kujua baadhi ya watu wanaokwenda kwenye ule mlima na kupata hiyo mercury. Nilithibitishiwa kuwa mercury watu wanaipata na nikapewa majina ya watu ambao wamenufaika na mercury hiyo na kwenda kuishi mjini.
Basi nikajawa na tamaaa na hamasa uwenda nami nikawa mmoja wa wanufaika hao. Nilipeleleza mpaka nikaijua nani mkuu wao.
Nikajipiga kifua siku moja nikamuingia mzee yule. Nikamsemesha kwa kiluguru, namimi niwe miongoni mwa watu watakaokwenda kutafuta mercury iweze kunisaidia, mzee alikataa akaaema hakuna kitu kama hicho wao wanaenda kule kwa shida zao na sio utajiri.
Sikukata tamaa, nikamfuata mwingine ambaye alinielekeze niende kwa yule mzee kwani ndio mkuu wa kikundi hicho cha kimila. Akaniambia fanya subira tu kwa siku moja mbili hautoweza kukubaliwa. Huyu mzee ndio mganga wa hapa kwetu na anatambulika na bibi wa milima ile. Basi siku ya kufuata dawa nitakwambia. Hatusemi mercury ni dawa ndio lugha inayojulikana na bibi wa mlima ule.
Nikaendelea na miangaiko yangu lakini nilikuwa sipungui kijiji kile kuomba ukaribu. Siku akaniambia dawa tutafuata alhamisi ijayo usiku. Ila usimwambie mtu na wala usionekane maeneo ya kijijini muda wa usiku.
Nikamuuliza mnafanyaje? Na hiyo dawa ipo maeneo gani katika mlima? Lengo la hili swali ni kujua formula na kupambana mwenyewe bila woga.
Akasema tunaenda na mzee usiku mkubwa na tunaimba nyimbo pale karibia na pango na kupiga ngoma mpaka bibi atuurize shida zetu. Akasema bibi ndio jini anayelinda mali zile....