True story: Jinsi nilivyopambana kutafuta mali za Mjerumani mkoani Morogoro, mauzauza na vimbwanga nilivyokutana navyo

True story: Jinsi nilivyopambana kutafuta mali za Mjerumani mkoani Morogoro, mauzauza na vimbwanga nilivyokutana navyo

Sehemu ya pili

Nikajrnga ukaribu na majirani wa shangazi yangu na kisha hata kujua baadhi ya watu wanaokwenda kwenye ule mlima na kupata hiyo mercury. Nilithibitishiwa kuwa mercury watu wanaipata na nikapewa majina ya watu ambao wamenufaika na mercury hiyo na kwenda kuishi mjini.
Basi nikajawa na tamaaa na hamasa uwenda nami nikawa mmoja wa wanufaika hao. Nilipeleleza mpaka nikaijua nani mkuu wao.

Nikajipiga kifua siku moja nikamuingia mzee yule. Nikamsemesha kwa kiluguru, namimi niwe miongoni mwa watu watakaokwenda kutafuta mercury iweze kunisaidia, mzee alikataa akaaema hakuna kitu kama hicho wao wanaenda kule kwa shida zao na sio utajiri.

Sikukata tamaa, nikamfuata mwingine ambaye alinielekeze niende kwa yule mzee kwani ndio mkuu wa kikundi hicho cha kimila. Akaniambia fanya subira tu kwa siku moja mbili hautoweza kukubaliwa. Huyu mzee ndio mganga wa hapa kwetu na anatambulika na bibi wa milima ile. Basi siku ya kufuata dawa nitakwambia. Hatusemi mercury ni dawa ndio lugha inayojulikana na bibi wa mlima ule.

Nikaendelea na miangaiko yangu lakini nilikuwa sipungui kijiji kile kuomba ukaribu. Siku akaniambia dawa tutafuata alhamisi ijayo usiku. Ila usimwambie mtu na wala usionekane maeneo ya kijijini muda wa usiku.
Nikamuuliza mnafanyaje? Na hiyo dawa ipo maeneo gani katika mlima? Lengo la hili swali ni kujua formula na kupambana mwenyewe bila woga.

Akasema tunaenda na mzee usiku mkubwa na tunaimba nyimbo pale karibia na pango na kupiga ngoma mpaka bibi atuurize shida zetu. Akasema bibi ndio jini anayelinda mali zile....
Chilita
 
Vile team roho mbaya ya konda msafi inafanya survey kuangalia wapi pa kuanzia!😁😁😁
AEHNYZ.jpg
 
Anataftwa mtu apigwe hapa vibaya mnoo..mi mwenyew nishawai tapeliwa hvyo hvyo maeneo ya machimbon huko sitosahau ***** zao..mara joka kubwa linakula ndege mara mapangoni stori nyiing..mara toa elf 50 tununue dawa hii mara dawa ile..***** kuja kushtukia hzo 40..mara 60 zmefika lak4...nilishtak polisi wale watu askar walicheka sanaaa wakanambia kesi hzo zipo kama 20 hiv..nmepigwa...enz hzo ..*****..
 
Anataftwa mtu apigwe hapa vibaya mnoo..mi mwenyew nishawai tapeliwa hvyo hvyo maeneo ya machimbon huko sitosahau ***** zao..mara joka kubwa linakula ndege mara mapangoni stori nyiing..mara toa elf 50 tununue dawa hii mara dawa ile..***** kuja kushtukia hzo 40..mara 60 zmefika lak4...nilishtak polisi wale watu askar walicheka sanaaa wakanambia kesi hzo zipo kama 20 hiv..nmepigwa...enz hzo ..*****..
Hapana wale wazee ni wakweli kabisa hawakuwa na nia ya kutapeli...naendelea
 
SEHEMU YA 3

Nimeombwa niendeleee japokuwa uko mbele kunatisha kidogo

Basi siku ya alhamisi nikafika kwa kuvizia vizia na kufika jioni watu wachache sana wakaanza kujikusanya. Sikutaka kuona na wafatilia bali siku ile nikaenda karibia na mlima ule na nikajificha mahala ili tu nijue formula za kupata mali.
Ilipofika saa 6 usiku kweli nikaanza kusikia sauti zikielekea mlimani na nyimbo pamoja na Ngoma. Nikathibitisha kuwa ni kweli. Formula yao ya kwanza nimeshaijua.basi sikutaka kuingilia mambo yao ni usiku mkubwa sana. Wakafanya ngoma zao kisha zikazima baada ya nusu saa wakaanza kurudi. Ilikuwa ni saa nane kasoro usiku.
Basi nikajibanza huko msituni mpaka jua likachomoza nikaenda zanu kijijini.
Saa 3 asubuhi nikaonana na mmoja wao ambaye alikuwa aliniambia mara ya kwanza nifanye subira.
Sasa akanifafanulia zaidi....
" tumeenda kuomba dawa, huku usiseme mercury utajua unafata mali, basi ukiwa na madhumuni hayo utapotea polini au kuonana na nyoka mkubwa sana wa kutisha. Huwa tunapika ngoma na kuimba kisha mzee kingalu ambaye ndiye mkuu wetu anasikiluza sauti ya bibi. Bibi huwa anasema mna shida gani? Mzee anajibu wajukuu zako wagonjwa sana tunaomba dawa, bibi anmruhusu aingie na chupa aweke na aje achukue wiki ijayo."
Anasema dawa hiyo inatoka kwa matone madogo sana na baada ya wiki tunapata kijiko kimoja tu ndio tunaruhusiwa kuchukua.

Nilifarijika sana nikapanga jinsi ya kuingia katika mapango hayo

Nitaendelea
 
Umeanza vituko na wewe,hata kitoto kichanga hakiwezi kupost part fupi hivi kama wewe yaani kama ni muvi umesimulia sehemu tu ya sterling kuweka risasi kwenye magazine
Waongo waongo hawa mimi nikiona story itaendelea tu halafu huo mwanzo ni kipisi huwa naachana nayo tu
 
Back
Top Bottom