Trump adai kuna wafungwa wa kutoka Congo DRC wanopelekwa Marekani. Je mambo yapi wanofanya hawa wahalifu huko Marekani?

Trump adai kuna wafungwa wa kutoka Congo DRC wanopelekwa Marekani. Je mambo yapi wanofanya hawa wahalifu huko Marekani?

Richard

JF-Expert Member
Joined
Oct 23, 2006
Posts
15,692
Reaction score
23,038
Mgombea mtarajiwa wa kiti cha uraisi wa Marekani na pia mshtakiwa aletiwa hatiani kwa makosa ya kughushi nyaraka Donald Trump leo ameongea na waandishi wa habari na wafuasi wake katika ofisi zake mjini New York.

Akiongea kwa muda wa dakika zipatazo 40 kuashiria kila kosa alotiwa hatiani kwa makosa yote 34, bwana Trump ametumia muda mwingi kuwashambulia jaji aliesimamia kesi yake na wazee wote wa baraza ambao wamemkuta ana hatia ya kughushi nyaraka za hesabuzake za kulipa kodi.

Bwana Trump atarajiwa kutangazwa kuwa mgmbea uraisi wa chama cha Republican siku mbili baada ya hukumu kutolewa mwezi Julai.

Lakini leo mchana akiongea na wafuasi wae na waandishi wa habari katika jumba lake maarufu kama Trump Tower, bwana Trump ametoa madai ya kuamsha akili pale alipodai kwamba kuna wafungwa kutoka Congo DRC Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambao wamekuwa wakipelekwa Marekani bila kufafanua kwamba wafungwa hao wapelewa huko kwa makusudio yepi.

Wachambuzi na wafuatiliaji wa masuala ya Afrika na huko Congo DRC harakaharaka wamekanusha madai hayo ya Donald Trump na kusema madai hayo hayana ukweli wowote.

Serikali ya Congo DRC pia imekanusha kuwepo kwa zoezi hilo ambalo kama lipo ni la kustaajabisha.

Je, ni kweli wapo wafungwa hawa wanopelekwa huko Marekani na kwa malengo yepi?

Au ndo kupewa mafunzo ya kijeshi kwa ajili ya kutumika kuleee...
 
Mgombea mtarajiwa wa kiti cha uraisi wa Marekani na pia mshtakiwa aletiwa hatiani kwa makosa ya kughushi nyaraka Donald Trump leo ameongea na waandishi wa habari na wafuasi wake katika ofisi zake mjini New York.

Akiongea kwa muda wa dakika zipatazo 40 kuashiria kila kosa alotiwa hatiani kwa makosa yote 34, bwana Trump ametumia muda mwingi kuwashambulia jaji aliesimamia kesi yake na wazee wote wa baraza ambao wamemkuta ana hatia ya kughushi nyaraka za hesabuzake za kulipa kodi.

Bwana Trump atarajiwa kutangazwa kuwa mgmbea uraisi wa chama cha Republican siku mbili baada ya hukumu kutolewa mwezi Julai.

Lakini leo mchana akiongea na wafuasi wae na waandishi wa habari katika jumba lake maarufu kama Trump Tower, bwana Trump ametoa madai ya kuamsha akili pale alipodai kwamba kuna wafungwa kutoka Congo DRC Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ambao wamekuwa wakipelekwa Marekani bila kufafanua kwamba wafungwa hao wapelewa huko kwa makusudio yepi.

Wachambuzi na wafuatiliaji wa masuala ya Afrika na huko Congo DRC harakaharaka wamekanusha madai hayo ya Donald Trump na kusema madai hayo hayana ukweli wowote.

Serikali ya Congo DRC pia imekanusha kuwepo kwa zoezi hilo ambalo kama lipo ni la kustaajabisha.

Je, ni kweli wapo wafungwa hawa wanopelekwa huko Marekani na kwa malengo yepi?

Au ndo kupewa mafunzo ya kijeshi kwa ajili ya kutumika kuleee...
Mwongo huyo; ujumbe aliotaka kufikisha kwa watu wake ni kuwa watu weusi wanaokwenda USA kutoka Africxa ni criminals waliotolewa kwenye magereza ya DRC. Ni kwamba hataki watu wesi kutoka Africa waende USA.
 
Mwongo huyo; ujumbe aliotaka kufikisha kwa watu wake ni kuwa watu weusi wanaokwenda USA kutoka Africxa ni criminals waliotolewa kwenye magereza ya DRC. Ni kwamba hataki watu wesi kutoka Africa waende USA.
Yule ni mbaguzi mshenzi kabisa
 
Trump atakuwa rais wa US soon tu
Hapana hawezi kuwa rais hata kidogo ingawa atatoa ushindani mkubwa sana kwa vile marekanni imegawanyika sana kiitikadi! Hata hivyo ata-destabilize sana utendaji kazi wa serikali iwapo Senate au House itachukuliwa na republican kwani ni mtu ambaye hataki kunyamaza na watu wa republican wanamwogopa sana. Serikali ijayo inaweza kumaliza miaka yote minne bila kutekeleza lolote la maana kutokana na mvuto baina ya congress na White House.

Wanasiasa wengine wakishashindwa uchaguzi hunyamaza na kustaafu siasa labisa, lakini yeye hakubali kushindwa na anataka jina lake liwe mbele kila siku.
 
Hapana hawezi kuwa rais hata kidogo ingawa atatoa ushindani mkubwa sana kwa vile marekanni imegawanyika sana kiitikadi! Hata hivyo ata-destabilize sana utendaji kazi wa serikali iwapo Senate au House itachukuliwa na republican kwani ni mtu ambaye hataki kunyamaza na watu wa republican wanamwogopa sana. Serikali ijayo inaweza kumaliza miaka yote minne bila kutekeleza lolote la maana kutokana na mvuto baina ya congress na White House.

Wanasiasa wengine wakishashindwa uchaguzi hunyamaza na kustaafu siasa labisa, lakini yeye hakubali kushindwa na anataka jina lake liwe mbele kila siku.
kama obama!
wenzake walipostaafu walipumzikanila yeye kila siku alikua anapiga makelele
 
Back
Top Bottom