Trump amechomoa betri ghafla, serikali za Afrika zenye viongozi walioshindwa kutumia rasilimali za nchi zao hawajui nini wafanye

Trump amechomoa betri ghafla, serikali za Afrika zenye viongozi walioshindwa kutumia rasilimali za nchi zao hawajui nini wafanye

Ila hiyo executive order ya Trump imepelekwa Mahakamani,sidhani kama itafanya kazi.
Itafanya kazi na namiombea Mungu ifanye kazi

Najua iliyopelekwa ni kuhusu uraia wa kuzaliwa ,watt wanaozaliwa kule kuwa raia..
 
Trump anawajua viongozi wa Afrika kuliko hata sisi waafrika tunavyowajua viongozi wetu. Haya maamuzi anayoyachukua Trump ni kwa manufaa ya waafrika.
Kaona trip nyingi za viongozi wakubwa kwenye nchi za mbali, wakitumia madege makubwa huku yamebeba watu kibao.
 
Mtu anajinyima rasilimali zake anakupa wewe, badala ya kutumia kwa manufaa ya watu wako;
1. Unanunua magoli kwa 5m?
2. Unanunua Sa100 2025 pikipiki nchi nzima?
3. Unanunua zaidi ya mabasi 200 ya ccm?
4. Unapeleka wajumbe zaidi ya 1,000 Dodoma na kuwapa more than 2m? Ili tu wakupitishe bila kuzingatia demokrasia?

Mwenzako anawakamua matajiri na watu wake kodi kubwa ili akupe wewe.
 
Mimi binafsi kwenye jambo lolote la kitaifa siweki udini au uchama.

Kiongozi akifanya vizuri nitampa pongezi zake lakini siwezi kugeuka kuwa mtumwa wa mtu. Never

Sitakuwa mtumwa wa mwanasiasa yeyote mpaka nitakufa.

Tulipiga kelele humu inakuwaje mtu unamsifia Rais huku mpaka vyoo vya shule vinajengwa kwa pesa za msaada ?

Bajeti yetu tunayosomewa na akina Mwigulu ni bajeti hewa, maana unapanga bajeti huku pesa huna. Ikitokea jambo la kutikisa Dunia bajeti inafail kwa 80%.

Tuna rasilimali nyingi hata kuzitaja naona uvivu lakini serikali ya CCM ambayo Watanzania wachache wamejitoa akili kuisifia kila asubuhi, mchana, jioni na usiku imeshindwa kuzitumia badala yake nchi inaishi kwa misaada.

Hii miezi 3 ya mapitio ya misaada ya Marekani ni pigo kubwa sana kwa wananchi mafukara maana ndio waathirika wakubwa.

Huenda hali ya maisha ya Watanzania ikabadilika zaidi na kuwa duni maana Trump ni kama amechomoa betri bila taarifa.
Trump asifiwe kwa ubunifu uliotukuka, tunapewa misaada kisha mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam anasema tunatibiwa kwa dawa za mama! Wajinga wanampigia makofi! Humu wamejaa tele akina Lucas Mwashambwa.
 
Trump asifiwe kwa ubunifu uliotukuka, tunapewa misaada kisha mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam anasema tunatibiwa kwa dawa za mama! Wajinga wanampigia makofi! Humu wamejaa tele akina Lucas Mwashambwa.
Akina Luca na rafiki zao kama ni wasomi wa nchi hii yafaa wakamatwe warudishwe kusoma chekechea kwa lazima.
 
Back
Top Bottom