Trump kulipwa bilioni 37 na kituo Cha TV Cha ABC kwa kumchafulia jina

Trump kulipwa bilioni 37 na kituo Cha TV Cha ABC kwa kumchafulia jina

econonist

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
20,189
Reaction score
29,663
Kituo Cha televisheni Cha ABC kimeamua kukubali kumlipa Rais Donald Trump kiasi Cha Bilioni 37 za kitanzania kama fidia ya kumchafulia jina Rais huyo mteule wa Marekani. Rais mteule Donald Trump aliamua kufungua kesi dhidi ya ABC baada ya mtangazaji wa ABC Bwana George Stephaphoulous kutangaza ya kwamba Trump ni mbakaji na kwamba alipatikana na hatia ya kumbaka mwanamke.

Ukweli ni kwamba mahakama haikusema hivyo kwamba Trump alikuwa na hatia ya kubaka bali alipatikana na hatia ya shambulio la aibu dhidi ya mwanamke huyo na sio ubakaji. Trump alienda mahakamani kudai fidia ya kuchafuliwa jina kwa kuitwa mbakaji. Baada ya kuona Trump kafungua kesi, ndipo ABC walipoamua kuomba msamaha na kukubali kesi iishe nje ya mahakama na kukubali kumlipa Trump kiasi Cha Dollar milioni 16 ambazo ni sawa na shilingi bilioni 38 za kitanzania.

Source: CNN
 
Shirika la Habari la ABC News limekubali kumlipa Rais mteule wa Marekani, Donald Trump takriban dola milioni 15, sawa na TSh. bilioni 35.5 ili kusuluhisha kesi ya kumchafulia jina, baada ya kutangaza kwamba alipatikana na kosa la ubakaji.
photo-output.jpeg

Mwanahabari George Stephanopoulos alitoa kauli hizo mara kwa mara wakati wa mahojiano mwezi Machi mwaka huu alipokuwa akimpinga mbunge mmoja kuhusu kumuunga mkono Trump.

Baraza la majaji katika kesi hiyo mwaka jana, liliamua kuwa Trump aliwajibika kwa kosa la unyanyasaji wa kijinsia ambayo ina ufafanuzi maalum chini ya sheria ya New York.

===
IMG_1590.jpeg
 
Yeye anadaiwa huko New York hataki kulipa, naye akayajenge na aliowakosea awalipe ili kuwe na usawa.
 
Muosha huoshwa naye ana hatia lukuki ingependeza naye akafuata utaratibu huu, wa kuyamaliza nje ya mahakama alipe wote alio wakosea.
 
Huyu mwamba kama ni mishale katupiwa ya kupitiliza but jamaa linachomoa! Ana bahati, amemtanguliza Mungu wa Yakobo mbele.
Ni kweli, kama sio Mungu wa Yakobo, wangemfyetua siku nyingi sana.
 
Back
Top Bottom