Trump: Nchi za BRICS zenye mpango wa kuikwepa Dola ya Marekani zitakumbana na ushuru wa asilimia 100, Wanaweza kwenda kutafuta “mjinga” mwingine

Trump: Nchi za BRICS zenye mpango wa kuikwepa Dola ya Marekani zitakumbana na ushuru wa asilimia 100, Wanaweza kwenda kutafuta “mjinga” mwingine

View attachment 3166300

BRICS = Brazi, Russia, India, China, South Africa

Kaandika kwenye ukurasa wake wa Twitter

Wazo kwamba nchi za BRICS zinajaribu kuachana na Dola ya Marekani huku tumekaa na kuwatazama LIMEKWISHA! Tunahitaji ahadi kutoka kwa nchi hizi kwamba hawataunda Sarafu mpya ya BRICS, wala kuunga mkono sarafu nyingine yoyote kuchukua nafasi Dola ya Marekani yenye nguvu duniani, vinginevyo zitakumbana na ushuru wa asilimia 100 kwenye bidhaa wanazoingiza na zijiandae kuaga kuuza kwenye uchumi ulionona wa Marekani. Wanaweza kwenda kutafuta “mjinga” mwingine! BRICS haiwezi kuchukua nafasi ya Dola ya Marekani katika Biashara ya Kimataifa, na nchi yoyote itakayojaribu inapaswa kuaga Marekani !

The idea that the BRICS Countries are trying to move away from the Dollar while we stand by and watch is OVER. We require a commitment from these Countries that they will neither create a new BRICS Currency, nor back any other Currency to replace the mighty U.S. Dollar or, they will face 100% Tariffs, and should expect to say goodbye to selling into the wonderful U.S. Economy. They can go find another “sucker!” There is no chance that the BRICS will replace the U.S. Dollar in International Trade, and any Country that tries should wave goodbye to America.​
Vita ya biashara inakuja...
 
Ukipandisha ushuru watakao umia ni watumiaji wa mwisho wa nchini kwako.

Kafuatilie trade war ya marekani na China 2018 Trump hajaanza kuwa mwendawazimu leo.

Uzuri ana deal na mataifa yenye akili yanayo nufahika na upumbavu wake.
Umesema vyema

Tariffs ni hidden tax itakayolipwa na Wamarekani na sio Wachina. Hiyo tariffs ni pigo kwa Wamarekani

Pili, itawaongezea production cost manufacturers wa Marekani wanaotegemea kuimport bidhaa China ili wafanye uzalishaji mwisho wa siku tena atakayebeba huo mzigo ni final consumer aliyeko Marekani

Trump atalazalisha inflation tu
 
Hujui màana ya kupandisha ushur mkuu, maana yake bidhaa za ndani zitapewa kipaumbele na kuangalia soko nafuu zaidi. Kumbuka bidhaa anazozalisha china kupeleka Marekani siyo kwamba Marekani hazipo ndiyo maana umeambiwa na Mr Trump 'wonderful economy ' Sasa unahisi wamarekani Wana njaa? Kwa ufupi ni kwamba iwapo US itapandisha Kodi kwa bidhaa za china itabidi makampuni ya wamarekani yenye viwanda china kwa sababu ya cheap labours yatabidi yawe reallocated US ili kujiendesha kwa faida. Na hii itapelekea china kuanguka kiuchumi kwa raia wake kukosa ajira na serikali kukosa mapato ya mauzo. Trump akili kubwa yule Mzee.
Trumpet anaweza akawa akili kubwa ila wewe ukawa akili ndogo sana unadhani brics imeanza kuanzishwa Jana na leo na marekani hawakujua kama inatishia uwepo wao kwanini wasinge hamishia hayo makampuni yao tokea awali trumpet unadhani hakuwahi kua rahisi wa marekani kabla kwanini hajafanya haya uloyasema kabla kijana unaelewa maana ya uchumi hata kwa asilimia moja kama kila mtu angekua anatumia kile anacho kizalisha kwakua tu anaweza basi uchumi usingekua na maana ngoja nikutoe tongo tongo kidogo hata uwe unatengeneza mpaka miti ila lazima uuze ama ununue ndani na nje ndio utapata maana na dhana halisi ya uchumi na kama kwa kutegemea tu soko la ndani basi uchina ana nafasi ya juu kuipiku marekani sababu kuu mbili nakupa ambazo marekani hana na hautakua nazo moja population ya china kubwa mbili skilled workers someni vijana nyie ndio mnatufanya waafrika wote tunaonekana vilaza
 
Umesema vyema

Tariffs ni hidden tax itakayolipwa na Wamarekani na sio Wachina. Hiyo tariffs ni pigo kwa Wamarekani

Pili, itawaongezea cost of production manufacturers wa Marekani wanaotegemea kuimport bidhaa China ili wafanye uzalishaji mwisho wa siku tena atakayebeba huo mzigo ni final consumer aliyeko Marekani

Trump atalazalisha inflation tu
Exactly na matokeo yake products za China zitakua expensive kuliko za ndani au nchi zingine, so wanunuzi watanunua za wapi?? Common sense tu wala sio majazba, imani au uchawi - typical business
 
Huyo Marekani yeye anauza wapi? Ukitoa ulaya ambayo kwanza uchumi wao usha fikia kikomo cha kukua, Marekani anategemea kuuza China ,India na Brazili.

Pia kumbukeni Bricks wana natural resources za kutosha hasa China Russia,Irani, Brazili.
Tatizo moja unafiki.. china hachelew kwenda kuongea na sim chooni na USA
 
Trumpet anaweza akawa akili kubwa ila wewe ukawa akili ndogo sana unadhani brics imeanza kuanzishwa Jana na leo na marekani hawakujua kama inatishia uwepo wao kwanini wasinge hamishia hayo makampuni yao tokea awali trumpet unadhani hakuwahi kua rahisi wa marekani kabla kwanini hajafanya haya uloyasema kabla kijana unaelewa maana ya uchumi hata kwa asilimia moja kama kila mtu angekua anatumia kile anacho kizalisha kwakua tu anaweza basi uchumi usingekua na maana ngoja nikutoe tongo tongo kidogo hata uwe unatengeneza mpaka miti ila lazima uuze ama ununue ndani na nje ndio utapata maana na dhana halisi ya uchumi na kama kwa kutegemea tu soko la ndani basi uchina ana nafasi ya juu kuipiku marekani sababu kuu mbili nakupa ambazo marekani hana na hautakua nazo moja population ya china kubwa mbili skilled workers someni vijana nyie ndio mnatufanya waafrika wote tunaonekana vilaza
Tangu 2018 Trump ameanza kupambana na China kwenye trade war, sanctions, tariffs, decoupling na derisking

Hakuna hata kimoja alichofanikiwa nashangaa wanaozisifu hizo ngonjera zake.

Wachina walishampuuza kitambo
 

Attachments

  • Screenshot_20241005_010637_WhatsAppBusiness.jpg
    Screenshot_20241005_010637_WhatsAppBusiness.jpg
    324.7 KB · Views: 2
Mchina ndumilakuwili atawachomolea fyuzi wenzake.....
China ni gaidi wa uchumi,yeye kazi yake ni kukusanya tuu hakuna jingine.Hawajui hata kuchangia maafa wao ni kukusanya na kuuza tuu,kwanini Hawa watu Wana roho mbaya hivi,ilikuwaje wakakua hivi na huku Japan ikipotea kiasi hiki,India nao ni walewale wanajua kukamua tuu
 
Ukiweka mahaba na chuki pembeni na ukautazama uchumi wa dunia ulivyo na namna biashara za dunia zinavyoendeshwa ni wazi kuwa mataifa itawachukuwa miaka mingi ya damu, tabu, na mateso kuachana moja kwa moja na Dola ya Marekani......

Kwa namna Marekani ameisuka nchi yake, uchumi wake na mifumo yake ya kibiashara na siasa zake ni wazi kuwa kila nchi inatamani kuuza au kushirikiana kiuchumi na Mmarekani...

Wafanyabiashara, matajiri na wawekezaji karibia wote kutoka pande zote dunia wanajiona wapo salama wakiwekeza Marekani kuliko nchi nyingine yoyote..........

Kwa kifupi anguko la Dola lipo lakini mizizi ya dola imeenda mbali na itachukuwa miaka mingi sana kuitoa.......

Je mataifa yapo tayari kuziingiza kwenye dhiki nchi na wananchi wake kwenye kupambana na anguko la Dola......je dunia ipo tayari kuzikabili athali za anguko la dollar ya Marekani na imejiandaaje kwa muda huo hadi kupata nyingine itakayokuwa stable kama Dola....???

Lisemwalo lipo....
 
Umesema vyema

Tariffs ni hidden tax itakayolipwa na Wamarekani na sio Wachina. Hiyo tariffs ni pigo kwa Wamarekani

Pili, itawaongezea cost of production manufacturers wa Marekani wanaotegemea kuimport bidhaa China ili wafanye uzalishaji mwisho wa siku tena atakayebeba huo mzigo ni final consumer aliyeko Marekani

Trump atalazalisha inflation tu
Wakulima wakimarekani walilalamika sana upuuzi wa DT 2018 China walipojibu mapigo

Uzuri huyu kichaa Trump yeye huwa anaanza alafu wenzake wanajua namna ya kumaliza
 
Ukiweka mahaba na chuki pembeni na ukautazama uchumi wa dunia ulivyo na namna biashara za dunia zinavyoendeshwa ni wazi kuwa mataifa itawachukuwa miaka mingi ya damu, tabu, na mateso kuachana moja kwa moja na Dola ya Marekani......

Kwa namna Marekani ameisuka nchi yake, uchumi wake na mifumo yake ya kibiashara na siasa zake ni wazi kuwa kila nchi inatamani kuuza au kushirikiana kiuchumi na Mmarekani...

Wafanyabiashara, matajiri na wawekezaji karibia wote kutoka pande zote dunia wanajiona wapo salama wakiwekeza Marekani kuliko nchi nyingine yoyote..........

Kwa kifupi anguko la Dola lipo lakini mizizi ya dola imeenda mbali na itachukuwa miaka mingi sana kuitoa.......

Je mataifa yapo tayari kuziingiza kwenye dhiki nchi na wananchi wake kwenye kupambana na anguko la Dola......je dunia ipo tayari kuzikabili athali za anguko la dollar ya Marekani na imejiandaaje kwa muda huo hadi kupata nyingine itakayokuwa stable kama Dola....???

Lisemwalo lipo....
Rubbish,
Umeanza kwa kujihami eti ukiweka mahaba pembeni, halafu ukayatumia hayo hayo mahaba!

Wewe mmarekani mweusi wa Nzega unafikiri unaweza kusema jambo baya dhidi ya Marekani?
Wagalatia mmekariri sana.
 
Wala usijali bwana utamu, dollar haitaanguka kwa uchawi na maombi, take or leave it
Uzuri anguko la dollars wala haihitajii uwe na elimu kuubwa kuliona kama linazidi kuendelea marekani kama empire inaanza kumeguka taratibu kwasasa inaanza ushawishi lengo kuu hapa dollars imeporomoke na ndio inaendelea hakuna anae omba dua watu wanakaa chini wanafanya majambo kaa hapo hapo
 
Tanzania itapona kweli katika vita hii baridi ya wakubwa ?

Kwa kiswahili:

BUNGE LA DUMA

Vyacheslav Volodin alihudhuria mkutano wa Vladimir Putin na Rais wa Muungano wa Mabunge Tulia Ackson​

Mkutano ulifanyika kando ya Kongamano la 10 la Wabunge wa BRICS huko St
Julai 11, 2024, 17:54
Rais wa Shirikisho la Urusi Vladimir Putin, Spika wa Baraza la Shirikisho Valentina Matvienko, Mwenyekiti wa Jimbo Duma Vyacheslav Volodin na Rais wa Muungano wa Mabunge, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson (picha kwa hisani ya vyombo vya habari huduma ya Rais wa Shirikisho la Urusi)

Rais wa Shirikisho la Urusi Vladimir Putin, Spika wa Baraza la Shirikisho Valentina Matvienko, Mwenyekiti wa Bunge la Duma Vyacheslav Volodin na Rais wa Muungano wa Mabunge, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson (picha kwa hisani ya vyombo vya habari huduma ya Rais wa Shirikisho la Urusi)


Rais wa Shirikisho la Urusi Vladimir Putin amekutana na Rais wa Muungano wa Mabunge, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson. Mwenyekiti wa Bunge la Duma Vyacheslav Volodin na Spika wa Baraza la Shirikisho Valentina Matvienko walihudhuria mkutano huo.

Vladimir Putin alikumbuka kwamba IPU "ni shirika linaloheshimika ambalo lilianzishwa nyuma mwishoni mwa karne ya 19. Nchi nyingi ni wanachama wake.

Tunakaribisha ukweli kwamba sasa inaongozwa na mwakilishi wa uchumi unaoendelea barani Afrika.

“Kwa upande wetu, tunatumai kwamba mtaunga mkono kazi ya mwelekeo wa wabunge wa BRICS, ambayo ni muhimu. Sio tu kwamba inaweka msingi wa kazi ya pamoja ili kuimarisha mfumo wa udhibiti kati ya mataifa yanayoshiriki, lakini pia inajenga mazingira mazuri ya kibinadamu kwa ajili ya kufikia malengo ya pamoja ya maendeleo. Kwa mara nyingine tena, ningependa kuwashukuru kwa ushiriki wenu katika mkutano wa wabunge wa nchi za BRICS,” alisema Vladimir Putin.

Mkutano wa Vladimir Putin na Tulia Ackson ulifanyika kando ya Mkutano wa 10 wa Wabunge wa BRICS unaoendelea mjini St.
1kutoka 4
Rais wa Shirikisho la Urusi Vladimir Putin na Mwenyekiti wa Jimbo la Duma Vyacheslav Volodin (mikopo ya picha: huduma ya vyombo vya habari ya Rais wa Shirikisho la Urusi)

Rais wa Muungano wa Mabunge, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson (picha ya hisani: huduma ya vyombo vya habari ya Rais wa Shirikisho la Urusi)

Rais wa Shirikisho la Urusi Vladimir Putin, Spika wa Baraza la Shirikisho Valentina Matvienko, Mwenyekiti wa Jimbo Duma Vyacheslav Volodin na Rais wa Muungano wa Mabunge, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson (picha kwa hisani ya vyombo vya habari huduma ya Rais wa Shirikisho la Urusi)

Rais wa Muungano wa Mabunge, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson (picha ya hisani: huduma ya vyombo vya habari ya Rais wa Shirikisho la Urusi)

Rais wa Shirikisho la Urusi Vladimir Putin na Mwenyekiti wa Jimbo la Duma Vyacheslav Volodin (mikopo ya picha: huduma ya vyombo vya habari ya Rais wa Shirikisho la Urusi)

Rais wa Muungano wa Mabunge, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson (picha ya hisani: huduma ya vyombo vya habari ya Rais wa Shirikisho la Urusi)

Rais wa Shirikisho la Urusi Vladimir Putin, Spika wa Baraza la Shirikisho Valentina Matvienko, Mwenyekiti wa Jimbo Duma Vyacheslav Volodin na Rais wa Muungano wa Mabunge, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson (picha kwa hisani ya vyombo vya habari huduma ya Rais wa Shirikisho la Urusi)

Rais wa Muungano wa Mabunge, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson (picha ya hisani: huduma ya vyombo vya habari ya Rais wa Shirikisho la Urusi)

Rais wa Shirikisho la Urusi Vladimir Putin na Mwenyekiti wa Jimbo la Duma Vyacheslav Volodin (mikopo ya picha: huduma ya vyombo vya habari ya Rais wa Shirikisho la Urusi)

Rais wa Muungano wa Mabunge, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson (picha ya hisani: huduma ya vyombo vya habari ya Rais wa Shirikisho la Urusi)

Rais wa Shirikisho la Urusi Vladimir Putin, Spika wa Baraza la Shirikisho Valentina Matvienko, Mwenyekiti wa Bunge la Duma Vyacheslav Volodin na Rais wa Muungano wa Mabunge, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Tulia Ackson (picha kwa hisani ya vyombo vya habari huduma ya Rais wa Shirikisho la Urusi)
Hapo ambaye hajui mlango wa ziada wa kutokea ni huyo babu anaye tizamana na PUTIN lkn wengine hasa PUTIN mwenyewe akiingia chakani unakuta alishajua kabisa mlango mwingine wa kutokea endapo alioingilia ukizibwa.
 
Back
Top Bottom