Trump usiisaidie fedha Africa, isaidie chaguzi zao na kukamata viongozi wao wezi.

Tunapishana mitazamo kwakuwa wewe unaongelea wajasiliamali; machinga na wauza nguo kutoka Gwanzu, China. Biashara kama hizo haziwezi kuendesha nchi. Nchi inaendeshwa na biashara za kimataifa kule ambako tunapata pesa za kigeni, USD na Euro na Yen. Masoko haya ndio silaha kuu ya wakoloni wakati wanaondoka tukidhani tumepata uhuru. Masoko haya haya hayako huru kwa nchi za Afrika zoooooote, hasa chini ya Jangwa la Sahara. Ndio maana nchi zote hizi zinafanana kiuchumi bila kujali ni chama kipi kinatawala nchi. Masoko haya ndiko inakopatikana mitaji ya uwekezaji na fedha za kununulia na kuendeleza technolojia ya kisasa kabisa.

Masoko haya yamejaa tariffs, ushindani wa ubora, ubaguzi, dhuluma na vikwazo visivyo vya haki.
 
Hata huo mtizamo ninao, (we consume what we do not produce catalyzed by neocolonialism)

Sisi wenyewe kwa wenyewe tuna kandamizana kwa mfumo wa. Ostracism, ukiwa na fikra chanya ambazo zitawanyang'anya washikatonge unashughulikiwa
 
Hata huo mtizamo ninao, (we consume what we do not produce catalyzed by neocolonialism)
Sisi wenyewe tuna kamdamizana kwa mfumo wa. Ostracism
entrepreneurship tunayowapa vijana wetu inawawezesha kupata ugali na mbonga 7 tu. Hata mchezaji akiwa mzuri kuliko Ronaldo hawezi kwenda kucheza Ulaya hivihivi bila ukiritimba mgumu kufuatwa lakini wao wanaweza kuja kwetu wakati wowote na vyovyote kuja kucheza. Hivyohivyo, hata kwa pamba, korosho, dhahabu, nyama, mayai kutoka Afrika ya weusi.
 
Uko sahihi kila mtu ni mjuaji akiweza kutembea ama kusema kama wewe labda hata kuendesha gari basi hapo humwambii kitu anakuwa anajua kila kitu tena wengine hutaka ufikiri wanavyotaka wawao hata kama hawajui back ground knowledge yako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…