Mkuu hizi dawa haziuzwi kwenye maduka ya dawa, zinatolewa bure na Serikali na zinatolewa kwa wagonjwa kwa prescription(kwa maelezo ya Daktari).
Suala la uhaba lipo na litaendelea kuwepo(nadhani unaijua serikali yetu na vipaumbele vyake awamu hii).
Dawa mbadala haitolewi ovyo ovyo kwa kujisikia tu bali ni kulingana na hali ya mgonjwa aliyo nayo kama maudhi(side effects) au kuimarika kwa hali (yaani kutoka Unstable kuwa Stable ).
Huo mbadala Daktari anaufanya.
-Kwa maelezo zaidi ya tatizo lako tembelea kituo cha Afya unapopatia hiyo huduma siku zote.