Try Again achia ngazi

Try Again achia ngazi

Ukishabikia sana Simba na Yanga lazima akili za kichwani zinaanza kupungua.

KUNA VIJANA WENGI MNO AKILI ZIMERUKA KABISA, HAWANA FUTURE WAO NI KUWAZA SIMBA NA YANGA TU.....

MSIPOTEZE MUDA NA UPUUZI WA SIMBA NA YANGA.

MY MESSAGE
MWENYE MASIKIO NA ASIKIE.
 
PALE Yanga hakuna MASHETANI wala MAJINI. Pale Kuna akili kubwa inayojua sayansi ya mpira. Katika mpira wa miguu akili ikikutana na pesa huwa tafarani.

Ndicho unachokiona REAL MADRID na MAN -CITY. Ndio unachokiona BAYERN MUNICH na maeneo mengine.

Kule Urusi kulikuwa na team inaitwa ANZHI MACHAKHCHKALA. Ilikuwa na pesa kweli kweli. Iliwahi kumnunua Samuel Etoo na kumfanya kuwa mchezaji anayelipwa zaidi duniani.

Ila bahati mbaya ilikuwa ni moja. Pesa za Suleiman Kerimov mmiliki wa team hazikukutana na maarifa makubwa ya mpira. Matokeo yake team ikayumba na kupotea.

Kuna siku msemaji wa Yanga alikamwe alisema namna ya bora ya kuidhibiti Yanga sio kuchukua wachezaji au watendaji wake bali ni kumsajili Injinia Watu wakadhani anafanya MAHOKA. Ila angalia!

Katika kikosi cha kwanza cha msimu uliopita, hayupo Fiston Mayele, hayupo Djuma Shaban, hayupo Yanick Bangala wala hayupo Zanzibar finest, Feisal Toto.

Ila kama hiyo haitoshi kocha mkuu alienda, Kocha msaidizi alienda, mtaalamu wa viungo alienda, Kocha wa magoli kipa alienda, pamoja na performance analyst wa team pia naye alienda. Ila unaiona Yanga? Hiyo ndio tafsiri sahihi ya ujenzi imara wa taasisi.

Unakumbuka baada ya Senzo kuamua kuondoka Yanga? Kila mmoja alidhani shughuli ya wananchi katika mipango na maarifa ilikuwa imefika mwisho!

Ila injinia akawatuliza. Akasema kama wao ndio waliomleta Senzo basi pia wanajua ni wapi pa kumpata mbadala wake. Baada ya muda tukamuona smart man Andre Mtine akiingia.

Unakumbuka story za kuondoka kwa Nasredeen Nabi? Unakumbuka ule mshangao na fadhaa waliokuwa nao wananchi? Unakumbuka hisia za wachambuzi na wadadisi kuwa huenda zama za Yanga na soka la kuvutia zilikuwa zimefika mwisho!!?

Ila sasa kuna Jorga Bonito kwa hisani ya Miguel Angel Gamondi. Fundi wa ki - Argentina aliyemfanya Rulani Mokwane na kikosi chake kukosa amani kwa dakika zote 180 za mechi zao.

Baada ya pongezi kwa wachezaji na benchi la ufundi, rudisha heshima kwa GSM na uongozi wa Yanga. Pale ndipo ilipo mipango. Pale ndipo Kuna mikakati inayofanya wanaokuja kuziba mapengo na kuua athari ya wanaoondoka!
MO STUKA SASA
TRY AGAIN NA, MANGUNGU HAWAJUI MPIRA WAAJIRI TD AU CEO ANAEJUA MPIRA YANGA WATAKUWA MABINGWA WA WA AFRIKA KABLA YAKO MAANA WANATEMBEA KATIKA NDOTO ZAKO
Hukumuona Mayele kwenye Kambi ya Simba Cairo?

Unataka nini tena?
 
Mangungu na kaka yake try again tunawakubali sana sisi Makolo.
 
Umeandika kwa uchungu sana baada ya Mwakarobo junior kutolewa CAFCL .

Pole sana 🐸🐸watazoea tu baada ya kupata uzoefu kama walionao Simba, 🐸🐸waendelee tu kujitafuta Ila waache makelele kwenye CAFCL huko sio NBCPL.
Simba ana uzoefu upi kwenye ligi ya mabingwa?
 
Ukishabikia sana Simba na Yanga lazima akili za kichwani zinaanza kupungua.

KUNA VIJANA WENGI MNO AKILI ZIMERUKA KABISA, HAWANA FUTURE WAO NI KUWAZA SIMBA NA YANGA TU.....

MSIPOTEZE MUDA NA UPUUZI WA SIMBA NA YANGA.

MY MESSAGE
MWENYE MASIKIO NA ASIKIE.
Sahihi
 
Wadau na wapenzi wa simba sport club naomba tuungane, katika kampeni hii ya kumshinikiza mo na kampuni yao ya METL kuondoka Simba, ili kupisha wawekezaji wengine.

Ni ukweli usiopingika kwamba uwekezaji wa mo na kampuni yao ya metl katika club yetu pendwa simba sport club hauna tija, hauna faida kwa simba na pia haueleweki
Tunahitaji kuwa wawekezaji wengi, ili

1. Kuwa na mtaji mkubwa,
2. Kuleta uwazi na uwajibikaji katika uendeshaji wa timu kwa sababu viongozi hawatakuwa vibaraka mwekezaji

Tunataka wawekezaji watakao weka hela mezani na sio kwenda kununua bond bot halafu ile fida ndio uilete kuendeshea timu, huu ni uwekezaji ambao hauna tija.

Muwekezaji akitumia brand ya simba kwenye bidhaa zake anatakiwa kulipia, na ashindanishwe na makampuni mengine, kama akikosa basi.

Nawasilisha
 
Back
Top Bottom