Tsh Milion tatu (3,000,000) tasilimu

Tsh Milion tatu (3,000,000) tasilimu

Mkuu 0909Hekima,

Uchakachuaji wa asali ni changamoto inayokua kwa kasi sana nchini mwetu, hili linachangiwa sana na wafanyabiashara na wafuga nyuki wasio waaminifu. Uhitaji wa asali bado ni mkubwa na unaendelea kukua kwa kasi ndani na nje ya Tanzania, cha kuzingatia ni kuwa na asali bora inayokidhi viwango vinavyohitajika. Mfano hai wa hili ni kiwanda cha kusindika asali kilichopo Visiga Kibaha kushindwa kufikia lengo lake la ununuzi asali toka wafuga nyuki mwaka jana kutokana na ubora duni wa asali.

Elimu ya ufugaji bora wa nyuki na uvunaji mzuri wa asali na mazao mengine ya nyuki utasaidia kupunguza tatizo la ubora duni. Kwa Morogoro, maeneo mengi wanauza mizinga, mfano SUA (Idara ya Misitu), Kihonda Viwandani n.k. Pia kuna watengenezaji wengi mitaani wa mizinga. Cha kuzingatia ni aina na ubora wa mizinga ya kutumia.

Karibu kwenye ufugaji nyuki! Kwa maelezo yoyote na msaada kuhusu ufugaji nyuki tafadhali tuwasiliane.

Safi sana mkuu, haya ndiyo mambo tunatakiwa tuyapate hapa JForums.

Kwa suala la asali kama nikiivuna tayari na nikaamua kuisafirisha kuja Dar es Salaam, ninaweza kukaa nayo siku ngapi bila kuharibika??

Au mpaka niichemshe??
 
mkuu asigwa bei ya mizinga inafikia kiasi gani kwa sasa!kama hapa moro ninashamba mikese.thanks
 
Nasahukuru wa kuu kwa michango yenu kwa sasa niliamua kuanza na asali lakin kabla sijaanza kufuga nyuki nimeamua kuanza kununua ili nijue market nina mzigo tayari pia mnakaribishwa kuniunga mkono.nataraji baada ya miez mitatu ninunue shamba nifuge mbuzi kadhaa kwani niko ktk mchakato wa kupata ardhi na nimeongea na manispa na wanaanza kugawa soon
 
Fanya hivi:

  1. Nunua ardhi ekari moja - Tshs 500,000/- max. Ardhi hii iwe inafaa kwa ajili ya kufuga nyuki. Kwa Morogoro jaribu maeneo ya Mikese, vijii nyuma ya Sangasanga (mf: Mafuru), Mkundi kwa mbele n.k.
  2. Nunua mizinga 10 ya kisasa ya nyuki (commercial beehives) - Tshs 1,200,000/-.
  3. Installation cost ya mizinga + usafiri - Tshs 350,000/-

Baada ya miezi sita - ceteris paribus:
  1. Kila mzinga utatoa lita 30 - 40.
  2. Utauza asali kwa Tshs 10,000/-
  3. Jumla ya mapato kwa mvuno mmoja itakua Tshs 3,000,000 - 4,000,000/-
  4. Utavuna mara mbili kwa mwaka i.e pato hapo juu *2

Kila la kheri!

Mkuu haya mawazo yako yamenikuna sana, Naomba kuuliza maswali ya msingi mawili matatu....

Hekari moja inaweza kuchukua mizinga mingapi kitaalamu na kibongo bongo inakaa mingapi??

Kama nitapata eneo la hekari say 50 nikaanzisha bustani yangu mwenyewe ya maua, je production inaweza kupanda kwa kuwa malighafi ya kutengeneza asali inakua karibu na nyuki hawawezi kwenda mbali??

Kwa uelewa wako binafsi vipi soko la asali kwa mtu anayezalisha mzigo mkubwa kwa mwaka??

Thanks in advance
 
mkuu asigwa bei ya mizinga inafikia kiasi gani kwa sasa!kama hapa moro ninashamba mikese.thanks

Mkuu kama unataka kuendesha kibiashara zaidi bei ya mzinga wa kutosha kutoa lita 40 kwa mara moja ie lita 80 kwa mwaka ni tsh 120,000 kama utataka kununua ile ya kitaalamu ila kbongo bongo inakwenda mpaka 60 au 70 hivi.
 
Mkuu bdo hebu weka humu elimu ya ufugaji wa mbuzi, inaonekana umekomaa katika sehemu hii. Unajua mbuzi kama kilimo ni njia muafaka ya kuachana na huu "umasikini" tunaoelezewa. Funguka mkuu bdo
 
Back
Top Bottom