TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

TTCL Customer Care

Official Account
Joined
Aug 18, 2016
Posts
279
Reaction score
317
Ndugu mteja,

Una tatizo lolote unapotumia mtandao wetu? Una ushauri wowote ili tuiboreshe huduma yetu?

Tafadhali itumie mada (thread) hii ili tukusaidie kwa urahisi.

Unapokuwa na tatizo, ili tukusaidie kirahisi zingatia haya:

- Ni tatizo gani? (T-PESA, SMS, Calls, Internet, usajili, kukatika kwa mawasiliano n.k)

- Maeneo gani? (Tukifahamu maana ulipo, inakuwa rahisi kukuelekeza wapi uende ili upate msaada toka kwa wakala wetu aliye karibu nawe)

- Tatizo limeanza lini na limejirudia au kuendelea kuwa kero kwako kwa muda gani?

- Kama ni ushauri, zingatia ya juu lakini tutafurahi tukijua kwanini unapendekeza unachopendekeza.

- Kama ni pongezi, zingatia ya juu na tungependa pia upendekeze lipi tufanye kuzidi kuiboresha huduma kwako.


Zifuatazo ni ofisi zetu za huduma kwa wateja ndani ya jiji la Dar es Salaam.


1. POSTA
[emoji654][emoji654][emoji654]Mtaa wa Samora, jengo la Extelecom ghorofa la Chini.


2. KARIAKOO
[emoji654][emoji654][emoji654]Mtaa wa Makamba/Msimbazi, jengo la Akamba Bus Service.

3. UPANGA
[emoji654][emoji654][emoji654]Mtaa wa Magole/Maliki, karibu na Diamond Jubilee.


4. MAGOMENI
[emoji654][emoji654][emoji654]Mtaa wa Minaki/Fundiki, karibu na Manispaa ya Kinondoni.


5. KIJITONYAMA
[emoji654][emoji654][emoji654]Kijitonyama Sayansi, barabara ya Ali Hassan Mwinyi/ Rose Garden.


6. OYSTERBAY
[emoji654][emoji654][emoji654]Barabara ya Haile Selassie.


7. UBUNGO
[emoji654][emoji654][emoji654]Jengo la Ubungo Plaza/ Ghorofa la chini.


8. MBEZI BEACH
[emoji654][emoji654][emoji654]Mbezi Makonde/ Jengo la Shamo Tower.


9. TABATA
[emoji654][emoji654][emoji654]Tabata Bima, barabara ya Segerea karibu na kanisa la Romani Katoliki.


10. CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM.
[emoji654][emoji654][emoji654]Jirani na tawi la benki ya NBC, jirani na kilipo kituo cha polisi cha UDSM.


11. BARABARA YA PUGU
[emoji654][emoji654][emoji654]Barabara ya Mwalimu Nyerere, karibu na Sigara.


12. WAGENI
[emoji654][emoji654][emoji654]Uwanja wa ndege.


13. PUGU
[emoji654][emoji654][emoji654]Jengo la Quality Centre, ghorofa la chini.


14. KISUTU
[emoji654][emoji654][emoji654]Mtaa wa Mchafukoge/Libya jengo la Haad Plaza.


15. TEGETA SHOP
[emoji654][emoji654][emoji654]Jengo la Kibo Complex, ghorofa la chini.


16. MWANANYAMALA SHOP
[emoji654][emoji654][emoji654]Mwananyamala A, barabara ya Mwinjuma yalipo makutano ya Mwananyamala A.


17. KURASINI
[emoji654][emoji654][emoji654]Kurasini Exchange Area, jirani na Chuo cha Diplomasia.


Wasiliana nasi:
[emoji337]022 210 0100
[emoji390] 0738 151 511
[emoji273]www.ttcl.co.tz


#RudiNyumbaniKumenoga
View attachment 1529645


Karibu.

Rudi Nyumbani Kumenoga
 
Hivi vocha za TTCL wanatengeneza na madini gani?

Mbona kuzipata imekuwa taabu sana, yaani vocha kupatikana mtaani ni habari ya kushangaza.

Nyie TTCL kama kampuni mama ya mawasiliano nchini mnataka kufanya biashara au huduma? Nauliza kwa sababu hamuonekani katika biashara na katika huduma pia hampo.

Huduma zenu TTCL zinapatikana katikati ya miji kwa kiwango kizuri kidogo vipi huku mashambani au mtandao wenu ni kwa ajili ya watu wa mjini sisi wa mashambani tuendelee kutumia Buzz.

Kwanini TTCL msijitokeze nje ya ofisi mjitangaze watu wawajue nini mnafanya, naona kama mmejifungia ndani na promotion zikifanyika mitandaoni tu.

Ni mara chache sana mashirika ya umma kutoa huduma zenye kukidhi vigezo vya watumiaji kutokana na kubweteka ila najua mngekuwa na mikakati mizuri basi kila mtaa ungekuwa unaimba TTCL katika mtazamo chanya ila kelele za sasa ni malalamiko ya huduma, hii inadhihirisha kuwa bado hamna mikakati kabambe ya kuteka sekta ya mawasiliano nchini huwenda tuwape miaka mingi.
 
Sina uhakika kama TTCL watajibu.. Ila yangu ni haya:

1. Meneja Masoko wenu TTCL ameshindwa kazi.. Hampo popular. Yaani kuna siku niluamua hadi kupiga simu kuulizia menu ya T-pesa.

2. Kuna kipindi nilienda Jijini Mbeya kikazi.. Kule ukinunua kifurushi cha internet ya TTCL basi ujue umeamua kutoa sadaka.. Hutatumia hata Mb 1. Ile ni extremely slow.

3. Hamna utaratibu wa kuwachombeza wateja.. Wenzenu wana vi sms au call kukbushia jambo
 
TTCL, Nyumbani kumejoga na tumerudi..

Swali langu ni kwanini mmebadirisha bei za vifurushi bila kutupa taarifa sisi wateja wenu.

Pili kwanini ttcl inapatikana katikati ya miji tu..ukitoka kidogo nnje ya mji hupati huduma kama inavyotakiwa hasa upande wa data..

Hongereni kwani upande wa voice mpo vizuri mno
 
Mimi huwa si mteja wa TTCL, ila kuna location fulani fulani huwa nikienda natumia mtandao wao.

Leo kuna kifurushi cha internet cha bandika bandua saa 24 (@TSH. 1000/=) kiliandikwa GB 4.. Sasa nashangaa nimejiunga nikawasha data, nikadownload "Dream League Soccer 2020" (MB 316) nkapat ujumbe et nimebakiwa na MB 50. Je, hii maana yake nini?
 
Obvious suala nitakalozungumzwa Pasi na shaka limezungumzwa na members hapo juu, Ila nitumie tu fursa hii kukazia maarifa, kiukweli TTCL ndio mtandao wangu kwa Mishe ya Internet na ninaenjoy vifurushi vyenu. Ila tatizo kubwa mpo tu katikati ya miji.

Napata shida sana nipokwenda nyumbani kusalimie huko Lindi vijijini.. Yaan ukianza kuiacha tu municipal ya Lindi basi mtandao unasepa mazima.

Nipo pale Nyangao - Lindi barabara kuu ya kuelekea Masasi District Ila mtandao hausomi kabisa.

Kwa nini wasiwe kama halotel ambao wanapatikana hadi remote area..?

Kuhusu suala la vocha za TTCL huwa siwazii, actually vocha zao ni adimu sana hata mijini Ila kwa kuwa kuna huduma ya T-Pesa hii ndo inanirahisishia sana, So naomba mlifanyie kazi hili.

Ni Mimi mteja wa TTCL kutoka NYANGAO-LINDI
 
Back
Top Bottom