TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

TTCL Corporation: Support thread (Maswali, ushauri na malalamiko)

Badala ya kutumia muda mwingi kwa kujivunia.., tumieni huyo muda kubuni, kuboresha na kuendeleza.... Mkifanya hivyo wala hautahitaji kuwaambia / kuwakumbusha watu wenyewe watakuwa wanaambiana tu.... Kama wenye busara walivyosema Kizuri Chajiuza.....
 
Mimi binafsi sihaongeza Salio mwezi Sasa baada ya kupandisha 1500 gb1 hiyo Ni wizi, vifurushi vya chuo mmeobeza Bei, Bando tamtam mmefuta. Basi Bali na Ttcl yenu
 
Asante kwa ushauri wako.
Nitaufikisha kwa menejementi.

#RudiNyumbaniKumenoga
SIO NITAUFIKISHA KUA PROFFESIONAL..NI TUTAUFIKISHA....NA WEWE NDO KAMPUNI TUNAHITAJI MAJIBU YALIYOJITOSHELEZA....MNAISHI KWA MAZOEA..MAWAKALA WAMEJAA NJE YA JENGO LENU ILA HAMFUATI RAIA WALIPO...KWENYE MFUMO WA SIMU ZA MKONONI MMEFERI KWA KWELI
 
Rekebisheni kifurushi cha bandika bandua, angalau iwe GB 1 saa mchana na GB 3 usiku mwa manane. Mkifanya hivyo mimi naachana na halotel. MB 500 mchana ni ndogo,
 
Hongera sana TTCL kazi yenu iko wazi kila mpenda maendeleo anaona wazi.
Rekebisheni bei za vifurushi angalau muendane na airtel hayo ni mawazo yangu
ubora uendane na nguvu ya mnunuaji itapendeza zaidi.
 
1. Mageuzi tunayoyaona hivi sasa kwenye matumizi ya mifumo ya kidigitali na kielektronik nchini yanatokana na uwepo wa miundombinu bora ya mawasiliano kutoka TTCL Corporation. Tunajivunia mafanikio haya.

2. TTCL Corporation imetoa mchango mkubwa katika kuchangia ukuaji wa sekta mbalimbali za maendeleo nchini. Hivi sasa tumefanikiwa kutoa huduma za mawasiliano kwa Vyuo Vikuu vya Elimu ya juu, Ofisi za Mabalozi, Taasisi za dini, Makampuni, Wateja wa Nje ya Tanzania, Mabenki, Taasisi za fedha, Taasisi za Serikali nk.

3. Ni lazima tujivunie mafanikio haya, tumeimarisha huduma zetu za simu za mkononi kwa kutumia teknolojia ya 2G, 3G na 4G nchi nzima ili kuhakikisha ubora wa huduma ya Intaneti na Sauti zinapatikana muda wote. Na tunaendelea kuboresha zaidi ili kukidhi mahitaji ya wateja wetu. Mageuzi yanaendelea

4. Hii ni hatua kubwa zaidi katika kuongeza mvuto kwa wateja wetu, tumefanya mageuzi makubwa katika kuongeza mvuto wa Maduka yetu ya Huduma kwa Wateja ili kutoa wigo kwa wateja wetu kufurahia huduma zetu kwenye mandhari mazuri. Tembelea maduka yetu upate huduma bora na nzuri kutoka kwa wahudumu wenye weledi na bashasha wakati wote.

5. Tunawashukuru sana wateja wote mliojiunga na mtandao wetu wa TTCL Corporation, tunajivunia sana kuwa nanyi. Tunawahakikishia tutaendelea kutoa huduma bora na zenye kiwango ili kuongeza chachu katika ukuaji wa maendeleo ya Taifa letu.

Asanteni kwa kutuunga Mkono.
6. Tumeongeza mawakala wa kuuza Vocha za Muda wa maongezi kupitia mawakala wakubwa na wadogo. Pia tumeimarisha upatikanaji wa Vocha kupitia njia za kielektroniki ili kukidhi mahitaji ya wateja wetu, hivi sasa unaweza nunua muda wa maongezi kupitia T-PESA, Mawakala wa Selcom, Mawakala wa Mobistock, Mawakala CRDB na NMB, kupitia mitandao mingine ya Simu, Wakala wa TPB, Cellulant nk

7. TTCL Corporation tuna haki ya kujivunia, tumeimarisha biashara, tumeboresha njia za mawasiliano na tumeongeza uwajibikaji ndani ya Shirika ambapo juhudi zimeleta mafanikio makubwa kwa kutoa GAWIO kiasi cha Shilingi Bilion 3.6/- (TZS) kwa serikali kwa mwaka wa fedha 2017/2018 na 2018/2019.

8. TTCL Corporation tumeshirikina kikamilifu katika kuhakikisha tunapeleka mawasiliano katika maeneo yote ambayo miradi ya ujenzi wa viwanda unaendelea nchini, tumepeleka mifumo ya mawasiliano yenye ubora ili kutoa fursa kwa wawekezaji katika sekta ya Viwanda kuwa na mazingira Rafiki ya mawasiliano. Kwa kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara tumepeleka mawasiliano ya Data na Sauti kupitia miundombinu ya TTCL Corporation kwenye Ukanda maalumu wa uwekezaji {Export Processing Zone (EPZ) na Special Economic Zone(SEZ) nchini ili kuchochea maendeleo ya sekta hiyo.

9. Tumegusa kila Miradi mikubwa kwa kuwapa Mawasiliano bora ya Data na Sauti, tunatambua umuhimu wa miradi hii katika ukuaji wa maendeleo ya Taifa letu. Tumeshiriki kikamilifu katika kupeleka mawasiliano ya Data na Sauti katika Bwawa la Kufua Umeme wa Maji la Mwalimu Julius Nyerere.

10. Tumehakikisha Sekta ya Afya inakuwa na miundombinu bora ya mawasiliano, tumeshirikiana na Wizara ya Afya na Taasisi zake katika kuimarisha TIBA MTANDAO ambapo Hospitali kubwa na ndogo nchini zimeungwa kwenye miundombinu ya mawasiliano ya TTCL Corporation ambayo imefanikisha utoaji wa TIBA kupitia mtandao.
Waongo wakubwa nyie

Vocha tu haipatikani,t.pesa ni ujinga ujinga tu unatoa pesa haitoki au unatuma haiendi kila siku network mbovu,mbaya zaidi hakuna mawakala wa kutosha wa T.pesa!!


Maajabu mengine kwamba mmefanya biashara mkapiga faida kiasi mkajikuta mnatoa gawio la 3.6 billion kwa biashara ipi mnayopiga faida kiasi hicho?


Boresheni huduma naimani mna mtaji kwa sababu mnajiendesha kwa kodi za watanzania!
 
1. Mageuzi tunayoyaona hivi sasa kwenye matumizi ya mifumo ya kidigitali na kielektronik nchini yanatokana na uwepo wa miundombinu bora ya mawasiliano kutoka TTCL Corporation. Tunajivunia mafanikio haya.

2. TTCL Corporation imetoa mchango mkubwa katika kuchangia ukuaji wa sekta mbalimbali za maendeleo nchini. Hivi sasa tumefanikiwa kutoa huduma za mawasiliano kwa Vyuo Vikuu vya Elimu ya juu, Ofisi za Mabalozi, Taasisi za dini, Makampuni, Wateja wa Nje ya Tanzania, Mabenki, Taasisi za fedha, Taasisi za Serikali nk.

3. Ni lazima tujivunie mafanikio haya, tumeimarisha huduma zetu za simu za mkononi kwa kutumia teknolojia ya 2G, 3G na 4G nchi nzima ili kuhakikisha ubora wa huduma ya Intaneti na Sauti zinapatikana muda wote. Na tunaendelea kuboresha zaidi ili kukidhi mahitaji ya wateja wetu. Mageuzi yanaendelea

4. Hii ni hatua kubwa zaidi katika kuongeza mvuto kwa wateja wetu, tumefanya mageuzi makubwa katika kuongeza mvuto wa Maduka yetu ya Huduma kwa Wateja ili kutoa wigo kwa wateja wetu kufurahia huduma zetu kwenye mandhari mazuri. Tembelea maduka yetu upate huduma bora na nzuri kutoka kwa wahudumu wenye weledi na bashasha wakati wote.

5. Tunawashukuru sana wateja wote mliojiunga na mtandao wetu wa TTCL Corporation, tunajivunia sana kuwa nanyi. Tunawahakikishia tutaendelea kutoa huduma bora na zenye kiwango ili kuongeza chachu katika ukuaji wa maendeleo ya Taifa letu.

Asanteni kwa kutuunga Mkono.
6. Tumeongeza mawakala wa kuuza Vocha za Muda wa maongezi kupitia mawakala wakubwa na wadogo. Pia tumeimarisha upatikanaji wa Vocha kupitia njia za kielektroniki ili kukidhi mahitaji ya wateja wetu, hivi sasa unaweza nunua muda wa maongezi kupitia T-PESA, Mawakala wa Selcom, Mawakala wa Mobistock, Mawakala CRDB na NMB, kupitia mitandao mingine ya Simu, Wakala wa TPB, Cellulant nk

7. TTCL Corporation tuna haki ya kujivunia, tumeimarisha biashara, tumeboresha njia za mawasiliano na tumeongeza uwajibikaji ndani ya Shirika ambapo juhudi zimeleta mafanikio makubwa kwa kutoa GAWIO kiasi cha Shilingi Bilion 3.6/- (TZS) kwa serikali kwa mwaka wa fedha 2017/2018 na 2018/2019.

8. TTCL Corporation tumeshirikina kikamilifu katika kuhakikisha tunapeleka mawasiliano katika maeneo yote ambayo miradi ya ujenzi wa viwanda unaendelea nchini, tumepeleka mifumo ya mawasiliano yenye ubora ili kutoa fursa kwa wawekezaji katika sekta ya Viwanda kuwa na mazingira Rafiki ya mawasiliano. Kwa kushirikiana na Wizara ya Viwanda na Biashara tumepeleka mawasiliano ya Data na Sauti kupitia miundombinu ya TTCL Corporation kwenye Ukanda maalumu wa uwekezaji {Export Processing Zone (EPZ) na Special Economic Zone(SEZ) nchini ili kuchochea maendeleo ya sekta hiyo.

9. Tumegusa kila Miradi mikubwa kwa kuwapa Mawasiliano bora ya Data na Sauti, tunatambua umuhimu wa miradi hii katika ukuaji wa maendeleo ya Taifa letu. Tumeshiriki kikamilifu katika kupeleka mawasiliano ya Data na Sauti katika Bwawa la Kufua Umeme wa Maji la Mwalimu Julius Nyerere.

10. Tumehakikisha Sekta ya Afya inakuwa na miundombinu bora ya mawasiliano, tumeshirikiana na Wizara ya Afya na Taasisi zake katika kuimarisha TIBA MTANDAO ambapo Hospitali kubwa na ndogo nchini zimeungwa kwenye miundombinu ya mawasiliano ya TTCL Corporation ambayo imefanikisha utoaji wa TIBA kupitia mtandao.
Niliwahi kumsikiliza Prof Lumumba,akisema "ukifanya kitu,harafu ukatumia muda mrefu kueleza ulichofanya,badala ya kuacha ulichofanya kijitsngaze,Basi ujue hujafanya kitu"
TTCL,imehujumiwa sana,watendaji wakuu wote ilibidi wawe jela.
Kwanza tuanze,TTCL ina data center ngapi?Tigo wanazo tatu ambazo ni Tier three,kiwango Cha kimataifa.
Nenda kwenye tower za TTCL uone Miundombinu ilivyo chakaa,TTCL Wana switch ngapi?nenda mbezi juu,uone switch ya Voda,ilivyo ya kiwango Cha juu.
Ili shirika,wanaoliongoza Wana vikampuni vidogo,kiasi kwamba Kuna mgongano wa kimaslahi mkubwa.
Sasa hv,hata ukitembea dar,uwezi kusikia inaitwa njoo usajiri au ununue laini ya TTCL,utasikia Voda,Tigo,halotel,
Kazi kubwa inahitajika.
Sio hizi mbwembwe.
Kama vp,tafuteni management kutoka MTN sothafrica.
 
Niliwahi kumsikiliza Prof Lumumba,akisema "ukifanya kitu,harafu ukatumia muda mrefu kueleza ulichofanya,badala ya kuacha ulichofanya kijitsngaze,Basi ujue hujafanya kitu"
TTCL,imehujumiwa sana,watendaji wakuu wote ilibidi wawe jela.
Kwanza tuanze,TTCL ina data center ngapi?Tigo wanazo tatu ambazo ni Tier three,kiwango Cha kimataifa.
Nenda kwenye tower za TTCL uone Miundombinu ilivyo chakaa,TTCL Wana switch ngapi?nenda mbezi juu,uone switch ya Voda,ilivyo ya kiwango Cha juu.
Ili shirika,wanaoliongoza Wana vikampuni vidogo,kiasi kwamba Kuna mgongano wa kimaslahi mkubwa.
Sasa hv,hata ukitembea dar,uwezi kusikia inaitwa njoo usajiri au ununue laini ya TTCL,utasikia Voda,Tigo,halotel,
Kazi kubwa inahitajika.
Sio hizi mbwembwe.
Kama vp,tafuteni management kutoka MTN sothafrica.
Sawa mkuu, tumekusikia.
 
Kwa kifupi kabisa,kajifunzeni Voda,Tigo,Halotel na Airtel wanachofanya,nyie bado mpo nyuma sana kiasi tunaogopa hata kujiunga na nyinyi,vocha zenu hazipatikani,mawakala wenu hakuna,yani unazunguka mjini kuitafuta TTCL huipati,nadhani bado mpo nyuma sana.
 
Kwa kifupi kabisa,kajifunzeni Voda,Tigo,Halotel na Airtel wanachofanya,nyie bado mpo nyuma sana kiasi tunaogopa hata kujiunga na nyinyi,vocha zenu hazipatikani,mawakala wenu hakuna,yani unazunguka mjini kuitafuta TTCL huipati,nadhani bado mpo nyuma sana.

Kujifunza toka kwa washindani wao Voda,Tigo,Halotel na Airtel ni moja. Mbili ni kuboresha zaidi na kuweka utofauti kati ya TTCL na hao wengine. Hii inawezekana sana na wakiweza hilo watakua juu mawinguni
 
Ndugu ttcl.
Ulishawahi kusikia sukari ya Kilombero inapigiwa debe kwamba Ni tamu?
Huu muda mnaotumia kusema blah blah, mngekua mnaotumia ku upgrade mitambo, huduma na watanyakazi. Kuna tofauti kubwa sana Kati ya mfanyakazi wa Vodacom na wa TTCL. Utafikiri wa TTCL anajitolea
 
Ndiyo bado ninayo
Nbona simpo tu mkuu.
Ingia SETTING kisha sehemu ya SECURITY.
Baada ya hapo,angalia walipoandika SET UP SIM CARD angalia ipo laini ya TTCL kama ipo ON weka OFF kisha ingiza PIN zilizopo kwenye kikadi cha laini.
 
[emoji51][emoji51][emoji51][emoji51]
Mnafeli sana
1. Madukani hakuna vocha

2. Hamjitangazi au mnatumia mbinu za kizamani, hebu ona wenzenu tigo, voda airtel huwezi katiza mtaa bila kukutana na wakala aliyevaa tishet la mtandao wao.

3. Vifurushi vyenu havina amsha amsha kama hao wengine

4. Hakuna mawakala wa kutoa pesa mitaaani mmelala lala tu kwasbb mnajua kuna mshahara mwisho wa mwezi.


Ningekuwa na uwezo ningekuwa nawatumbua hadi kupatikane mtu sahihi
,
 
Back
Top Bottom