Tuache tabia ya kuchunguliana kwa sangoma haina maana ni uongo tu

Tuache tabia ya kuchunguliana kwa sangoma haina maana ni uongo tu

Mung Chris

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2017
Posts
3,391
Reaction score
3,849
Mazungumzo kati ya sangoma na Syntia yalikuwa hivi

Synthia: Hodi hapa

Sangoma: ingia

Synthia: ahsante shkamoo docta

Sangoma: marhahabaaaaaa, karibu ukae

Synthia: ahsante

Sangoma: sema shida yako

Synthia: docta kuna mkaka flani hivi ananitongoza ila sijamkubalia, nikaona nije nikuone ili unisaidie kumuangalia kama ana mke, kama ndio mume wangu kabisa, je anapesa na atakuwa ananisaidia nikiwa na shida.

Sangoma: enhe anaitwa nani nipe majina yake yote, unayo picha yake

Synthia: ndio majina haya hapa nimeandika na picha yake hii hapa

Sangoma: Grrrrrr, grrrrrr, grrrrrrr nimemuona huyu hapa grrrrrrrrrr, sasa huyu mwanaume sio mume wako anataka tu ukae naye na mfanye yenu basi

Synthia: docta hela anazo eheh

Sangoma: Huyu ninavyo muona hana shida kabisa ila chunga sana muweke karibu sana na wewe

Synthia: sasa docta huyu mkaka si umfanyie kitu ili pesa zote awe ananipa mimi, kila ninachosema awe anakubali wala asifurukute

Sangoma: hamnashida atakuwa anakupa kila kitu, sasa hela ya vifaa umeleta sh ngapi lakini

Synthia: jamani doctor hela sio tatizo

Sangoma: grrrrrrrrr, grrrrrrrrrr, grrrrrrrrrr utapata kila unacho kitaka nimesha mchukua huyu mchumba wako kila kitu atakupa

Synthia: ahsante ndo navyotaka nataka nimlie hela zake hadi nimjengee mama yangu nyumba kijijini na hata jua.

Sangoma: haya nenda kaoge hii *awa, muwekee kwenye maji ya kuoga na hii hapa uweke chini ya mto hakikisha haioni.

ITAENDELEA MAY 6, 2018.
 
We ulisikiaje hayo mazungumzo kama.na wewe hukuepo kwa Sangoma?
 
Huu uzi wanawake hawawezi kukubali kuwa wameuelewa kwakua wana interest nao.
 
Back
Top Bottom