Tuambie uongo uliowahi kuambiwa kuhusu magari

Dunamist

JF-Expert Member
Joined
Aug 13, 2018
Posts
474
Reaction score
686
Imagine nikiwa mdogo nliambiwa ETI Range rover haziruhusiwi kupaki benki, kwa sababu eti zina speed kali kwa hiyo zikitumiwa na majambazi kupora, polisi hawawezi kuzifukuzia wakazipata.

Halafu pia eti, Range rover huwa hazipinduki, eti kwa sababu tairi zake huwa zinatanuka gari ikitaka kupindiuka au ikiwa inakata kona kali ikiwa speed.

Mlionilisha haya matango pori hamuendi mbinguni.
 
Gari hizo hizo tuliambiwa kama kuna maji zinapita tu hatà kama ni mengi maana zenyewe zinaelea tu kwenye maji.
 
Me niliambiwa gar ni anasa....kuja kujua ni essential aisee.
 
Hakuna aliedanganywa kama mimi.. mi niliambiwa kuna gari zikikugonga haufi kwasababu zimetolewa kadude ka kuuwa!..🤣🤣
Sahivi nipo kuzimu kama unanduguyo yupo huku mtaje nimpe salamu zako..😜
 
Niliambiwa ukiwa na gari ww ni tajiri, kumbe ni tajiri wa stress tu
 
mkuu sio RANGE ROVER

ni PEOGOUT 504 almaarufu enzi hizo *FAIVOFOO* enzi ya MWALIMU mpk kuja mwinyi hizo ndinga zilikuwa haziruhusiwi kupaki mbele ya bank ikiwatayari kwa mtindo wa kutaka kuondoka
kutokana na waharifu majambazi majambakaya kikenya na kiburundi kuzitumiakufanya uporaji
ikikimbizana na gofu inaachiwa vumbi tu
 
Vile vile range rover eti ukiikimbiza hadi sped ya mwisho kwenye dush board eti kuna kioo ambayo kuna picha ya mtu anapita akiwa kajitwika jeneza
 
Ukiwa na gari we ni tajiri, ila saivi nawaona wenye wanaacha magari nyumbani tunabanana kwenye daladala. sijajua ni wese au service?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…