Tuanze Kujipanga Kwa Uchakataji wa Mazao ya Kilimo na Ufugaji

Druggist

JF-Expert Member
Joined
Nov 10, 2010
Posts
439
Reaction score
528
Waheshimiwa itifaki imezingatiwa.Baada ya Kushughulika na Kilimo kwa miaka kadhaa,iliyoambatana na hasara Hapa na pale,hebu tuanze kutafakari Mazao yetu jinsi ya kuyaongezea thamani kwa kuzingatia haya:-
1)Ni mazao yapi yanazalishwa kwa wingi,kwa gharama nafuu (Kuna economies of scale katika production) ya kufocus nayo?
2)Mazao hayo yakiongezewa thamani yanaweza kuwa exported au soko lake lipo la Kutosha ?
3) Gharama za uzalishaji zinaweza kutufanya kuwa competitive soko ni? i.e.tuna competitive advantage?--Nishati,skilled labour force,packaging materials nk
4)Tuna sera na sheria Ambazo ni rafiki kwa Viwanda vya Kusindika mazao ya Kilimo (agrobased factories)
Karibuni!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…