Gaston Mbilinyi
JF-Expert Member
- Jan 24, 2010
- 296
- 51
Matokeo ya kidato cha nne 2012 yametoka hivi karibuni na yameleta gumzo miongoni mwa jamii ya ndani na nje ya Tanzania kutokana na namna wanafunzi walivyofeli. Achilia mbali kufeli, wanafunzi wengine badala ya kujibu maswali wakachora picha za watu, wengine wakatukana matusi na wengine kuandika beti za bongo fleva! Viongozi wetu wameweweseka na hata kupata kigugumizi maana inaonekana wana mchango mkubwa kwa watoto kufeli kiasi hicho! Hakika hii ni aibu ya taifa wala si ya watoto waliofeli tu.
Nimekuwa nikifuatilia sababu zinazotajwa kuwa zimechangia wanafunzi hao kufeli na wengi wanasema sababu zifuatazo kuwa ndio source ya sisi kama taifa kuaibika kiasi hiki.
1. Ukosefu wa walimu.
2. Ukosefu wa vitabu vya kiada na ziada ( kufundishia na kujifunzia)
3. Ukosefu wa maktaba
4. Ukosefu wa Maabara
5. Kukosekana kwa haki za walimu wanazopaswa kulipwa kisheria
6. Kukosekana kwa mitaala kumesababisha ufundishaji uwe shagalabaghala toka shule moja hadi nyingine
7. Kukosekana kwa motisha kwa walimu.
8. Upungufu wa vitabu na vifaa vya maabara.
9. Utandawazi ambao umechukua sehemu kubwa ya ubongo wa wanafunzi na hivyo kupuuza masomo.
10. Wazazi kutoshirikiana kwa ukaribu na walimu katika usimamizi wa wanafunzi.
11. Uwezo binafsi wa wanafunzi kuwa mdogo kwani wengine huchukuliwa wakiwa na alama za chini sana katika
kuingia kidato cha kwanza.
12. Uwezo mdogo kwa baadhi ya walimu.
13. Ualimu kuwa ni kimbilio la baadhi ya wakosa ajira ambao hawapo tayari kufundisha ila wapo tayari kwa mshahara.
14. Baadhi ya viongozi wa nchi kuona suala la elimu si muhimu ila siasa ndiyo muhimu kwao hivyo nguvu huelekezwa
katika siasa na hivyo elimu kutokuendeshwa kitaalamu bali kuongonzwa kisiasa.
15. NECTA wamejaa watu wa dini moja ambayo inakomoa watu wa dini nyingine
16. Masomo yanafundishwa kwa kiingereza badala ya Kiswahili
17. Watoto wanaanza form one wakiwa wadogo mno hivyo uelewa wao kuwa mdogo pia
18. Hali duni ya mazingira ya kufundishia mfano wanasema hakuna madawati na wengine chaki, umeme, n.k.
19. Watoto wa wakubwa/vigogo kutosoma katika shule hizi kunafanya vigogo kutojali kuboresha mazingira ya kufundishia
20. Shule nyingi za private ama ni za vigogo au vigogo wanahisa katika shule hizo hivyo hata huku kwa sisi walala hoi
kukiwapo kubovu hawajali, wao wanaangalia zaidi biashara yao ya hizo shule za private
Naamini na wengine yawezekana wamesikia sababu zingine wanaweza kuongezea hapo. Lakini najiuliza kujua sababu tu ya wanafunzi kufeli kunatosha? Kama ni kweli sababu ndio hizo, basi sasa tuchukue hatua nyingine ya kujadili namna tutakavyo weza kuondoka hapo kwaajili ya kuondoa tatizo.
Mimi nafikiri shule na vyuo vifungwe kwa japo mwaka mmoja na ndani ya mwaka huo yafuatayo yafanyike:
1. Sensa ya walimu ifanyike sambamba na shule tulizo nazo (ingawa shule zinajulikana)
2. Idadi ya walimu iliyopo igawiwe kwa shule zilizopo kwa kuzingatia nani anafundisha nini ili kuepuka walimu wanaofundisha
somo moja kulundikwa shule moja.
3. Walimu wafanyiwe semina au makongamano kwaajili ya kuwaweka sawa maana inaonekana wengine wanajisahau
4. Serikali iboreshe mazingira ya kufundishia kwa kuhakikisha inaweka vitabu na vifaa vingine pamoja na madawati
5. n.k.
Naomba michango yenu ya nini kifanyike ili kutatua tatizo la wanafunzi wetu aw sasa kufeli, kumbuka kila tatizo huwa na jibu.
Nimekuwa nikifuatilia sababu zinazotajwa kuwa zimechangia wanafunzi hao kufeli na wengi wanasema sababu zifuatazo kuwa ndio source ya sisi kama taifa kuaibika kiasi hiki.
1. Ukosefu wa walimu.
2. Ukosefu wa vitabu vya kiada na ziada ( kufundishia na kujifunzia)
3. Ukosefu wa maktaba
4. Ukosefu wa Maabara
5. Kukosekana kwa haki za walimu wanazopaswa kulipwa kisheria
6. Kukosekana kwa mitaala kumesababisha ufundishaji uwe shagalabaghala toka shule moja hadi nyingine
7. Kukosekana kwa motisha kwa walimu.
8. Upungufu wa vitabu na vifaa vya maabara.
9. Utandawazi ambao umechukua sehemu kubwa ya ubongo wa wanafunzi na hivyo kupuuza masomo.
10. Wazazi kutoshirikiana kwa ukaribu na walimu katika usimamizi wa wanafunzi.
11. Uwezo binafsi wa wanafunzi kuwa mdogo kwani wengine huchukuliwa wakiwa na alama za chini sana katika
kuingia kidato cha kwanza.
12. Uwezo mdogo kwa baadhi ya walimu.
13. Ualimu kuwa ni kimbilio la baadhi ya wakosa ajira ambao hawapo tayari kufundisha ila wapo tayari kwa mshahara.
14. Baadhi ya viongozi wa nchi kuona suala la elimu si muhimu ila siasa ndiyo muhimu kwao hivyo nguvu huelekezwa
katika siasa na hivyo elimu kutokuendeshwa kitaalamu bali kuongonzwa kisiasa.
15. NECTA wamejaa watu wa dini moja ambayo inakomoa watu wa dini nyingine
16. Masomo yanafundishwa kwa kiingereza badala ya Kiswahili
17. Watoto wanaanza form one wakiwa wadogo mno hivyo uelewa wao kuwa mdogo pia
18. Hali duni ya mazingira ya kufundishia mfano wanasema hakuna madawati na wengine chaki, umeme, n.k.
19. Watoto wa wakubwa/vigogo kutosoma katika shule hizi kunafanya vigogo kutojali kuboresha mazingira ya kufundishia
20. Shule nyingi za private ama ni za vigogo au vigogo wanahisa katika shule hizo hivyo hata huku kwa sisi walala hoi
kukiwapo kubovu hawajali, wao wanaangalia zaidi biashara yao ya hizo shule za private
Naamini na wengine yawezekana wamesikia sababu zingine wanaweza kuongezea hapo. Lakini najiuliza kujua sababu tu ya wanafunzi kufeli kunatosha? Kama ni kweli sababu ndio hizo, basi sasa tuchukue hatua nyingine ya kujadili namna tutakavyo weza kuondoka hapo kwaajili ya kuondoa tatizo.
Mimi nafikiri shule na vyuo vifungwe kwa japo mwaka mmoja na ndani ya mwaka huo yafuatayo yafanyike:
1. Sensa ya walimu ifanyike sambamba na shule tulizo nazo (ingawa shule zinajulikana)
2. Idadi ya walimu iliyopo igawiwe kwa shule zilizopo kwa kuzingatia nani anafundisha nini ili kuepuka walimu wanaofundisha
somo moja kulundikwa shule moja.
3. Walimu wafanyiwe semina au makongamano kwaajili ya kuwaweka sawa maana inaonekana wengine wanajisahau
4. Serikali iboreshe mazingira ya kufundishia kwa kuhakikisha inaweka vitabu na vifaa vingine pamoja na madawati
5. n.k.
Naomba michango yenu ya nini kifanyike ili kutatua tatizo la wanafunzi wetu aw sasa kufeli, kumbuka kila tatizo huwa na jibu.