TUCTA: Kima cha chini cha mshahara kiwe 970,000

TUCTA: Kima cha chini cha mshahara kiwe 970,000

Kaimu Katibu Mkuu wa TUCTA amesema wamefanya tafiti kubaini kiwango cha mshahara ambacho kinaweza kumtosha mtumishi kuendesha maisha yake.

Kutokana na Tafiti yao wamependekeza kiwango cha chini mshahara kiwe Tsh. 970,000 kutokana na gharama za maisha za sasa.

Hayo yamesemwa siku ya maadhimisho ya siku ya wafanyakazi ambayo kitaifa yamefanyika katika uwanja wa CCM Kirumba Mwanza.

View attachment 1770128

Pia soma: LIVE - Mei Mosi Mwanza: Rais Samia ahutubia, aahidi kuongeza mishahara kuanzia mwakani
Kabla hamjazungumza na serikali mjitambue kuwa ninyi vyama vya wafanyakazi ni vitanzi kwa watumishi. Serikali inapoongeza mishahara bila huruma mnamnyoa kila mfanyakazi 2%ya huo mshahara. Mmefanya hivi miaka mingi na wafanyakazi hawaoni msaada wenu kwao. Nyie ni sawa na viwavi jeshi kwenye shamba la maharage. Hamna chembe ya huruma. Fikiria kila mwezi unamfyeka kila mtumishi wastani wa shs 30,000/-mmeanzisha vitega uchumi lukuki lakini faida haijulikani ni ya nani. Wengine na mabenki wanayo lakini bado wanawafyeka wafanyakazi michango. Hamweleweki hata kidogo. Mngekuwa na akili angalao kidogo mngepunguza rate za makato kufikia 1% au mkaweka fixed amount ambayo kila mtumishi atachangia kwenye chama cha wafanyakazi. Wafanyakazi wote wana haki sawa lakini wengine wanalazimishwa kuchangia zaidi kupitia hiyo%.chakamwata walikuja na sera nzuri kea watumishi lakini mliwapiga vita kila mahali kama vile nyie mna haki miliki ya wafanyakazi(walimu)hili laihusu zaidi CWT. Ondoeni unyonyaji wenu kwa watumishi ndio muwe na uhalali wa kuzungumzia mshahara wa wafanyakazi.
 
Hao wabunge wako wangapi,na watumishi n wangapi
Unataka ujue idadi ili uhalalishe nini? Sikia wanasiasa wamefanikiwa kwa kiasi kikubwa kuua akili ya mbongo, wanasiasa wanalipana mishahara minono, lkn mtumishi kulipwa laki 9 hataki anaziona ni nyingi kupita kiasi. Mungu atuhurumie kwa kweli inasikitisha.
 
Mtumishi yupi?
Na wa level ipi ya elimu? Mfanya kazi wa Tanzania na dunia ya tatu kwa ujumla mshahara wake nyuma kuna mnyororo wa tegemezi zaidi ya 20. Na malengo yao ni ya muda mfupi sana, anataka siku 3 baada ya kuajiriwa awe na gari, ajenge nyumba na fenicha toka Dubai.
 
Kama wabunge wanavuta million 14 inashindikanaje kwa mtumishi.
Kumbe ni ulinganisho, sio utafiti? Uelewe 14m alipwazo mbunge si mshahara, ile ni hongo kwa shughuli ya kupitisha miswaada isiyo na kichwa wala miguu na mingine iletwayo usiku wa manane kwa hati ya dharula, na maumivu ya kupiga meza za bungeni.
 
Viongozi wa chama cha wafanyakazi unakuta walikimbia umande hawajui chochote kuhusu Uchumi hao wakikaa kikao kingine watakuja na kima cha chini milioni mbili wao kuzungumzia unyanyasaji makazini viongozi kuwapeleka jela na kuwatoa Kama watoto hilo hapana afya na mazingira mazuri migodini kimya makato kwa wafanyakazi haya ya mikopo kwa wanafunzi kimya kuomba wafanyakazi baadhi ya sekta wawe na aina ya mikopo isiyo kandamizi na kutengeneza mazingira bora kwa Wafanyakazi wao kimya kuzingatia muda kazi na mapumziko kwa Wafanyakazi wao hawasemi wanakaa kwenye mshahara tuu wakati yapo mangi ili mfanyakazi aishi maisha bora yasio na stress...
 
Watumishi wa umma wanajiona kama wapo wenyewe tu sijui hawajui ni 0.6% ya raia wote? Huu upuuzi wa kudai laki 9.7 ni Seriikali gani hii itakayolipa hyo pesa? Hv wanajua impact ya mshahara kupanda huku mitaani ?
Na hawajui hiyo mishahara ni kodi wanazokamuliwa wafanya biashara ambao wengine ni wachuuzi sokoni ambao pato halisi hata laki moja kwa mwezi hapati, na hufanya kazi zaidi ya saa 12 kwa siku , siku zote 365 za mwaka yupo kazini.
 
Kumbe ni ulinganisho, sio utafiti? Uelewe 14m alipwazo mbunge si mshahara, ile ni hongo kwa shughuli ya kupitisha miswaada isiyo na kichwa wala miguu na mingine iletwayo usiku wa manane kwa hati ya dharula, na maumivu ya kupiga meza za bungeni.
Kwa hiyo babu watumishi hamtaki kulipwa laki Tisa mnataka laki tatu tu, kwa kuwa kiongozi tz ni raha sana huongozi kwa presha.
 
Hata chini ya mia, kwani sh 50000 ikiwa malipo ya mwezi serikalini elewa sh itakuwa imepanda thamani.
Hebu weka fact za kiuchumi kutetea point yako, kama watumishi wa serikali hawafiki laki tano, lkn mtaani kuna mamilioni ya vibarua wanalipwa elf50 kwa mwezi, mbona nauli haijawa chini ya shingi mia, hivi hizi facts za kiuchumi hayo matangopori mnalishwa na nani?
 
wapendekeze na namna serikali inapo/inavyoweza kupata mapato ya kumudu hayo maongezeko!
 
Back
Top Bottom