BARD AI
JF-Expert Member
- Jul 24, 2018
- 3,591
- 8,826
Siku chache baada ya wanachama wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT), kutaka mjadala wa kikokotoo urudi upya, Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta) limesema utaratibu wote ulifuatwa na suala hilo lilishafikiwa mwisho.
Kauli hiyo imekuja baada mkutano ulioshirikisha CWT na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kuvunjika baada ya kuibuka kutokuelewana katika kiwango cha kikokotoo.
Baadhi ya wajumbe walimnyooshea kidole Kaimu Rais wa CWT, Dinah Mathamani, wakidai ameshindwa kuendesha kikao hicho.
Rais wa Tucta, Tumaini Nyamhokya alisema yanayotokea CWT hawezi kufahamu mitazamo yao ni ipi lakini suala la kikokotoo lilishapita na ni sheria.
“Sijui tunajadili nini kwenye sheria, tulishafuata taratibu zote hadi likafika hapo lilipofika. Masuala mengine ni masuala ya mtu mmoja katika chama siwezi kuwazuia wasiwaze lakini kama ni suala la utaratibu ulifuatwa na suala la kikotoo likafikia mwisho,” alisema.
Msimamo wa Tucta uliungwa mkono na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (Tughe), Rugemalira Rutatina akisema kupitia shirikisho hilo, wameshamalizana na Serikali kuhusu suala la kikokotoo, tatizo lililopo ni mifuko ya hifadhi ya jamii kutotoa elimu kwa wafanyakazi.
“Sisi tulishamalizana nao (Serikali) ila hawatoi elimu, watoke nje wakatoe elimu, watu waweze kuelewa, huo ndio mgogoro tulio nao. Lakini mambo ya kikokitoo sisi huko tulishatoka,” alisema.
Alipoulizwa nini mkakati wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi (PSSSF) kutoa elimu juu ya kikokotoo hicho baada kugonga mwamba CWT juzi, Meneja Uhusiano na Elimu kwa wanachama wa mfuko huo, James Mlowe aliahidi kulitolea ufafanuzi suala hilo leo.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (THTU), Dk Paul Loisulie, alisema hata kwao bado kuna vuguvugu halijapoa watu wametulia tu lakini iko siku wataibuka.
Alisema inahojiwa kwa nini wabunge wapewe mafao yote lakini wafanyakazi wapangiwe kiwango cha kupewa na kwanini mifuko ya hifadhi ibaki na fedha yao nyingi.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Dk Joseph Mhagama alisema kabla ya Mei Mosi mwaka huu, Serikali iliieleza kamati hiyo kuwa wamekubaliana na wadau waliridhika na kikokotoo hicho kipya ambacho ni asilimia 33.
“Maoni yangu ni kwamba ieleweke uamuzi ulifanyika collectively (kwa ushirikiano), kwa maana kulikuwa na mashauriano, haukuwa uamuzi wa upande mmoja, maana yake Serikali ilikaa na wadau na kufikia mwafaka wa asilimia 33,” alisema.
Dk Mhagama alisema ni vyema kama hawajaridhika (CWT), Serikali ione umuhimu wa kufanya mashauriano na wadau ili kupata uelewa wa pamoja kuhusu hatua hizo zilizochukuliwa.
Kwa upande wake Dinah alisema kabla ya kukutana mwezi ujao katika Mkutano mkuu wa CWT, watamweleza Waziri mwenye dhamana hisia za wanachama kuhusu kikokotoo. Hata hivyo, alisema baada ya kutangazwa kwa kikokotoo hicho kipya Mei mwaka huu, jambo hilo limefanyiwa kazi kwa muda mrefu na wameshirikishana.
“Kwa upande wetu ambao kikokotoo kilikuwa asilimia 50 na kushushwa kuwa asilimia 33, nadhani tutapata mshtuko lakini hali ndivyo ilivyo kwa kuwa tumeelezwa kwanini tumefikia hapa na faida zake bila kujali waliokuwa asilimia 50 au asilimia 25 lakini kubwa ni mifuko kuwa endelevu,” alisema.
MWANANCHI
Kauli hiyo imekuja baada mkutano ulioshirikisha CWT na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF) kuvunjika baada ya kuibuka kutokuelewana katika kiwango cha kikokotoo.
Baadhi ya wajumbe walimnyooshea kidole Kaimu Rais wa CWT, Dinah Mathamani, wakidai ameshindwa kuendesha kikao hicho.
Rais wa Tucta, Tumaini Nyamhokya alisema yanayotokea CWT hawezi kufahamu mitazamo yao ni ipi lakini suala la kikokotoo lilishapita na ni sheria.
“Sijui tunajadili nini kwenye sheria, tulishafuata taratibu zote hadi likafika hapo lilipofika. Masuala mengine ni masuala ya mtu mmoja katika chama siwezi kuwazuia wasiwaze lakini kama ni suala la utaratibu ulifuatwa na suala la kikotoo likafikia mwisho,” alisema.
Msimamo wa Tucta uliungwa mkono na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (Tughe), Rugemalira Rutatina akisema kupitia shirikisho hilo, wameshamalizana na Serikali kuhusu suala la kikokotoo, tatizo lililopo ni mifuko ya hifadhi ya jamii kutotoa elimu kwa wafanyakazi.
“Sisi tulishamalizana nao (Serikali) ila hawatoi elimu, watoke nje wakatoe elimu, watu waweze kuelewa, huo ndio mgogoro tulio nao. Lakini mambo ya kikokitoo sisi huko tulishatoka,” alisema.
Alipoulizwa nini mkakati wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi (PSSSF) kutoa elimu juu ya kikokotoo hicho baada kugonga mwamba CWT juzi, Meneja Uhusiano na Elimu kwa wanachama wa mfuko huo, James Mlowe aliahidi kulitolea ufafanuzi suala hilo leo.
Hata hivyo, Mwenyekiti wa Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Elimu ya Juu Tanzania (THTU), Dk Paul Loisulie, alisema hata kwao bado kuna vuguvugu halijapoa watu wametulia tu lakini iko siku wataibuka.
Alisema inahojiwa kwa nini wabunge wapewe mafao yote lakini wafanyakazi wapangiwe kiwango cha kupewa na kwanini mifuko ya hifadhi ibaki na fedha yao nyingi.
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Katiba na Sheria, Dk Joseph Mhagama alisema kabla ya Mei Mosi mwaka huu, Serikali iliieleza kamati hiyo kuwa wamekubaliana na wadau waliridhika na kikokotoo hicho kipya ambacho ni asilimia 33.
“Maoni yangu ni kwamba ieleweke uamuzi ulifanyika collectively (kwa ushirikiano), kwa maana kulikuwa na mashauriano, haukuwa uamuzi wa upande mmoja, maana yake Serikali ilikaa na wadau na kufikia mwafaka wa asilimia 33,” alisema.
Dk Mhagama alisema ni vyema kama hawajaridhika (CWT), Serikali ione umuhimu wa kufanya mashauriano na wadau ili kupata uelewa wa pamoja kuhusu hatua hizo zilizochukuliwa.
Kwa upande wake Dinah alisema kabla ya kukutana mwezi ujao katika Mkutano mkuu wa CWT, watamweleza Waziri mwenye dhamana hisia za wanachama kuhusu kikokotoo. Hata hivyo, alisema baada ya kutangazwa kwa kikokotoo hicho kipya Mei mwaka huu, jambo hilo limefanyiwa kazi kwa muda mrefu na wameshirikishana.
“Kwa upande wetu ambao kikokotoo kilikuwa asilimia 50 na kushushwa kuwa asilimia 33, nadhani tutapata mshtuko lakini hali ndivyo ilivyo kwa kuwa tumeelezwa kwanini tumefikia hapa na faida zake bila kujali waliokuwa asilimia 50 au asilimia 25 lakini kubwa ni mifuko kuwa endelevu,” alisema.
MWANANCHI