[QUOTE="ukh
Tatizo linaanzia katika mfumo wa elimu.
Elimu ni jambo la kwanza kwa umuhimu katika taifa lolote; lakini, inasikitisha kwamba, mitaala ya elimu haikidhi mahitaji ya mazingira, na vile vile elimu inachangia uoga na ajinga kwa kiasi kikubwa.
Vijana wengi sana wanaamini katika kusoma ili waajiriwe, na hawana wazo la kuanzisha biashara zao wenyewe.
Mfano, utakuta mtu ana masters ila kaajiriwa na mtu asiye soma au aliyesoma kidogo. Hapa maana yake ni kwamba, huyu mwajiri hana elimu ila ni jasiri kuliko mwenye elimu ya masters.
Kwa hiyo elimu na mtaala wake kwa ujumla, unaua ubunifu kwa vijana.
Siasa nazo si rafiki kwa vijana.
Takwimu zinaonyesha kuwa asilimia 70+ ya Watanzania wanategemea kilimo.
Lakini cha ajabu ni kwamba, bajeti katika kilimo ni ndogo sana ukilinganisha na sekta nyingine.
Vile vile, mitaala ya elimu haijakipa kilimo kipaumbele cha kutosha.
Masoko ya mazao si rafiki na sera za kupiga marufuku usafirishaji wa mazao nje ya nchi unawaumiza sana wakulima, na inafifisha kilimo biashara.
Mimi binafsi ni mhitimu wa shahada, lakini nimejikita katika ujasiriamali wa kilimo biashara
Ni hayo tu
ukhuty