Tufanyeje kurejesha uzalendo Tanzania?

Tufanyeje kurejesha uzalendo Tanzania?

Hivi Uzalendo huo wa ' "...Kutovunja sheria za nchi yako..." ni Upi haswa?

ni nchi gani inaongoza Duniani kuwa na sifa hizo?
Ni tafsiri (coined by the political bureaucrats) na kuwekwa kwenye mtaala ili tufunzwe kwenye somo la siasa, practically baada ya kuhitimu shule inadhihiri kwamba tulikuwa brainwashed, kwa sababu inathibitika kwamba keki ya taifa kumbe hainaga mgawanyo sawia kwa wana wa nchi na hii inastawisha umaskini ambao ukikomaa hupoteza uzalendo.
 
Uzalendo tafsiri yake nyepesi ni kutokuvunja sheria za nchi yako.
Hii ni tafsiri ya kijinga kabisa kuwahi kuisoma. Uzalendo ni kuipenda nchi yako na watu wake, nukta!

Kurudisha uzalendo ni rahisi sana. Wanasiasa na vyama vyao na nchi na vyombo vyake vianze kuwa wazalendo kwanza. Wananchi watafuata mkondo naturally!

Umeweka picha ya Mwalimu hapo, aliipenda nchi yake na watu wake na ndio maana wananchi wakafuata mkondo.
 
Ni tafsiri (coined by the political bureaucrats)
Hawa "political bureaucrats" wa nchi gani mahususi?
na kuwekwa kwenye mtaala ili tufunzwe kwenye somo la siasa,
Ili nielewe, hao political bureaucrats waliweka tafsiri inayosema...au kwa lugha nyepesi...waliobambika tafsiri ya kuwa "kutovunja sheria ya nchi yako" ...ni Uzalendo na wamefanya hivyo kwa kuweka kwenye mitaala ya shule?
practically baada ya kuhitimu shule inadhihiri kwamba tulikuwa brainwashed, kwa sababu inathibitika kwamba keki ya taifa kumbe hainaga mgawanyo sawia kwa wana wa nchi na hii inastawisha umaskini ambao ukikomaa hupoteza uzalendo.
lbda najixnganya. Huu Uzalendo na mashaka nao...

Ukikosa kipande kizuri cha keki ya Taifa
...unaweza kuwa maskini, na ukiwa maskini unapoteza Uzalendo kwa kuwa tumefundishwa uzuzu na Wanasiasa?

hivyo basi
Tung'ang'anie kupata kipande kikubwa cha keki ili tuepuke umasikini ili tuwe Wazalendo.

Tuepuke mitaala inayoshawishiwa na political bureaucrats katika elimu za siasa ambamo inatufanya tuwe "brainwashed" na kutojali Uzalendo.
 
Hii ni tafsiri ya kijinga kabisa kuwahi kuisoma. Uzalendo ni kuipenda nchi yako na watu wake, nukta!

Kurudisha uzalendo ni rahisi sana. Wanasiasa na vyama vyao na nchi na vyombo vyake vianze kuwa wazalendo kwanza. Wananchi watafuata mkondo naturally!

Umeweka picha ya Mwalimu hapo, aliipenda nchi yake na watu wake na ndio maana wananchi wakafuata mkondo.
Kamaradi Stefano,

Tuelimishe zaidi kwenye haya:-

Vipi ukiipenda nchi yako lakini unavunja sheria zake huo ni uzalendo?

Vipi Peter Greenberg anayeipenda nchi limbwende Tz ni mzalendo?

Wawekezaji wa kigeni wanaoipenda nchi ni wazalendo (kama pia hawavunji sheria zake)?

Wakurugenzi wa makampuni ya kigeni yaliyoingia mikataba tata na taifa ni wazalendo?

Hivi uzalendo unahusu uraia?

Kwenye mchango wako aya ya pili na tatu umenishawishi kwa ziada Kamaradi Stefano.
 
Uzalendo tafsiri yake nyepesi ni kutokuvunja sheria za nchi yako.

Chanzo cha uzalendo kutoweka ni umasikini ambao unatia watu tamaa siyo tu ya kulimbikiza mali kwa wastani na ziada, bali kutafuta chochote cha kuokoa roho/uhai kwa maana ya mahitaji ya msingi ya chakula, malazi na mavazi ambayo haya nayo yamekuja kuwa changamoto kwenye jamii pasina ufumbuzi kupatikana.

Nchi zote zilizoendelea duniani zilitanguliza na kulinda uzalendo.

Tufanyeje kurejesha uzalendo Tanzania?

Toa ushauri wako ukijuwa kwamba kutoweka kwa uzalendo nchini/kwenye jamii kunakuathiri na kizazi chako.

View attachment 2233208 View attachment 2233211
Taswira zote kwa hisani ya google.
Tanzania ilijifunza ubinafsi kwa njia mbaya, ndiyo maana uzalendo ukavunjika. Kabla ya Utawala wa Mwinyi, nchi ilikuwa na uzalendo sana, ila hali ya uchumi aliyokuta Mwinyi ikamlazimisha kukubaliana masharti ya IMF na World bank, ambayo yalitaka kubinfsisha mashirika yote. Sasa kuanzia pale ndipo ubinafsi ukaanza, na hivyo ni ubinafsi ulioanza kwa njia mbaya sana iliyosukumwa ya shida. Ubinafsi huo ndio umeondoa uzalendo kabisa nchini.

Mtanzania akiambiwa ahujumu nchi ili apate pesa, atafanya hivyo. Unaona kuwa kuna watanzania waliokuwa wanashabikia ndege za ATCL kukamatwa nje ya nchi, na kuna watanzania waliokuwa wakishiriki katika sakata hilo ili wapate hela. Kuna watanzania walioshirikiana na makampuni ya madini kuihujumu serikali mapato yake mradi wao wapate kitu fulani. Maafisa wa kodi walikuwa mbele sana kuhujumu mapato ya serikali ili wazipate wao. Mifano ni mingi sana. Kuna Wakati Magufuli alishindanishwa na Rais Akufo kwenye Tuzo fulani, Watanzania wakawa mbele sana kumpigia kampeini Akufo na kumponda Magufuli katika medani ya Kimataifa. Kuna Wakati Diamond alikuwa kwenye kipengele fulani cha tuzo za BET, watanzania wakapiga kempeini sana asipate tuzo katika medani ya kimataifa.

Utashangaa nchi kama Kenya pamoja na kwamba wana matatizo ya Ukabila kwa muda mrefu, lakini linapokuja swala la uzalendo kwa nchi yao, wako juu sana na wanakuwa kitu kimoja. Wote wanajivunia na kulinda kilicho cha Kenya bila kujali itikidi na makabila yao.
 
Tanzania ilijifunza ubinafsi kwa njia mbaya, ndiyo maana uzalendo ukavunjika. Kabla ya Utawala wa Mwinyi, nchi ilikuwa na uzalendo sana, ila hali ya uchumi aliyokuta Mwinyi ikamlazimisha kukubaliana masharti ya IMF na World bank, ambayo yalitaka kubinfsisha mashirika yote. Sasa kuanzia pale ndipo ubinafsi ukaanza, na hivyo ni ubinafsi ulioanza kwa njia mbaya sana. Ubinafsi huo ndio umeondoa uzalendo kabisa nchini.

Mtanzania akiambiwa ahujumu nchi ili apate pesa, atafanya hivyo. Unaona kuwa kuna watanzania waliokuwa wanahsbaikia ndege za ATCL kukamatwa nje ya nchi, na kuna watanzania waliokuwa wakishiriki katika sakata hilo ili wapate hela. Kuna watanzania walioshirikiana na makampuni ya madini kuihujumu serikali mapato yake mradi wao wapate kityu fulani. Maafisa wa kodi walikuwa mbele sana kuhujumu mapato ya serikali ili wazipate wao. Mifano ni mingi san.

Utashangaa nchi kama Kenya pamoja na kwamba wana matatizo ya Ukabila kwa muda mrefu, lakini linapokuja swala la uzalendo kwa nchi yao, wako juu sana na wanakuwa kitu kimoja. Wote wanajivunia na kulinda kilicho cha Kenya bila kujali itikidai na makabila yao.
Kamaradi Kichuguu,

Umeongea kitu real!

Kwenye mauaji ya Kenya 2007-2008, Wakenya waliheshimu mitaji iliyowekezwa bila kuihujumu wakijuwa baada ya vita watataka kurudi kwenye ajira zao ili maisha yaendelee na vizazi vyao (uzalendo wa kutovunja sheria huu) ndiyo maana baada ya machafuko yale Kenya haikushuka kwenye FDI wala uchumi haukuyumba. Waliuana kikabila kati ya staff na staff lakini hawakuchoma wala kuiba kiwanda, unique!

Hapa Tz tunahujumu mali za umma (kama ulivyosema) hata bila nchi kuwa vitani.
 
Kamaradi Kichuguu,

Umeongea kitu real!

Kwenye mauaji ya Kenya 2007-2008, Wakenya waliheshimu mitaji iliyowekezwa bila kuihujumu wakijuwa baada ya vita watataka kurudi kwenye ajira zao ili maisha yaendelee na vizazi vyao (uzalendo wa kutovunja sheria huu) ndiyo maana baada ya machafuko yale Kenya haikushuka kwenye FDI wala uchumi haukuyumba. Waliuana kikabila kati ya staff na staff lakini hawakuchoma wala kuiba kiwanda, unique!

Hapa Tz tunahujumu mali za umma (kama ulivyosema) hata bila nchi kuwa vitani.
Tuko tayari hata kuvunja viti vya Uwanja wa Taifa kwa sababu za kibinafsi bila kujua kuwa hiyo ni mali ya walipakodi wa Tanzania.
 
You have said it all Yoda.

Ila hata hii ya sasa nayo ikipata msimamizi na mtekelezaji mzuri huenda uzalendo ukarejea. Mwl alitumia hii hii.

Mwalimu aliongoza maiti hai. Siku CCM itaacha kutawala nchi hii kwa shuruti uzalendo utakuwepo.
 
Uzalendo kwa itikadi ya ccm ni kisifia viongozi wakuu hasahsa rais. Kwa itikadi yetu sisi wengine huo ni unyumbu

Kipindi cha Magufuli ilikuwa ngumu kutofautisha uzalendo na ujinga.
 
Tuko tayari hata kuvunja viti vya Uwanja wa Taifa kwa sababu za kibinafsi bila kujua kuwa hiyo ni mali ya walipakodi wa Tanzania.
Ngoswe penzi kitovu cha uzembe na Edwin Semzaba, ni kitabu kilichoandikwa miaka mingi lakini kumbe kilikuwa kinaona leo!

Ni kitabu ambacho nafikiri Polisi ingeruhusiwa kutandika watu viboko kukisoma kwa ulazima ili kupandikiza maarifa yaliyomo hasa kada ya utumishi wa umma na wasomi.

Ameibua dhamira kuhusu mambo yanayoigusa jamii ya leo kama vile uzembe, madhara ya ulevi, uzembe kazini, suala la matabaka kati ya mjini na vijijini. Mtazamo, falsafa na msimamo wake ni kulenga kuibadilisha jamii na kuleta maendeleo.

Mada zake:
1. Ulevi na ufisadi wa wasomi.
2. Kurubuni watoto wa kike wa shule kukatisha masomo.
3. Tofauti ya viwango vya maisha mijini na vijijini kunakovuta vijana wengi kukimbilia mijini kutelekeza mashamba na mifugo vijijini.
4. Ametumia sensa kufikisha ujumbe.

Ufisadi leo umetambuka hadi kusafirisha wanyama hai na binadamu (human trafficking).

1653158146289.png

Taswira kwa hisani ya google.
 
Kamaradi Stefano,
Majina ya Kikomunisti haya siyapendi kama nini 😉

Tuelimishe zaidi kwenye haya:-

Vipi ukiipenda nchi yako lakini unavunja sheria zake huo ni uzalendo?
Sheria yoyote inayoumiza nchi au wananchi haina uzalendo ndani yake na wazalendo wanajua cha kufanya.

Vipi Peter Greenberg anayeipenda nchi limbwende Tz ni mzalendo?
Huyo Pita ni raia wa Bongo?

Wawekezaji wa kigeni wanaoipenda nchi ni wazalendo (kama pia hawavunji sheria zake)?
Kwani Tanzania ni nchi yao?

Wakurugenzi wa makampuni ya kigeni yaliyoingia mikataba tata na taifa ni wazalendo?
Duh!

Hivi uzalendo unahusu uraia?
Wewe ni mzalendo wa Marekani? UK? uganda? Malawi?
Kwenye mchango wako aya ya pili na tatu umenishawishi kwa ziada Kamaradi Stefano.
GTH
 
Back
Top Bottom