aleesha
JF-Expert Member
- Oct 17, 2016
- 798
- 1,178
Kukamatwa watu kula Mchana Zanzibar ~ Watanganyika wasio Waislamu wamezusha Mjadala.
Ni vyema tukafahamu ya kuwa MILA, DESTURI, SILKA na UTAMADUNI ni mfumo wa maisha kamili ya kila jamii. Zanzibar kwa karne nyingi imekuwa ikitajika na kusifika ikafikia kubandikwa jina Tolerance Country. Kwa miongo kadhaa iliyopita zimeanza kuja hizi nganu zenye sura ya udini kwa lengo lile lile kama unataka kumuua mbwa mpe jina baya. Hayo yamekuja kutoka kwenye kundi fulani la kisiasa na kudhani ni mtaji kwao kumbe ni kuizamisha Zanzibar.
Sina hakika kama katazo la kula HADHARI mchana wa RAMADHANI lipo kisheria au la. La muhimu, kuna watu wanadhani katazo la kula hadharani mchana wa mwenzi mtukufu wa ramadhani ni katazo makhsusi kwa Watanganyika na Wakiristo. Wasichotaka kukifahamu katazo linamlenga kila binaadamu wakiwemo Wazanzibari na Waislamu wenyewe.
Kwa faida ya anaetaka kufaidika mwanamke wa Kiisilamu hawezi kufunga mwezi mzima (29/30) kutokana na sababu za kimaumbile hivyo mwanamke huyu ndani ya nyumba yetu tumezaliwa, tumelelewa na kukua pamoja mimi huwa siijui ni lini yupo ndani ya siku zake (hedhi). Nakusudia kusema ndani ya myumba yetu wakati yeye anaudhuru wa kisheria anaruhusiwa kula siku hizo (baada ya ramadhani anakuja kuzilipa) basi pia huwa anakula kwa kujificha. Huwa hali mbele yetu tukimuona.
Kuna wagonjwa nao wanaruhusiwa kula kisheria (wakipona wanakuja kulipa na wasipopona wanatolewa fidia). Wakiwa ndani ya nyumba lakini mfumo wao wa kula unakuwa ni tofauti na miezi mengine yote.
Kuna watoto ambao hawajatimia umri wanaruhusiwa kula basi hawa watoto pia huwa hawali ovyo ovyo majiani wana utaratibu wameekewa wao wenyewe wanaifahamu na kuiheshimu ramadhani kupita kiasi.
Mfano ulio hai watoto wangu mimi binafsi wanakwenda skuli na chuoni huwa wanapewa fursa warudi myumbani kula kisha warudi tena skuli au chuoni kuendelea na vipindi, mwanangu mmoja anakwenda nyumbani kula na kurudi skuli mtoto mmoja haendi anaona aibu kuwa ataitwa KOBE (jina la utani kwa mtoto asiyefunga) jaribu kufikiria mtoto wa miaka 7 anaona aibu kugundulika kuwa hakufunga anahiyari abakie skuli asirudi nyumbani kula kwa kuchelea asijulikane kuwa ni kobe!
Tulio zaliwa na kukulia Zanzibar kwa miongo kadhaa tumewashuhudia wageni kutoka mabara ya mbali wakiuheshimu utamaduni huu. Ajabu iliyoje majirani zetu na ndugu zetu wa karibu tulitegemea wao ndio wawe sehemu kutoa elimu hii badala kuhoji kwani Zanzibar na Tanganyika ni nchi tofauti? Tanganyika kuna baadhi ya MILA na TAMADUNI hakuna Zanzibar. Kadhalika Zanzibar kuna baadhi MILA na TAMADUNI hazifanani kabisa na Tanganyika si ajabu.
Zanzibar wapo Wakiristo tumezaliwa nao na kucheza nao tumekuwa wote hakuna hata siku moja Mkiristo wa Zanzibar anaweza kufanya upuuzi wa kula hadharani mchana wa ramadhani.
Siungi mkono watu kujichukulia sheria mikononi lakini vile vile sikubaliani na watu ambao hawana tolerance ya kuheshimu utamaduni wa wengine na kudhani wao pekee wana haki ya kuingia kwenye nyumba ya mtu na kufanya anachoona yeye ni sawa kwake. Heshima ni kitu cha bure kwani mtu akichukuwa chakula chake na kuenda kula ndani kwake kuna tatizo gani? Karaha ya kula mchana wa mwezi mtukufu wa ramadhani watu wanadhani inawahusu Watanganyika na Wakiristo tu, haya yashawafika hata Wazanzibari na Waislamu. Kosa linalofanyika ni kule kujichukulia sheria mikononi na kupelekea kuumiza watu.
Sisi tulipo nchi za wamaharibi kuna mambo mengi tumezuiwa tusifanye na tunaheshimu hizo taratibu. Mfano sisi tuna msikiti lakini ni marufuku kuadhini kwa bomba (spiker) kwa hiyo tunaadhini kimya kimya na kusali kimya kimya tumepungukiwa nini kwenye imani yetu?
Assallam aleykum.
Ni vyema tukafahamu ya kuwa MILA, DESTURI, SILKA na UTAMADUNI ni mfumo wa maisha kamili ya kila jamii. Zanzibar kwa karne nyingi imekuwa ikitajika na kusifika ikafikia kubandikwa jina Tolerance Country. Kwa miongo kadhaa iliyopita zimeanza kuja hizi nganu zenye sura ya udini kwa lengo lile lile kama unataka kumuua mbwa mpe jina baya. Hayo yamekuja kutoka kwenye kundi fulani la kisiasa na kudhani ni mtaji kwao kumbe ni kuizamisha Zanzibar.
Sina hakika kama katazo la kula HADHARI mchana wa RAMADHANI lipo kisheria au la. La muhimu, kuna watu wanadhani katazo la kula hadharani mchana wa mwenzi mtukufu wa ramadhani ni katazo makhsusi kwa Watanganyika na Wakiristo. Wasichotaka kukifahamu katazo linamlenga kila binaadamu wakiwemo Wazanzibari na Waislamu wenyewe.
Kwa faida ya anaetaka kufaidika mwanamke wa Kiisilamu hawezi kufunga mwezi mzima (29/30) kutokana na sababu za kimaumbile hivyo mwanamke huyu ndani ya nyumba yetu tumezaliwa, tumelelewa na kukua pamoja mimi huwa siijui ni lini yupo ndani ya siku zake (hedhi). Nakusudia kusema ndani ya myumba yetu wakati yeye anaudhuru wa kisheria anaruhusiwa kula siku hizo (baada ya ramadhani anakuja kuzilipa) basi pia huwa anakula kwa kujificha. Huwa hali mbele yetu tukimuona.
Kuna wagonjwa nao wanaruhusiwa kula kisheria (wakipona wanakuja kulipa na wasipopona wanatolewa fidia). Wakiwa ndani ya nyumba lakini mfumo wao wa kula unakuwa ni tofauti na miezi mengine yote.
Kuna watoto ambao hawajatimia umri wanaruhusiwa kula basi hawa watoto pia huwa hawali ovyo ovyo majiani wana utaratibu wameekewa wao wenyewe wanaifahamu na kuiheshimu ramadhani kupita kiasi.
Mfano ulio hai watoto wangu mimi binafsi wanakwenda skuli na chuoni huwa wanapewa fursa warudi myumbani kula kisha warudi tena skuli au chuoni kuendelea na vipindi, mwanangu mmoja anakwenda nyumbani kula na kurudi skuli mtoto mmoja haendi anaona aibu kuwa ataitwa KOBE (jina la utani kwa mtoto asiyefunga) jaribu kufikiria mtoto wa miaka 7 anaona aibu kugundulika kuwa hakufunga anahiyari abakie skuli asirudi nyumbani kula kwa kuchelea asijulikane kuwa ni kobe!
Tulio zaliwa na kukulia Zanzibar kwa miongo kadhaa tumewashuhudia wageni kutoka mabara ya mbali wakiuheshimu utamaduni huu. Ajabu iliyoje majirani zetu na ndugu zetu wa karibu tulitegemea wao ndio wawe sehemu kutoa elimu hii badala kuhoji kwani Zanzibar na Tanganyika ni nchi tofauti? Tanganyika kuna baadhi ya MILA na TAMADUNI hakuna Zanzibar. Kadhalika Zanzibar kuna baadhi MILA na TAMADUNI hazifanani kabisa na Tanganyika si ajabu.
Zanzibar wapo Wakiristo tumezaliwa nao na kucheza nao tumekuwa wote hakuna hata siku moja Mkiristo wa Zanzibar anaweza kufanya upuuzi wa kula hadharani mchana wa ramadhani.
Siungi mkono watu kujichukulia sheria mikononi lakini vile vile sikubaliani na watu ambao hawana tolerance ya kuheshimu utamaduni wa wengine na kudhani wao pekee wana haki ya kuingia kwenye nyumba ya mtu na kufanya anachoona yeye ni sawa kwake. Heshima ni kitu cha bure kwani mtu akichukuwa chakula chake na kuenda kula ndani kwake kuna tatizo gani? Karaha ya kula mchana wa mwezi mtukufu wa ramadhani watu wanadhani inawahusu Watanganyika na Wakiristo tu, haya yashawafika hata Wazanzibari na Waislamu. Kosa linalofanyika ni kule kujichukulia sheria mikononi na kupelekea kuumiza watu.
Sisi tulipo nchi za wamaharibi kuna mambo mengi tumezuiwa tusifanye na tunaheshimu hizo taratibu. Mfano sisi tuna msikiti lakini ni marufuku kuadhini kwa bomba (spiker) kwa hiyo tunaadhini kimya kimya na kusali kimya kimya tumepungukiwa nini kwenye imani yetu?
Assallam aleykum.