Tuhuma dhidi ya JK zaikoroga CCM



inaonekana hufuatilii mambo...watu wameanza kupigia kelele udhaifu wa jk tangu siku za kwanza ......hawajaanza leo....

na werevu walijua tangu mwanzo kuwa ni BOMUUU!!
 
Lakini kwa huyu bwana yamezidi.....na kuombwa kuishawishi Marekani eti kuwaondolea vizuizi Cuba, nguvu hiyo hana....fuatilia uone...


Ikitokea kaweza kuishawishi? maana yeye ni Rais wa kwanza kuarikwa white house na Obama hivi Obama anaarika Marais wadhaifu?
 


Kwahiyo mkuu unataka kusema Rais Obama anapenda kuwa na marafiki zake Wadhaifu kama JK, WAHENGA WALISEMA NDEGE WANAOFANANA HURUKA PAMOJA HIVYO OBAMA NAE NI DHAIFU?KWA MAANA HIYO WAMAREKANI NAO NI WAKUBUZWA KAMA WA TZ NDIYO MAANA WAKAMCHAGUA RAIS DHAIFU?
 
Wahenga walisema uzee dawa. Lakini ukifuatilia hoja na maneno ya baadhi ya wazee wetu kama Makamba unajiuliza kama kweli bado huu usemi wa wahenga unaendelea kuwa na maana iliyotarajiwa.
Usemi wa wahenga (busara zisizopinda) ni zaidi ya urithi, hivyo mjinga mmoja kama huyu hawezi na wala asepewe nafasi ya kuwafanya wazee wote waonekane mbumbumbu. Hivyo inabidi tumchukulie kama wale wazee wanaobaka watoto wadogo, kitendo hiki kimetokea mara nyingi lakini sio kibali cha wazee wote kudharaulika.
 
Matheo Qares na Bwana Mussa walikuwa wapi jamani? Bila shaka baad ya kufulia wana tamaa ya kurudi ulingoni.Poor guys! Mmeshakuwa spent force na njia ya kurudi ulingoni mliyotumia ni non starter!
 
ikitokea kaweza kuishawishi? Maana yeye ni rais wa kwanza kuarikwa white house na obama hivi obama anaarika marais wadhaifu?


marekani hawafanyi kitu bure bila manufaa...hata wakati walipokuwa wamemfanya blair akaitwa kambwa ka bush[poodle] walitaka uingereza ipeleke majeshi iraq na afrighanistan......

marekani wanapenda ku take advantage ya marais wadhaifu..........they called them good men!!!..wanataka uranium yetu na madini mengine.......wewe unafikiri rais anatakiwa apendwe na wageni au raia wake!!! Anawajibika kwa nani mwisho wa siku!!!
anayejuwa uzuri au ubaya wa mke ni mwenye mke...........sio hawara!!!
 
Kuna 'mentality' ambayo naamini si nzuri, tunayo Watanzania. Hata kama mtu alikuwa kiongozi huko nyuma, akapigwa chini (kufulia), haruhusiwi kutoa maoni yake? Kuna watu wanaamini kabisa kwamba, Malecela, Mkapa, Sumaye, Salim, Warioba, Salimin, Jumbe, na wengineo wote waliowahi kushika madaraka huko nyuma, hawaruhusiwa kuukosoa uongozi uliopo madarakani. Ni kweli hivi ndivyo inavyotakiwa?
 
Kwa kiasi fulani wazee wetu hawa wanafanya hivyo sio kwa kuipenda NCHI yao. Wanafanya hivyo kwa kuwa utawala wa sasa umewatupa nje. Hawana ushawishi tena. Wengine kwa kuwa "mgombea wao" hakufanikiwa. Vinginevyo kuukosoa uongozi ulioko madarakani huku uking'ang'ania kuwa mwanachama wa chama hichohicho ni kichekesho.
 
Makambaaaaaaaa anapalilia kibarua ata ungekuwa wewe ungefanya.
ILA JK kwa sasa ni sikio la kufa lisilosikia dawa kwa kweli,utashangaa next year CCM watampitisha tena kwa kishindo mimi nipo
 


Kwa points zako unazoongelea kutaka kuthibitishiwa udhaifu wa Mheshimiwa Rais kama baba yetu Makamba anavyo taka kuthibitishiwa kila kitu wakati hali halisi inaonekana hata kwa mwanafunzi wa Darasa la saba inanipa mashaka sana.

Rais wa Cuba Mr Raul kumwomba Rais JK kuishawishi Marekani haina maana ya udhaifu au ushupavu. Unaweza mwomba mtu kukusaidia kitu endao waona labda ana ukaribu au hata mazingiza yake yana ruhusu kukutana na yule mhitaji wako.


Si lazima uwe shupavu au jasiri ktk kumwombea mtu msaada.Hata wewe waweza mwomba mkeo msaada wa kwenda toa taarifa kazini endapo utaugua ghafla.

Tuukubali ukweli japo unauma..!! Anguko la utawala wa mheshimiwa ni aibu kubwa kwa watu tuliomtegemea.!! Tujaribu kubadirika na kuondokana na viongozi matapeli wa maneno matamu yenye asali..Tunahitaji vitendo kwa sasa...!!
 

Hayo ni mawazo yako. Kwani walichoongea ni uongo??? Bila Mkulu kumshughurikia RA (Kagoda) atapata shida sana, na Mungu anasikia kilio cha watu maskini.
 


Mkuu si siri mtu mwenye "mentality" ya jinsi hii ana kasoro au ameathirika physiologically , na anajaribu kuwashawishi watu wenye upeo wa kuchambua mambo waamini ule ujinga wake..!

Kama hututokubali kukosolewa basi hatutoweza kubadirika hata kidogo..!! Mzee Makamba lazima akubaliane na hali kwamba wakati wa porojo porojo na kunukuu mistari ya Bibilia na Miswafu ulishapitwa na wakati.

Huwezi kulazimisha picha ya kibakuli kuwa picha ya sahani japo zote ni picha za vyombo vya kulia chakula ..!!
 

Unajua Mkuu hata Mangula na marehemu Kolimba walipokuwa madarakani hawakuoni ubovu wa chama chao lakini walipokuwa nje waliona kasoro zote. Kumbuka Kolimba alivyosema kuwa CCM imekosa dira jinsi alivyoshukiwa na hata kufa!! leo hii Mangula naye ameona haya.. Usishangae Makamba akitoka ndio ataona kuwa alikuwa anatetea pumba!!
 
Makamba awatukana wanaoshauri Kikwete asigombee 2010

Na Leon Bahati

KATIBU mkuu wa CCM, Yusuf Makamba, ambaye katika miezi ya karibuni amekuwa akihaha kutoa ufafanuzi, kukanusha au kujibu tuhuma mbalimbali dhidi ya chama hicho tawala, jana alikuwa na kazi nyingine ya kumtetea Jakaya Kikwete baada ya waziri katika serikali ya awamu ya tatu kushauri asiteuliwe kugombea urais 2010 iwapo atashindwa kufanya maamuzi magumu dhidi ya mafisadi.

Safari hii, Makamba alitumia maneno makali kumjibu waziri huyo, Matheo Qares akisema watu wenye fikra kwamba CCM inaweza kumtosa mwenyekiti wake kwenye mbio za urais wakati wa uchaguzi mkuu wa mwakani, "ni wehu".

Qares, ambaye aliwahi kushika wadhifa nyeti wa Waziri wa Menejimenti ya Utumishi wa Umma, alitoa rai hiyo juzi kwenye kongamano la kumuenzi muasisi wa taifa la Tanzania aliposema kuwa CCM haina budi kutafuta mwanachama mwingine wa kugombea nafasi ya urais mwaka 2010 iwapo Kikwete atashindwa kufanya maamuzi magumu dhidi ya mafisadi, ambao alisema hawakijui chama na wengine uraia wao una utata.

Lakini jana, Makamba alisema watu wenye fikra hizo ni wehu kwa kuwa uteuzi wa wagombea ndani ya CCM ni mchakato usiotoa ruhusa kwa mawazo binafsi ya watu.

"Mtu mwenye akili nzuri hawezi kusema kwamba Rais Kikwete ameshindwa kutekeleza wajibu wake. Anayefikiria hivyo, ni mwehu," alisema Makamba alipotakiwa kutoa maoni yake kuhusu kauli hizo.

Alisema ni vyema watu hao wakafahamu kuwa mgombea urais wa CCM anateuliwa kwa mujibu wa taratibu za chama kupitia vikao mbalimbali hivyo, wazo binafsi halina nafasi.

Alipoulizwa kuhusu shutuma zinazoelekezwa kwa Rais Kikwete, Makamba alisema asingependa kujibu hoja zilizotolewa na mjumbe mmoja mmoja kwenye kongamano hilo.

Lakini akaeleza kwamba yupo tayari kutoa maoni yake binafsi baada ya Taasisi ya Mwalimu Nyerere kuwasilisha kwake mapendekezo waliyofikia kwenye kongamano hilo.

"Mimi mwenyewe sikuwepo kwenye kongamano hilo. Wala sijui mapendekezo yao. Siwezi nikatolea maoni hoja za mtu mmoja mmoja alizotoa kwenye Kongamano hilo. Nitakapopata mapendekezo ya jumla ya taasisi hiyo, nitakawa katika nafasi nzuri ya kutoa maoni yangu."

Katika kongamano hilo, Rais Kikwete amekuwa akilaumiwa kwa kutochukua hatua dhidi ya watu wanaotuhumiwa kwa ufisadi, wengi wao wakielezwa kuwa ni wafanyabiashara ambao wanatuhumiwa kukiteka chama kwa kutumia nguvu zao za pesa.

Wakati fulani Joseph Butiku, mwenyekiti wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere ambayo iliandaa kongamano hilo, alisema Rais Kikwete amezungukwa na mafisadi ambao wanaitafuna nchi.

Akizungumza kwenye kongamano hilo juzi, Qares alisema rais hana budi kufumba macho na kuwashughulikia hao watuhumiwa ambao wanadai Kikwete hakujuana nao barabarani na kama atashindwa basi ashauriwe kuwa miaka yake mitano inamtosha.

Kabla ya Qares, Musa Nkangaa, ambaye aliwahi kuwa waziri kwenye serikali ya awamu ya pili, aliituhumu CCM kuwa imepoteza hadhi na kujikuta ikikumbatia matajiri wachafu.

Kwa mujibu wa Nkangaa, CCM imekuwa si chama cha wakulima na wafanyakazi tena, bali kimebaki kuwa chama cha matajiri.

"Ndiyo maana imekuwa ikiweweseka kuwashughulikia watuhumiwa wa Richmond na Kagoda," alisema akimaanisha kashfa ya utoaji zabuni ya ufuaji umeme wa dharura kwa Richmond Development Company LLC na tuhuma za wizi wa mabilioni ya fedha kutoka BoT.
 


Na kocha mzuri wa mpira si lazima na yeye awemo uwanjani !!
 
Hypothesis 1: Kwa Makamba kuendelea 'kula' inategemea sana uwepo wa Jk madarakani kama Rais.
 
Wahenga walisema uzee dawa. Lakini ukifuatilia hoja na maneno ya baadhi ya wazee wetu kama Makamba unajiuliza kama kweli bado huu usemi wa wahenga unaendelea kuwa na maana iliyotarajiwa.

Dawa nyingine zime-expire mkuu, tehe tehe tehe😀
 
]Nyuki;686174]Siamini kama ni rais dhaifu Tanzania na Africa,hayo ni maono na fikra binafsi ambazo ni ruhusa mtu kutoa maoni kikatiba.

Kam kunauthibithisho wa udhaifu wa Rais JK basi uelezwe ili tuone ukweli wa habari hizi.
Udhaifu wake unatokana na kutothubutu kutoa maamuzi. Kila kitu kinaenda shaghala baghala. Hamna control ya mawaziri, watumishi, huoni kama huo ni udhaifu?

Hivi juzi Rais wa CUBA amekaririwa akimuomba Rais JK amsaidia kuishawishi Marekani kuondoa vizuizi iliyoiwekea CUBA.Sasa najiuliza hivi unawexza kwenda kumuomba usaidizi wowote ule kwa mtu aliyedhaifu?
Raisi wa CUBA hana data za utendaji wa JK. Inawezekana amechukua reference ya number of trips za Marekani alizofanya JK au pengine alikua anamkejeli. Angekua anamuheshimu angemtumia naibu waziri kumpokea?

Uozo wote tunaouona sana sidhani kama umetokea kwa awamu hii ya nne pekee,kwa awamu zote zilizopita kulikuwa na mapungufu mengi sana.
Bado unabakia kuwa ni uozo na wala haijustify uzaifu wake mkuu wangu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…