Guselya Ngwandu
Member
- Sep 17, 2021
- 39
- 84
Mbunge wa Misungwi, mmiliki wa timu ya Gwambina Alexander Mnyeti ameibua hoja zinazoonesha kuwa na rushwa katika mpira wa Tanzania.
"Wale watu wanataka uje kwenye mpira kwa ubabaishaji wakikuomba hela utoe,l a sivyo utapangiwa ratiba ngumu hadi uchukie. Unapangiwa kwenda Mbeya unacheza unarudi misungwi tena unarudishwa mbeya.
"Uwanja wangu unafungiwa una kila kitu napelekwa Nyamagana ambayo Kapeti limeshachubuka na choo hakuna cha Wageni wananitoa Kwangu ambapo hata mechi za CAF zinaweza kuchezwa hapo.
"Tatizo kuu lilianzia nlipokataa mechi ziende CCM Kirumba za Simba na Yanga wao wanataka hvyo ili wapige hela tu. Nmeamua kuona kuwa nimefaeli uwekezaji wa soka kwa sasa nasubiri hao mabwana najua hawatakaa Milele hapo TFF ndo nitarudi na mimi.
"Nimeshavunja timu na vijana nmeshawaruhusu waende makwao nashangaa TFF wanajitekenya na kucheka mara ooh tuipokonya Point Gwambina na Faini. Sasa wanawapokonya watu ambao hawapo?
"Lengo lao kuu lilikuwa Gwambina ashuke na Apotee na mimi nasema heri nishuke kabisa kuliko nina uwanja mzuri tena niwe nawalipa hela watu burebure."
Alisema Mbunge wa Misungwi Mnyeti kupitia Clouds FM.
"Wale watu wanataka uje kwenye mpira kwa ubabaishaji wakikuomba hela utoe,l a sivyo utapangiwa ratiba ngumu hadi uchukie. Unapangiwa kwenda Mbeya unacheza unarudi misungwi tena unarudishwa mbeya.
"Uwanja wangu unafungiwa una kila kitu napelekwa Nyamagana ambayo Kapeti limeshachubuka na choo hakuna cha Wageni wananitoa Kwangu ambapo hata mechi za CAF zinaweza kuchezwa hapo.
"Tatizo kuu lilianzia nlipokataa mechi ziende CCM Kirumba za Simba na Yanga wao wanataka hvyo ili wapige hela tu. Nmeamua kuona kuwa nimefaeli uwekezaji wa soka kwa sasa nasubiri hao mabwana najua hawatakaa Milele hapo TFF ndo nitarudi na mimi.
"Nimeshavunja timu na vijana nmeshawaruhusu waende makwao nashangaa TFF wanajitekenya na kucheka mara ooh tuipokonya Point Gwambina na Faini. Sasa wanawapokonya watu ambao hawapo?
"Lengo lao kuu lilikuwa Gwambina ashuke na Apotee na mimi nasema heri nishuke kabisa kuliko nina uwanja mzuri tena niwe nawalipa hela watu burebure."
Alisema Mbunge wa Misungwi Mnyeti kupitia Clouds FM.