Tuiombee sana CHADEMA

Unataka uenyekiti kwa kumshambulia Mwenyekiti aliepo hadharani
Kosa kubwa
 
Ujui hofu ya mbowe ipo wapi mbowe ana damu ya baadhi ya wanachadema tena siyo mbowe tu na genge lake hivyo wanajua wakiachia kiti ndiyo basi tena mambo yao yataanikwa ni kama samia tu samia ni ngumu kutokugombea 2025 kwa sababu ya damu zilizopo mkononi mwake
 
Huu mgogoro umesukwa kwa makini sana wakiwa na malengo makuu mawili. Mosi ni kujaribu kuibomoa Chadema kabla ya uchaguzi mkuu, pili kufififsho hoja za aibu ya uchaguzi wa serikali za mitaa 2024. Ghafla habari za Chadema zinaandikwa na kutangazwa na media zote za serikali!
 
Kwa nini wapambe wa Lissu hawataki akutane na Mbowe kwenye debe? Yaani Lissu kwa nini apite bila ushindani? Kuna mtu kamuengua Lissu? So yuko kwenye mpambano? Sasa mnalia nini?.
Kugombea nafasi moja na mtu mwenye mamlaka dhidi ya wasimamizi au waratibu wa huo uchaguzi ni ubatili. Mbowe lazima ashinde.
Mfano mkurugenzi wa wilaya au halmashauri au manispaa toka chama tawala ndiyo husimamia na kutangaza matokeo ya uchaguzi ambao mwanachama mwenzie anashindana na wapinzani.
 
Mshana, nimevunjika moyo mno na uamuzi wa Mbowe. Kwa maoni yangu , CHADEMA inabeba tumaini la mabadiriko kwa wale wanaooenda mabadiriko.Lakini sasa matumaini hayo yanafifia.Nionavyo mimi ,uamuzi wa Mbowe unatoa fursa kwa mfumo corrupt kupenyeza pesa chafu kwenye uchaguzi utakaofanyika ili kumpata mwenyekiti wa chama,au fitina tu ili Lissu ashindwe.Baada ya hapo Mbowe atampiga vita Lissu ili kupunguza upinzani wa ndani ya chama.


Na baada ya kushindwa ,naona kabisa Lissu hataweza tena kudumu Chadema.Busara tu ya kawaida ingemtuma Mbowe kustaafu kwa heshima na kumwachia Lissu ili apambane na ccm.Kwa sasa Mbowe hana jipya especially kwenye kupambana na ccm na mbinu zao chafu za kuiba kura .Tunahitaji mbinu na ujasiri mpya wa kupambana na wizi wa kura kwenye chaguzi za kitaifa,na Mbowe hana mbinu mpya .
 
Huu uchaguzi umefanya hata watu tulioona mna akili CHADEMA kuwa kumbe ni wajinga. Nashangaa na uchawi wako wote bado unaendelea kuota ndoto za mchana.
 
Haya majina ya M s vyepesi kwao kuachia madaraka...
Museven,mugabe,mobutu ,Mbowe...etl
 
Wakati watu wakimsema mbowe kuwa mwenyekiti wa Chadema muda mrefu wewe na wenzako mkasema ndio demokrasia nyinyi wanachama ndio munaamua kiongozi aendelee au asiendelee Sasa imekuaje leo mnapiga kelele
 
Mshanaa shiiiiihh usiwaamshe!!!
Anaamshaje aliyelala brother?!!! Ye ndo inabidi aamshwe.......aambiwe kuyakalia matatizo Huku ukikomaa kumnyoshea kidole jirani badala ya kubuni mbinu ya kuyamaliza ni uzwazwa ambao hautokuja kuleta faida hata miaka 1000.

Hata hivyo, Hivi ccm ya kuamshwa na chadema kweli?!!!! Jamani ee, hebu watoto nendeni tuition tupisheni kwanza jukwaani hapa.
 
Bado nina imani
Bado nina imani na mwamba atafanya tofauti.. Bado nina imani na CHADEMA! Hatuna mbadala😭
 
Huu uchaguzi umefanya hata watu tulioona mna akili CHADEMA kuwa kumbe ni wajinga. Nashangaa na uchawi wako wote bado unaendelea kuota ndoto za mchana.
Sina tatizo kabisa kwa asilimia 100 kwa lolote utakaloandika kuhusu mimi au CHADEMA kwakuwa wewe si mmoja wetu..🙏🏿🙏🏿🙏🏿
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…