Kipigo cha Taifa Star na Swailand 1-0 na kisha dhidi ya Madagascar Cha 2-0. Kimenifanya nitafakari sana na kukumbuka misemo ya Wahenga isemayo midomo uumba.Na hasa kauri za watu wazima [Wazee].
Kauli ya Rais Mstaafu Mzee Ally Hassan Mwinyi mmoja ya viongozi wenye busara za hali ya juu kuwahi kutokea Tanzania, alisema; "Soka ya Tanzania ni kichwa cha mwendawazimu, kila mtu anajifunzia kunyoa". Mzee Mwinyi alisema hayo, baada ya klabu ya Simba kufungwa na Stella Abidjan mabao 2-0 Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika fainali ya Kombe la CAF mwaka 1993. Na ninakumbuka aliwahi kurudia kusema hivyo; "Soka ya Tanzania bado kichwa cha mwendawaimu,", baada ya kushuhudia matokeo mengine mabaya.
Kauli hii nzito ambayo imekuwa kinywani mwa maisha ya Watanzania..toka ilipotolewa na kuendelea kuwa nukuu kila mara timu ya Taifa inapopokea kipigo toka kwenye timu za mataifa mengine, kauri hiyo imenifikilisha sana na kunipa muda wa kuona mimi kama Mtanzania nina sehemu gani katika kuona Taifa Star inatokana na kauri hiyo.
Watu wazima na viongozi wa dini watanielewa kwa haya nitakayosema ''MIDOMO YETU INAUMBA'' ndio kusema midomo ya Mzee Wetu Mwinyi nayo imeendelea kuumba.
Kilichotokea Kwa Kauri ile, ilikuwa ni matamanio ya Mzee Mwinyi kuona Taifa Star inashinda mechi zake kimataifa,lakini kila iliposhiriki matokeo iliyoleta nyumbani yalikuwa hayamfurahishi Rais Mwinyi [Kama Baba Mwenye Nyumba-Tanzania] kwa kipindi hicho kama Rais wa Tanzania.Katika kuonyesha hisia yake hiyo akajikuta anatumia misemo ya WAHENGA wake [WAZEE WALIOTANGULIA KUASISI KAURI HIZO] kuwa Tanzania ni kama kichwa cha mwendawazimu ambae kila anaetaka kujifunza basi wake mkasi atanyoa kadri jiko lake litakavyoona.
Wakati kauli hii inatoka nilikuwa kinda sana...1993...na leo ni Baba wa Watoto kauli hii imeendelea kuwa MWIBA wa UKWELI wa maisha yetu Watanzania katika mpira wa soka.
Binafsi nimeshawishika kujiunga na baadhi ya Watanzania kushauri yafuatayo, na kuwaomba wafuatao;
1: RAIS MSTAAFU MWINYI NA MARAIS WENZIE;
Kujiandaa kuwapokea Taifa Star wa leo pale atakapofuatwa na Watanzania kwa ajili ya ushriki wake katika kuufanya moyo wake kama ilivyo miyo ya Watanzani wengi wanavyokwaza na matokeo ya Taifa Star, kukubali KWA UMOJA wetu tubadilishe AKILI YETU na kuanza kuwa na MIOYO YA KUIONA SI KICHWA CHA MWENDAWAZIMU bali MKUKI WA MASAI WA KITANZANIA KUKABLIANA NA SIMBA YOYOTE YULE.
Kwa kauli mpya maalumu kinywani mwa Rais huyo Mstaafu kuomba akiwa na Wazee, Viongozi wa Kidini, Na Wanamichezo wa Tanzania pamoja na Wapenzi wa Michezo Tanzania kauri itakayomtoka iwe ''TAIFA STAR NI MKUKI WA WATANZANIA KUWASHINDA WASHINDANI WETU WOTE KWENYE MCHEZO HUO''.Tamko ilo liendane na ishara za vitendo katika tukio [Event] maalumu kuwakabidhi wachezaji walioko katika tukio hilo kila mmoja MKUKI WAKE huku wao wakimkabidhi MIKASI ambayo atashirki kuichoma MOTO ishara ya kuonyesha UMIKASI tuliokuwa tunanyolewa nayo umekwisha sasa tutakuwa washambuliaji kwa ASILI YA KIMASAI kumkabili mnyama yoyote.
2: CHAMA CHA SOKA [TFF] NA SHRIKISHO LA MICHEZO TANZANIA [BMT]
Kuanda tukio [Event] maalumu litakalo tumika kama tukio ka kihistorai maalumu kwa ajili ya Mzee Mwinyi kushiriki katika tukio hilo kufanya ishara maalumu ya ufutaji wa Kauri hiyo CHUNGU kwa Watanzania wote wapendao soka la Tanzania.
TFF na BMT kwa umoja wao waandae Tamasha ilo maalumu litakalo ratibiwa nao katika moja ya siku za mwisho wa jumaa yani Jumamosi [Saturday] kwa kuanda Tamasha ya Mechi ya Kirafiki Kusindikiza tukio hilo Maalumu ambalo Mzee Mwinyi atalifanya Kabla Ya Mechi husika ya kirafiki Katika Uwanja Mpya wa Taifa.Mzee Mwinyi akiongozwa na Rais Jakaya Kikwete, Mzee Mkapa, Wazee wapige dua la Asili, Viongozi wa Dini zote nao Wapige Dua zao kwa ajili ya kuomba Baraka za Ushindi ili iwe ni tangulizo la kiimani kila mara timu zetu hasa Taifa Star zinaposhrikia michezo n mataifa mengine.
Mechi hiyo ya Kirafiki ni Timu ya Taifa Star Wadogo Kwa Wakubwa Wakike na Kiume zote kufanywa Mseto mmoja na kisha Kugawanywa mara mbili kisha kushindana zenyewe.Mechi hii ikawe chachu ya ushindi daima.Refa wa mechi hizo wanaweza kuwa ni viongozi wa kidini toka kwenye mseto wa imani.
3:VIONGOZI WA KIDINI
Ushriki wa wazee wa dini zenye kutambulika Kwenye shughuri za Kitaifa, nia ni kuongoza maombi na Ibada kiimani katika kuibadilisha mioyo na akili zetu [Mindset] Watanzania ambazo kipindi cha Rais Mstaafu Ally Hasaan Mwinyi alikuwa na dhamana zetu Watanzania hivyo siku hiyo akiwa na Viongozi hao wakidini, Wazee Wa Jadina Marais wenzake watakuwa na mawazo mapya ya kiimani juu ya timu zetu za TAIFA ngazi zote.Na kwa niaba ya Watanzania wapokee dua toka kwa viongzoi wa Kidini katika kufunga mlango wa kuwa kichwa cha mwendawazimu na kufunguwa ukulasa mpya wa kuwa na mlango mpya wa kukabidhi MKUKI kama ishara ya siraha ya Ushindi Kitaifa.
4: WAZEE WA KIJADI [MACHIFU NA WAZEE WA KIMILA].
Ushiriki wao nao ni muhimu kwa kuwa nao ni sehemu ya jamii, kupitia dua zao za kijadi wanafungua milango ya wahenga wao kusimama mbele na nyuma ya Watanzania kila inapo itwa siku ya mechi zetu na mataifa mengine katika mashindano yoyote yale na kokote pale Duniani.
5: WANAMICHEZO NA WAFADHILI WA MICHEZO
Ushriki wa Wanamichezo na Wafadhili mbalimbali wa michezo kuwa sehemu ya tukio hilo kwa kuwa michezo na ufadhili ni MOYO mmoja katika kuleta ushindi wa Timu ya Mchezo wowote ule.Katika tukio hilo sio Mbaya Mara baada ya Mzee Mwinyi kutoa Mikuki kwa Wachezaji wa timu ya Soka siku ya tukio. Tukio hilo pia liendane na kuwepo na Mwakilishi kwa mmoja mmoja wa timu zinazocheza au shiriki michezo ya Kimataifa kutoka na Ligi Kuu [VPL].Pia kuwe na mwakilishi mmoja mmoja wa michezo mbalimbali tunayoshiriki Kimataifa kama Riadhaa, Ngumi, Mchezo wa Kikapu, Mpira wa Pete, na mingineyo yoyote yenye kuweza kuwapa vijana wa Tanzania ajira.
6: WATANZANIA
Hawa ndio washriki wakuu wa Tamasha la kufuta MINDSET zao, hawa ndio walengwa wa kusudio la kuwajenga KIROHO [SPIRITUALLY] kujiona kila timu yao inapoingia kwenye mashindano ya kimataifa basi wao TIMU yao NI WASHINDI DAIMA.Tamasaha hili lifanyike uwanja wa TAIFA MPYA na kiingilio bure cha Msingi wapatikane WAFADHILI kulifanya liwe na mvuto wa ina yake na kuweka kumbukumbu ya UTAIFA kuwa ile kauli NZITO YA UWENDAWAZIMU IMEKWISHA ZIKWA...LASMI KWA TAIFA.Na vijana wa kizazi kipya ambao kauri hii hawakupata kuiskia wakati inatolewa bali, wameiskia kama nukuu..Basi ni muda lasmi wapate NUKUU lasmi ya KITAIFA na kila TAIFA linaposhirki basi WATANZANIA wote kwa ujumla Watamke kama tumaini la USHINDI na ata ITOKEAPO tukafungwa tuone tuna nafasi ya kulekebisha makosa.
7: VYOMBO VYA HABARI;
Ushriki wa vyombo vya habari ni kuhakikisha mtizamo wa Taifa kuhusu Timu zetu za Taifa zinatoka kuwa Kichwa cha Mwendawazimu.Hapa ni Uzarendo...Ni sehemu ambayo Kila chombo cha habari kitumike katika kuhamasisha kauri mbinu ya kuweka hamasa kwa Watanzania kuondokana na ushriki wao katika hukumu ya kujiona wao ni kichwa cha mwendawazimu.Ka biidii ya dhati ya vyombo vya habari Taifa linatoka katika kujiona wanyonge wa Mashindano ya Kimataifa na Kuwa ni Washindi wa Michezo hiyo Kimataifa.Kwa wale wenye imani ya Kikirstu kuna misemo kama ''ALIWAZALO MJINGA NDIO LIMTOKEALO''.Hatuna budi sasa kwa nyakati hizi AKILI zetu Watanznaia ziendane na kuwaza mambo chanya [positive] na si has [Negative].
Tufike sehemu kama Taifa tujitanabaishe kwa ujumla wetu,mioyo ya kushindwa isiwe ni mawazo ya KITAIFA.Mashindano ya Kimataifa yatuunganishe kuwa washindi kabla ya kuingia Uwanjani.
8: MALINZI FAMILY:
Na hakika kwa wenye ufahamu familia hii, hamko kwenye soka au sekta ya michezo ka bahati mbaya.Wamejitanabaisha kama familia ya Wanamichezo.Mdogo wa Malinzi Senior Dionis ni Jamal Malinzi ambae ni Rais wa TFF ambao ndio wenye HATI MILKI ya lugha ya kichwa cha mwendawazimu, lakin pia Malinzi Senior Dions Malinzi yeye ni Kiongozi wa Baraza la Michezo Tanzania kwa awamu ya pili sasa.Kwa umoja wao wakiiunga nguvu zao na kuandaa Tamasha la kuondoa IMANI YA KICHWA CHA MWENDAWAZIMU kwenda MKUKI WA USHINDI WA WATANZANIA.Kwa kushrikiana kwao wanaweza kuasisi mabadiliko rohos [Spirt] ya jinsi Watanzania tunavyopokea timu zetu tunavyoshriki michezo kimataifa.Inaanza na kutamka kwa mdomo kisha uumbaji unafuata.Mungu alisema naiwe Mchana kukawa na nuru na kuwe na giza ikawa Usiku.
Jukumu hili la family hiyo iliyoko kwenye uongozi wa michezo ni kuongoza kutuandaa akili zetu Watanzania kuanza kufikilia kwa mtizamo chanya [Positive Perceptions].
Jisomee barua hiyo, nimeichukua kama ilivyo Toka
kwa Maulid Kitenge
"BARUA YA WAZI KWA ALLY HASAN MWINYI.
====================================
AWALI YA YOTE KWANZA KABISA NAPENDA KUKUPA HESHIMA YAKO MZEE WANGU ,
RAIS WANGU MSTAAFU ALHAJ ALLY HASAN MWINYI SHIKAMOO MZEE.
NIA NA DHUMUNI YA BARUA HII NI KUKUTAKA WEWE UKIWA KAMA MZEE WETU
KUTENGUA KAULI YAKO ILEEE ULIYOSEMA TANZANIA NI KICHWA CHA MWENDAWAZIMU.
KUMBUKA MZEE WANGU MANENO YA MTU MZIMA YAKITOKA HUWA HAYARUDI MATUPU .
VIJANA WAKO TUNATAABIKA NA KAULI YAKO KWA MAANA MPAKA LEO INATUTAFUNA.
ALHAJI MWINYI TUNAKUOMBA KWA MOYO MKUNJUFU
TENGUA KAULI YAKO YA KUWA TANZANIA NI KICHWA CHA MWENDAWAZIMU
ILI KULINUSURU TAIFA KATIKA MASWALA YA MICHEZO HUSUSANI MPIRA WA MIGUU.
MZEE WETU HIVI SASA TUPO KATIKA HALI MBAYA KULIKO VILE
KABLA HUJATOA KAULI YAKO KWA MAANA HAPO MWANZO TULIKUWA
TUNAJIKONGOJA YANI UAFADHALI ULIKUWEPO.
ZAMANI TIMU ILIKUWA HAINA MAANDALIZI MAZURI KAMBI ILIKUWA INAWEKA JESHI LA WOKOVU ,
WACHEZAJI WANAENDA MAZOEZINI NA DALADALA HUKU POSHO KUKIWA HAKUNA
ILA WALIPIGANA NA KUILETEA NCHI HESHIMA.
MHESHIMIWA TANGU UTOE KAULI YAKO ILE TAIFA STARS IMEKUWA KWELI KICHWA CHA MWENDAWAZIMU.
HAKUNA WA KUINUSURU TAIFA STARS ZAIDI YAKO WEWE ALHAJ ALLY HASANI MWINYI.
ONA LEO HII TUNAFUNGWA NA NCHI AMBAYO MFALME WAKE HANA
ANACHOWAZA ZAIDI YA KUOA VIGORI KILA MSIMU UFIKAPO.
MZEE WETU TUNAKUOMBA TENA NA TENA YANI TUPO CHINI YA MIGUU YAKO
TENGUA KAULI YAKO ILI KUINUSURU STARS YETU.
SINA MENGI ZAIDI MZEE WANGU ILA NATUMAI UJUMBE WANGU UTAKUFIKIA NA UTAUFANYIA KAZI.
WAKO KATIKA UJENZI WA TAIFA."
***** wako mimi ******