Tuishie kwenye kuandika hukumu kwa lugha adhimu ya Kiswahili au twende mbali zaidi?

Tuishie kwenye kuandika hukumu kwa lugha adhimu ya Kiswahili au twende mbali zaidi?

Elius W Ndabila

JF-Expert Member
Joined
Jul 17, 2019
Posts
324
Reaction score
649
TUISHIE TU KWENYE KUANDIKA HUKUMU AU TWENDE MBALI ZAIDI?

Na Elius Ndabila
0768239284

Jana Mh Rais alimpongeza Jaji wa Mahakama kanda ya Msoma ambaye aliandika hukumu kwa lugha ya Kiswahili. Mh Rais hakuishia kumpongeza tu, bali jana hiyo hiyo alimteua kuwa Mhe Zepharine Nyalugenda Galeba kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani. Mteule huyo ameapishwa leo Ikulu ya Chamwino Jijini Dodoma.

Wakati akiapishwa, pamoja na mambo mengine Mhe Rais amemshauri Waziri wa Katiba Mhe Dkt Mwigulu Lameck Madelu Nchemba kuwa apeleke mswaada Bungeni ili Mahakama zianze kuandika hukumu kwa lugha ya kiswahili ambayo ni lugha rafiki kwa Watanzania na ni kuonyesha uasisi wa Baba wa Taifa ambaye aliysunganisha Makabila zaidi 121 kuongea lugha moja ya Kiswahili.

Ninampongeza Rais kwa ujasiri huo na moyo ambao amekuwa nao juu ya kukuza hii lugha adhimu ya kiswahili.

Lakini wakati Mhe Rais anashauri hilo, mimi nimeenda mbali kuwa kwa nini sasa tusione haja ikiwezekana hata sheria zinazotungwa na Bunge kuandikwa kwa kiswahili? Tumeona Wabunge wakifanya mijadala kwa lugha fasaha ya kiswahili, lakini linapokuja swala la kuandika sheria zinaandikwa kwa Kingereza na wakati mwingine Sheria zinapoanza kutumika Wabunge nao wanakuwa wanazishangaa!

Mshangao huu wakati mwingine mtaani tunatafsiri kuwa labda wabunge baada ya kutunga sheria wanaoenda kuandika tena kwa lugha za kiingereza wanabadilisha? Ninakumbuka wakati sheria ya Kikokotoo inataka kuanza kutumika Wabunge wengi tukiwauliza hii sheria inasemaje nao walikuwa hawaelewi. Leo tukiwauliza hili la bodi ya mikopo likoje kutoka asilimia 8 hadi 15 wengi wao hawajui.

Sasa kwa nini sheria za bunge nazo zisiandikwe kwa lugha ya kiswahili kutoka kwenye muswada ili wabunge waweze kuwa na uelewa wa pamoja?

Ninadhani hili halitasubiri kauli ya Mh Rais, bali wabunge wetu tuliowaamini wanaweza kutusaidia kulitafuna.
 
Mimi naona tatizo letu la msingi sio lugha bali ni namna tunavyofikiri na tunavyo Fanya.

Ubora wa hukumu haujalishi lugha, hataikiandikwa kwa kabila la jaji inategemea tu kaandika nini.
 
Sheria kuandikwa kwa lugha ya kiswahili sio mwarobaini wa kupatikana kwa haki na watu kuelewa hizo sheria kama msingi wa sheria ni ukandamizaji zitabaki kuwa hivyo hivyo hata kama tukiandika kwa lugha zetu za makabila.
Kweli ndugu, sheria sio lugha, kwamafano sheria inayokataza matokeo ya urais kupingwa mahakamani hata iandikwe Kilatini, Kireno, Kipare, Kisukuma nk, bado itabaki kuwa kama ilivyo.
 
Kweli ndugu, sheria sio lugha, kwamafano sheria inayokataza matokeo ya urais kupingwa mahakamani hata iandikwe kilatini, kireno, kipare,kisukuma nk, bado itabaki kuwa kama ilivyo.
... of course. Kinachokosekana kwenye sheria za nchi hii sio "lugha" bali enforce ya hizo sheria ili iweze ku-apply kwa usawa makundi na nyanja zote bila ubaguzi.

Hata zijapoandikwa kwa lugha za mbinguni; kama hazitoi haki sawa kwa wote ni sawa na shaba iliayo; hazifai kitu. Hata zijapoandikwa kwa lugha za malaika, au za majini, au za kuzimu, au za makabila, au lugha yoyote iwayo; kama zina upendeleo ni sawa na upatu uvumao; tena ni ubatili!
 
Si hilo tu tumkumbushe mh. Rais juu ya suala la kutumia lugha ya kiswahili kama lugha ya kufundishia hadi chuo kikuu. Kwa maoni yangu lugha ni moja ya sababu kubwa ya kudumaa kwa elimu yetu.

Juzi tu nilikuwa namhoji kijana wa kidatu cha nne ambaye hakufanya vizuri mtihani wa kumaliza wa kidatu cha tatu. Huyu kijana alifanya vizuri mtihani wa kumaliza kidatu cha pili lakini mambo yakawa tofauti ilipofika kidatu cha tatu.

Kijana alijibu kwa uwazi kabisa kuwa sababu ilikuwa ni lugha. Kwa baadhi ya maswali hakuyaelewa kwa hiyo hakuyajibu na yale aliyoyaelewa hakuweza kujieleza kwani tafauti na aliopofanya mtihani wa kidatu cha pili ambao ulikuwa na multiple choice nyingi huu ulikuwa na maswali ya kujieleza.

Nina hakika yaliyompata kijana huyu yangewapata wengi kama wangefanya mtihani huo. Lugha ya Kingereza ina umuhimu wake hasa katika mazingira ya sasa ya science na teknologia. Lakini hilo linawezekana kwa kuifanya lugha ya KIingereza kuwa somo la lazima kwa shule zote na kuajiri walimu wazuri wa lugha kwa ngazi zote lakini watoto wetu wafundishwe maarifa kwa lugha yao mama.
 
Kuandika kwa kiswahili kwa sababu wananchi hawaelewi kiingereza au ni kwa sababu ya kukienzi!

Hukumu zimekuwa zikiandikwa kwa kiingereza kwa sababu gani? Ni kukienzi au ni nini?

Hukumu katika jumuia ya madola hurejelewa popote pale majaji wanapotaka kutoa uamuzi.

Je, ikiwa zitatolewa kwa lugha zote mbili haiwezekani?

Tutafanya makosa ikiwa uamuzi huu unatokana tatizo la kutokujua Kiingereza.
 
Sheria kuandikwa kwa lugha ya kiswahili sio mwarobaini wa kupatikana kwa haki na watu kuelewa hizo sheria kama msingi wa sheria ni ukandamizaji zitabaki kuwa hivyo hivyo hata kama tukiandika kwa lugha zetu za makabila.
Nchi hii ni ya ajabu kweli, leo nimemsikia msomi kabisa eti anasema endapo sheria zitaandikwa kwa kiswa, hata watu kufanya makosa itapungua sana kwani watakuwa wakijua kuwa akifanya hivi ataadhibiwa vilee! Hahaaaa!!iyaani wanataka kuwaaminisha watu kuwa hukumu ikiandikwa kisw, ndio mwisho wa kutumia mawakili, eti mtu utaisoma tu na kuielewa na kuikatia rufaa?!!YAANI UKISHINDWA KUWAONGOZA WATANZANIA, HATA MARAIKA WATAKUSHINDA!
 
Vitivo vya sheria chuo kikuu navyo viangalie kufundisha masomo ya sheria kwa kiswahili. Itasaidia kupanua tafsiri.
 
Ukisikia kuingizwa chaka ndio huku one man show ndiyo hii
Kilajambo kubwa huwa na sera hivi hili hata kwenye kile kitabu chenye kurasa miatatu na ushee(ilani ccm) lipo uk upi? Katiba inasemaje au imebadili kipengele kinacho elekeza

Tisikurupuke
 
Nchi zote za jumuiya ya madola zilikubaliana ziweke rekodi za hukumu kwa lugha ya Kiingereza as a lingua Franca ili mataifa mengine yaweze kutumia baadhi ya hukumu Kama reference kufikia judgement.

Sasa ikatungwa sheria kwamba lugha ya mahakama itakua ni aidha kiswahili au kiingereza lakini rekodi itawekwa kwa kiingereza as a lingua Franca.

Sasa assume Nigeria wakaandika kihausa, sisi tukaandika kiswahili, wakongo wakaandika kifaransa na kadhalika nakadhalika huoni Kama itawajia vigumu wanasheria kwenye ishu ya kurefer previously cases kufikia judgement?

Tufikiri tuache ushabiki maandazi
 
Back
Top Bottom