Tujadili mapungufu ya Sera yetu ya Viwanda. Unadhani ina mapungufu gani?

Tujadili mapungufu ya Sera yetu ya Viwanda. Unadhani ina mapungufu gani?

Tanzania kwa mtazamo uliopo sasa wa viongozi na taasisi kama TRA, OSHA, Halmashauri za miji, NEMC, n.k;kamwe haiwezi kuwa nchi ya uchumi wa viwanda.

Usitegemee kama kutakuwa na mwekezaji mjinga ambaye ataenda kuwekeza mahali ambapo kila siku sheria na kodi zinabadilika.

Unaomba kibali, kodi tofauti, unaanza kujenga kodi imebadilika, unaagiza mitambo kodi imebadilika, unaanza uzalishaji kodi imebadilika. Bado matamko ya maDC na maRC ambao hawajawahi kujenga hata genge lakini wanataka wakuamrishe namna ya kuendesha kiwanda.

Mahali ambapo sheria na kodi hubadilika kila mara, huchochea uchuuzi na siyo ujenzi wa viwanda. Hakuna atakayeenda kujenga kiwanda mahali ambapo hujui kesho sheria itakuwaje, kodi itakuwaje, Rais atasemaje, RC na DC watasemaje, OSHA na NEMC watasemaje!!

Mataifa kama Uingereza, sheria yao ya uwekezaji, haijawahi kubadilika tangu miaka ya 1950. Siyo wajinga kufanya hivyo.

Faida inayotokana na kiwanda huchukua miaka mingi mpaka kuanza kupatikana. Kabla hujaanza yakubidi ufanye projections zako. Kwa Tanzania haiwezekani. Utafanyaje projections wakati kila siku kodi na sheria zinabadilika?

Kwa nchi ya namna hii, unafanya tu biashara ya kuagiza vitu toka China, Thailand, India, Uturuki, n.k. Ukiona sheria na kodi zimepanda, unaacha. Sasa kama umejenga kiwanda, utafanyaje?

Kwa mazingira ya Tanzania yaliyopo sasa, sahau, sahau, sahau kabisa, ujenzi wa viwanda. Vitakuwa vinajengwa vidudu fulani, vinavyofanana na viwanda lakini siyo viwanda.

VAT for wholesellers and retailers kwa Ghana ni 3%, Tanzania ni 18%. Ghana kuna wakati uchumi wake ulikuwa unakua kwa kiwango cha 12%. Rais wao ni mchumi, na mwenye uelewa mzuri wa uchumi wa Dunia.

Note: HAKUNA NCHI YOYOTE DUNIANI ILIYOKUWA MASKINI AMBAYO IMEWAHI KUPATA MAENDELEO KWA KUONGEZA KODI, ISIPOKUWA KWA KUPUNGUZA SANA VIWANGO VYA KODI NA KUONDOA KODI NYINGI.

Adui mkubwa wa maendeleo ya uwekezaji ni uwingi wa kodi na kodi kubwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo serikali ina-focus sana kuwawekea mazingira mazuri ya uwekezaji wafanyabiashara wenye mitaji mikubwa. Ukiacha watu wanaolalamika kwa niaba yao huku mitandaoni kisiasa zaidi kuliko uhalisia, jamaa huko juu mazingira yao yapo vizuri.

Tatizo ni wafanyabiashara wadogo ndio wenye mazingira magumu sana sitoshangaa kuona stats za biashara kukuwa Tanzania ni ndogo sana.

It’s OK kutaka mfanyabiashara mwenye turnover ya 4 million kwa mwaka kuwa na TIN number kama TRA inavyomlazimisha ila kumdai kodi ni wazimu.

Juzi nilikuwa namsikia mkurugenzi wa elimu ya kodi kutoka TRA akiwa ITV eti mtu mwenye mauzo ya tsh 10000 kwa siku anatakiwa kujisajili kulipa kodi, are these ppl serious?

Mtu mwenye mauzo ya elfu kumi kwa siku gross profit yake akitoa na expenses kwenye hiyo hela labda faida yake elfu tatu mpaka sita kwa siku.

Kwa mwezi biashara hizo zinatengeneza kati ya elfu 90 mpaka laki moja elfu 80 halafu huyu unataka alipe kodi. Wakati kima cha chini cha mshahara kwenye ajira ambacho hakina PAYE ni 270K.

Ideal unataka watu wajiajiri, wakue kibiashara na kutengeneza ajira, ili kufanya ivyo unataka mfanyabiashara mdogo apate nafuu kuliko mwajiriwa mwenye kipato kidogo.

Kwetu ni vice versa kuna more incentive ya kuajiriwa kuliko kwa mfanyabiashara mdogo si unatuma salamu mbaya.

Udhani kama ni watu wenye serious agenda ya kukuza biashara ndogo ndogo zaidi ya maneno ya siasa.

Matendo yao ayashawishi watu wafungue biashara. Wanaofanya ivyo sio kwa sababu ya incentives, isipokuwa hawana namna nyingine ya kupata mkate lakini ukweli ni kwamba mazingira ya wafanyabiashara wadogo wadogo wengi sio rafiki kabisa.
 
Mkuu, hawa makamanda walioko humu ndo unataka mjadili nao sera ya viwanda? Uwezo wa kujadili sera wameutoa wapi? Wajadili sera halafu matusi atukane nani? Hawa ni watu wa porojo tu na mtusi tu!
Kwa hiyo jf waliopo wote ni makamanda? Wale buku 7 nao ni makamanda?
 
Habari za leo wakuu,

Uzii huu utakuwa maalum kuijadili sera yetu ya viwanda.

Bila kutukana wala kumnyoshea mtu yeyote kidole, naomba kila mmoja atoe maoni yake.

Mada: Wewe unahisi sera yetu ya viwanda ina mapungufu gani?

Zingatia ili taifa letu liweze kuendelea linahitaji kuwa na sera bora ya viwanda. Sera bora ya viwanda inatakiwa kutoa dira ya maendeleo ya uchumi wa taifa.

Zingatia muda mwingine sera inaweza kuchukua mda mrefu kuleta matokeo chanya.

Sote tumeona jitihada zinazo fanywa na serikali yetu ya awamu ya tano na sita katika kutoa motisha kwa watanzania kujenga na kuanzisha viwanda.

Lakini pia tumeona jinsi ambavyo serikali imetumia jitihada kufufua taasisi za umma. Serikali imefufua ATCL, TTCL, n. k.

Zingatia mfumo wowote wa biashara ya kiuchumi hauwezi kufanya kazi vizuri bila serikali kuingilia. Hivyo ni lazima serikali nayo iingie kwenye mfumo huo ili kazi iende vizuri. Ndio sababu mnaona kwenye usafiri wa anga mnaiona serikali kupitia ATCL, kwenye mawasiliano mnaiona serikali kupitia TTCL, n.k.

Serikali ikiwa karibu na mfumo wa kiuchumi ni rahisi kupata taarifa zinazo husu mzunguko mzima wa kiuchumi, kasoro na matatizo mbalimbali. Mimi nadhani pia kuiachia sekta binafsi iendeshe mfumo mzima wa uchumi peke yake sio vizuri na swala hili lina athari kiuchumi.

Nikija kwenye swala la mchakato mzima wa sera yetu ya viwanda. Sera yetu ni nzuri sana na itatuletea faida nyingi sana huko mbeleni. Ila nilikua napenda ili sera yetu ifanikiwe asilimia 100 hasa kwenye swala la ujenzi wa viwanda, nadhani ingechagua baadhi ya viwanda vile ambavyo tunaona tunaweza kuviendesha vizuri na vikatatuletea faida nyingi kama vile utoaji wa ajira nyingi, mapato mengi na bidhaa nyingi.

Nilikua nasoma jarida moja jinsi ambavyo china wanapigana kukuza uchumi wao, wao katika sera yao ya viwanda wamechagua utengenezaji wa magari ya umeme. Hivyo nguvu yao yote wameilekeza kwenye uwekezaji wa viwanda vya magari ya umeme, utafiti na ubunifu katika viwanda vya magari ya umeme.

Naomba niishie hapa.

Hivyo ndugu yangu kama una maoni dondosha maoni yako

Usitukane.
Kwanza Tz kuna sera ya viwanda?
 
Chuma ndiyo msingi wa viwanda. Kama hatuzalishi chuma tusahau kuwa nchi ya viwanda. Kama huzalishi chuma hata kiwanda cha pini na sindano huwezi kuwa nacho.
 
Chuma ndiyo msingi wa viwanda. Kama hatuzalishi chuma tusahau kuwa nchi ya viwanda. Kama huzalishi chuma hata kiwanda cha pini na sindano huwezi kuwa nacho.
okay, kwa hivyo wewe una maoni gani juu ya hili
 
Tuna viwanda 100 kila mkoa! Tuko vizuri au Uongo ndugu zangu?
 
Habari za leo wakuu,

Uzii huu utakuwa maalum kuijadili sera yetu ya viwanda.

Bila kutukana wala kumnyoshea mtu yeyote kidole, naomba kila mmoja atoe maoni yake.

Mada: Wewe unahisi sera yetu ya viwanda ina mapungufu gani?

Zingatia ili taifa letu liweze kuendelea linahitaji kuwa na sera bora ya viwanda. Sera bora ya viwanda inatakiwa kutoa dira ya maendeleo ya uchumi wa taifa.

Zingatia muda mwingine sera inaweza kuchukua mda mrefu kuleta matokeo chanya.

Sote tumeona jitihada zinazo fanywa na serikali yetu ya awamu ya tano na sita katika kutoa motisha kwa watanzania kujenga na kuanzisha viwanda.

Lakini pia tumeona jinsi ambavyo serikali imetumia jitihada kufufua taasisi za umma. Serikali imefufua ATCL, TTCL, n. k.

Zingatia mfumo wowote wa biashara ya kiuchumi hauwezi kufanya kazi vizuri bila serikali kuingilia. Hivyo ni lazima serikali nayo iingie kwenye mfumo huo ili kazi iende vizuri. Ndio sababu mnaona kwenye usafiri wa anga mnaiona serikali kupitia ATCL, kwenye mawasiliano mnaiona serikali kupitia TTCL, n.k.

Serikali ikiwa karibu na mfumo wa kiuchumi ni rahisi kupata taarifa zinazo husu mzunguko mzima wa kiuchumi, kasoro na matatizo mbalimbali. Mimi nadhani pia kuiachia sekta binafsi iendeshe mfumo mzima wa uchumi peke yake sio vizuri na swala hili lina athari kiuchumi.

Nikija kwenye swala la mchakato mzima wa sera yetu ya viwanda. Sera yetu ni nzuri sana na itatuletea faida nyingi sana huko mbeleni. Ila nilikua napenda ili sera yetu ifanikiwe asilimia 100 hasa kwenye swala la ujenzi wa viwanda, nadhani ingechagua baadhi ya viwanda vile ambavyo tunaona tunaweza kuviendesha vizuri na vikatatuletea faida nyingi kama vile utoaji wa ajira nyingi, mapato mengi na bidhaa nyingi.

Nilikua nasoma jarida moja jinsi ambavyo china wanapigana kukuza uchumi wao, wao katika sera yao ya viwanda wamechagua utengenezaji wa magari ya umeme. Hivyo nguvu yao yote wameilekeza kwenye uwekezaji wa viwanda vya magari ya umeme, utafiti na ubunifu katika viwanda vya magari ya umeme.

Naomba niishie hapa.

Hivyo ndugu yangu kama una maoni dondosha maoni yako

Usitukane.
Umeandika kwa Mapenzi mazuri ya kizalendo. Lakini wazalendo Ni watu wakweli sana.

Sera hii ingefaa kuanza kwa kuzingatia msingi kwanza.

Wataalamu wachache waliopo wangefufua viwanda vilivyopo Kisha Sera ingeanza na elimu ya juu kwa kutangaza vipaumbele na idadi gani ya wasomi inahitajika kimkakati ili kuchochea utekelezaji wa Sera hiyo miaka ijayo.
Hivyo vipaumbele vya mikopo ya elimu ya juu kuhusiana Kozi za masuala ya viwanda vyuo vikuu vingezingatiwa.
Zaidi kungekuwa na udhibiti wa uhakika wa ajira wakati wa utekelezaji na sio kuajiri wageni kwa wingi.
 
Tutatue kwanza kero ya umeme, maji ndo tujadili kuhusu viwanda vinginevyo tunapotezeana muda tu.
Mm hata sera yenyewe ya viwanda sijaiona na kusoma kwanza Naona kapoteza muda tu hata mawaziri wenyewe wa viwanda sijui kazi zao.Wacha nipite.
 
Back
Top Bottom