Tujadili na kuchambua Sheria za kodi; VAT na Income Tax

Tujadili na kuchambua Sheria za kodi; VAT na Income Tax

Malyenge

JF-Expert Member
Joined
Jan 16, 2012
Posts
6,658
Reaction score
3,659
Wakuu leo tujadili na kuchambua sheria za kodi tajwa hapo juu. Tutafute ni wapi sheria zina utata ili tuzichangie kwa kutolea ufafanuzi (interpretation) na jinsi inavyotakiwa kuwa.
Mfano kifungu fulani kinaposema jambo fulani tujadili utata wake na ufafanuzi wa utata huo (kutafsiri uhalisia na maana ya sheria inavyomaanisha ama kutaka iwe).
Karibuni sana.........'
 
Good topic mr
Mie concern yangu kubwa ni kwa hizi allowance ambazo wanapeana kwa minajili ya kua non taxed,kama allowance za wabunge au sis offc.
Kuchukua allowance na kuja kurefund back claims

Tuziangalie hiz sheria vema na makundi ambayo tanapaswa kunufaika na hili na sio wenye nacho zaid ya wasio nacho
 
Good topic mr
Mie concern yangu kubwa ni kwa hizi allowance ambazo wanapeana kwa minajili ya kua non taxed,kama allowance za wabunge au sis offc.
Kuchukua allowance na kuja kurefund back claims

Tuziangalie hiz sheria vema na makundi ambayo tanapaswa kunufaika na hili na sio wenye nacho zaid ya wasio nacho

Allowance hizi zinatozwa kodi na sheria ya kodi ya mapato kifungu cha 7(2)(a). Kifungu hiki ndio msingi wa kutoza kodi allowances. Kifungu 7(3) kimezitaja allowance na marupurupu mengine yaliyopo kifungu cha 7(2)(a) kama yakiwa kwenye mazingira fulani basi yasamehewe kodi.
Mfano allowance unayopewa kwa ajili ya kwenda nje ya eneo lak la kazi kusimamia ili kazi za mwajiri wako zifanyike allowance hiyo haitozwi kodi. Na msingi huohuo uliopo katika kanuni ya 4(1) ya VAT General Regulation 1998 wajiriwa ama mteja akilipiwa malazi na chakula VAT ya manunuzi (input VAT) haikubaliki isipokuwa kama ni kwa sababu na nature ya kazi ama mazingira. Kwa hiyo mtumishi akilipiwa malazi wakilipiwa chakula kwa sababu yuko nje ya kiyuo chake cha kazi au yuko "site" basi kanuni hiyo huruhusu VAT ya manunuzi kudaiwa katika kifungu cha 16(4).


TURUDI KWENYE ALLOWANCES:
Kimsingi allowances zote kwa mujibu wa sheria ni lazima zitozwe kodi isipokuwa ni kwa sababu zilizotajwa kwenye sheria ya kodi ya mapato kifungu 7(3).


MISAMAHA YA KODI YA MAPATO
Waziri amepewa mamlaka ya kusamehe kodi yoyote hata kama haijatajwa kwenye jedwali la 2 la sheria ya kodi ya mapato lililoorodhesha vipato vilivosamehewa kodi.
Kodi iliyosamehewa ndio iko kwnye jedwali la pili la sheria ya kodi ya mapato ambapo item "S" ndipo tunakuta ile fedha ya mwisho kabla ya bunge halijavunjwa karibia na uchaguzi baada ya miaka mitano ya kulitumikia bunge IMESAMEHEWA.


WABUNGE WAMESAMEHEWA ALLOWANCE?
Kwa mujibu wa sheria ya kodi ya mapato ukiacha gratuity zao (malipo ya kiinua mgongo wakati bunge linavunjwa) hamna hata sehemu moja wabunge wamesamehewa allowance zao za kila mwezi zinazoambatana na mishahara yao.....hakuna kabisa hata aje professor hapa kifungu hicho hatakiona......!!!!!!Allowance zote zinatozwa kodi!!!!!!!


JE NI SAWA KWA ALLOWANCES KUTOTOZWA KODI WAKATI SHERIA HAIJASEMA?
Mimi sijui isipokuwa sheria ya kodi ya mapato kifungu cha 7 hakiruhusu ubaguzi......(discrimination).
Sasa kwa nini wenguine watozwe na wengine wasitozwe wakati wale wasiotozwa hawakusamehewa popote? Hilo ni suala la kisera na kiutawala zaidi. Tuwashauri kitaalamu ni kwa kiasi gani linaumiza.
 
Allowance hizi zinatozwa kodi na sheria ya kodi ya mapato kifungu cha 7(2)(a). Kifungu hiki ndio msingi wa kutoza kodi allowances. Kifungu 7(3) kimezitaja allowance na marupurupu mengine yaliyopo kifungu cha 7(2)(a) kama yakiwa kwenye mazingira fulani basi yasamehewe kodi.
Mfano allowance unayopewa kwa ajili ya kwenda nje ya eneo lak la kazi kusimamia ili kazi za mwajiri wako zifanyike allowance hiyo haitozwi kodi. Na msingi huohuo uliopo katika kanuni ya 4(1) ya VAT General Regulation 1998 wajiriwa ama mteja akilipiwa malazi na chakula VAT ya manunuzi (input VAT) haikubaliki isipokuwa kama ni kwa sababu na nature ya kazi ama mazingira. Kwa hiyo mtumishi akilipiwa malazi wakilipiwa chakula kwa sababu yuko nje ya kiyuo chake cha kazi au yuko "site" basi kanuni hiyo huruhusu VAT ya manunuzi kudaiwa katika kifungu cha 16(4).


TURUDI KWENYE ALLOWANCES:
Kimsingi allowances zote kwa mujibu wa sheria ni lazima zitozwe kodi isipokuwa ni kwa sababu zilizotajwa kwenye sheria ya kodi ya mapato kifungu 7(3).


MISAMAHA YA KODI YA MAPATO
Waziri amepewa mamlaka ya kusamehe kodi yoyote hata kama haijatajwa kwenye jedwali la 2 la sheria ya kodi ya mapato lililoorodhesha vipato vilivosamehewa kodi.
Kodi iliyosamehewa ndio iko kwnye jedwali la pili la sheria ya kodi ya mapato ambapo item "S" ndipo tunakuta ile fedha ya mwisho kabla ya bunge halijavunjwa karibia na uchaguzi baada ya miaka mitano ya kulitumikia bunge IMESAMEHEWA.


WABUNGE WAMESAMEHEWA ALLOWANCE?
Kwa mujibu wa sheria ya kodi ya mapato ukiacha gratuity zao (malipo ya kiinua mgongo wakati bunge linavunjwa) hamna hata sehemu moja wabunge wamesamehewa allowance zao za kila mwezi zinazoambatana na mishahara yao.....hakuna kabisa hata aje professor hapa kifungu hicho hatakiona......!!!!!!Allowance zote zinatozwa kodi!!!!!!!


JE NI SAWA KWA ALLOWANCES KUTOTOZWA KODI WAKATI SHERIA HAIJASEMA?
Mimi sijui isipokuwa sheria ya kodi ya mapato kifungu cha 7 hakiruhusu ubaguzi......(discrimination).
Sasa kwa nini wenguine watozwe na wengine wasitozwe wakati wale wasiotozwa hawakusamehewa popote? Hilo ni suala la kisera na kiutawala zaidi. Tuwashauri kitaalamu ni kwa kiasi gani linaumiza.

Mkuu kuna allowances ambazo wanalipwa watumishi wa serikali zimetajwa kwenye ITA hazitozwi kodi. Mfano acting allowance, per diem, extra duty, nk. Mwanzoni zilikuwa zikitozwa kodi lakini nadhani Finance Act, 2011 ama 2012 iliziondoa kwenye kodi. Usifanye generalization.
 
Mkuu kuna allowances ambazo wanalipwa watumishi wa serikali zimetajwa kwenye ITA hazitozwi kodi. Mfano acting allowance, per diem, extra duty, nk. Mwanzoni zilikuwa zikitozwa kodi lakini nadhani Finance Act, 2011 ama 2012 iliziondoa kwenye kodi. Usifanye generalization.

Yes ziliondolewa kodi kwa watumishi wa umma. Hoja yako nini hapa?
 
Yes ziliondolewa kodi kwa watumishi wa umma. Hoja yako nini hapa?
Kwani wewe hoja yako ilikuwa nini? Manake naona kama tuaelekea njia tofauti. Umesema hakuna sheria inayosema allowances zisikatwe kodi
 
Napata shida kuelewa Kifungu 72 (1) cha ITA. Naomba ufafanuzi.
 
Napata shida kuelewa Kifungu 72 (1) cha ITA. Naomba ufafanuzi.

Multinational corporations yaani makampuni makubwa ya nje yanayokuja kuwekeza hapa nchini kwa kawaida yakishapata faida yatairudisha faida hiyo kwao. Sasa kitendo cha kusafirisha faida kwao ndio kinaitwa repatriated income of a Permanent Establishmentkitendo tunachokiona katika kifungu cha 72(1) cha sheria ya kodi ya mapato ya mwaka 2004.
Kwa kawaida faida hiyo inakuwa tayari imeshatozwa kodi ya mapato yaani corporation tax kwa kiwango cha sailimia 30 (kama kiwango hicho tunavyokiona katika aya ya 3(1) katika jedwali la kwanza la sheria ya kodi ya mapato ya mwaka 2004).
Sasa katika urudishwaji wa faida kwao na kampuni iliyowekeza nchini napo inatakiwa ilipwe kodi ya urudishwaji faida kwao kama tunayoiona fomula ya namna ya kukokotoa kodi ya urudishwaji faida hiyo ili tuitoze kodi ya asilimia kumi (10%) tunayoiona katika jedwali la kwanza la sheria ya kodi ya mapato aya ya 3(2),
72(1) inaelezea fomula ya kukokotoa ili tuitoze kodi faida inayorudishwa kwao na kampuni iliyowekeza nchini kwetu.
Fomula inasema tunachukua A+B-C

Amabo A ni Thamani ya Asset za kampuni hiyo za mwanzo wa mwaka baada ya kuotoa depreciation allowance tuliyoikokotoa mwaka jana na kui allow kama tax deductive expenditute (tunayoiona kifungu cha 17 cha sheria ya kodi ya mapato ya mwaka 2004 na jedwali la tatu la sheria hiyo aya ya 3(1) ya jedwali hilo.

Ambapo B ni hiyo faida iliyokatwa kodi
Na C ni Thamani ya Asset baada ya kukokotoa depreciation allwance na kui allow mwaka huu.

Just ni fomula tu ya jinsi ya kupata hicho kiasi utakachokitoza kodi ya asilimia 10 kama kodi ya kusafirisha faida nje ya nchi.

Labda kikubwa wahasibu waliobobea wanachoshindwa kukielewa ni kwamba kampuni ya nje ilikuja kuwekeza hapa nchini inatakiwa kulipia kodi ya urudishwaji faida kwao hata kama mwaka huo haikurudisha faida nje ya nchi.....! Ikionekana tu kwamba ilipata faida basi lazima repatraeted income taxation ifanyike. Kumekuwa na madai ya kusema unanikataje kodi ya repatriation wakarti sijasafirisha faida kwetu? Jibu ni rahisi tu kwamba kama hujasafirisha leo basi ipo siku utaisafirisha kwa hiyo Mamlaka wacha ikate kodi yake kabisa ili siku utakapoisafirisha usiwe na madeni ama usilete kazi ya kupambanua ipi ni ipi.
 
Kwani wewe hoja yako ilikuwa nini? Manake naona kama tuaelekea njia tofauti. Umesema hakuna sheria inayosema allowances zisikatwe kodi

Mkuu nilikuwa namaanisha hao wabunge hakuna mahala walikuwa wamesamehewa kodi allowances zao. Walikuwa hawalipi si kwa sababu sheria imesema bali ni uamuzi wao tu........
 
Kuna mtaalamu mmoja wa Kodi alisema "Tax is not always proportionate rather is progressive" Naomba ufafanuzi mtaalamu huyo alikuwa ana maanisha nini?
 
Kuna mtaalamu mmoja wa Kodi alisema "Tax is not always proportionate rather is progressive" Naomba ufafanuzi mtaalamu huyo alikuwa ana maanisha nini?

Mkuu nyelesa umesoma vizuri thread? Tujadili sheria za kodi......................... na si theory za kodi. Hicho unachokisema ni theory za kodi na si sheria za kodi. Hilo swali wachumi wanalijua maana ni zile mojawapo ya principles of taxation ambazo ni theory na wala si sheri.
Wewe uliza vifungu na tafsiri yake utapewa majibu mazuri tu mkuu.....
 
Last edited by a moderator:
Nauliza tuu,. hivi waalimu na wanajeshi wanalipa kodi wakiagiza gari kupitia babdarini,..nataka nitafute namie kfaa chakutembelea ila kodi nweeh!.
 
Back
Top Bottom