Tujadili namna ya kutafuta pesa

Tujadili namna ya kutafuta pesa

De Professor

JF-Expert Member
Joined
May 21, 2021
Posts
237
Reaction score
505
Wanajamvi nataka niwasilishe hoja kibabe

Ni hivi kuna zile kauli ooh Mapenzi sio pesa, pawepo na upendo wa dhati basi, ooh ndani pawe na Amani na Upendo ndio kitu kikubwa nisawa.

Ila tu nikazie Hasa kwa Mwanaume pambana uwezavyo uwe na visenti ili mkitaka kwenda Coco kula miogo unato tu cent achane na Samaki Samaki kama sio uwezo wako, mkitaka kubadili mbonga na menu vinafanyika bila neno, sio chakula tu ndani hakuna, wengine hadi Dawa ya Meno ni tabu kuwepo ndani mwisho wa siku kale ka upendo kanayeyuka taratibu taratibu mwisho wa siku mnaishi kwa mazoea ndani.

Basi tufanye hivi huu uwe uzi endelevu mje tupeane namna ya kuzikusanya hizo zilizomfanya Manara kukalia kuti kavu Simba. Kijana, Baba, Mama na Dada mwenye haiba ya Upambanaji na mwenye kuhakikisha haukai pasipo kufanya kitu. Watu waliofanya vitu tofauti tofauti iwe ni Biashara au aina yeyote ya kitu kinachoweza kutengeneza Pesa kwa muda mfupi return ya kuanzia week 1. Ili basi aliye muajiliwa ila anaomtaji asisite kuwekeza na kuzingusha pesa. Aliye na Mtaji ila hajui afanye nini nayeye apate kitu cha kufanya na Asiekuwa na Mtaji ila anatamani kuja kufanya jambo walau ajue nini ataenda kufanya.

#1. Wazo langu la kwanza Biashara ya Mayai hasa ya kisasa ukipata sehemu yenye mzunguko mkubwa kama wauzaji wa chips na vibanda vingi wakaweka order zao ni rahisi wewe kuchukua mzigo na kupeleka sehemu husika ndani ya week 1 ukawa umeshapata return ya pesa yako.

Angalizo: Shughuli za uwekezaji kama Bitcoin,Forex, Alliance, Forever living na wengine wa Network Marketing usizilete sizipingi ila tu sio mahali pake hapa Asanteni.
 
Sijaelewa mkuu ishu ni ujasiriamali au kuhusu mapenz sio pesa
Jamaa ameamua kutumia jukwaa pendwa na kuwa mbunifu wa kupenyeza mada yake!

Point ni kwamba anahitaji kupewa tips za kupata hela kwa biashara zenye returns ya muda mfupi so anaomba mawazo yetu wengine ila kwa kuanza amefikiri kuhusu biashara ya mayai mtaani! Ina returns nzuri iwapo wauza chips wamekuzunguka eneo hilo!
 
Jamaa ameamua kutumia jukwaa pendwa na kuwa mbunifu wa kupenyeza mada yake!

Point ni kwamba anahitaji kupewa tips za kupata hela kwa biashara zenye returns ya muda mfupi so anaomba mawazo yetu wengine ila kwa kuanza amefikiri kuhusu biashara ya mayai mtaani! Ina returns nzuri iwapo wauza chips wamekuzunguka eneo hilo!
Hapo nmemuelewa sasa [emoji1787][emoji1787] kajiongeza
 
Huu uzi huwez kufika mbali..... Watu wanapenda sana ngono #ccm itawale milele
 
Betting ndio kila kitu


PSG win
Juve win
Liverpool win
Buyern win


Stake :1milion

Pay out :5.7 million

Kwa wiki hapo
 
Back
Top Bottom