Tujadili uhalisia wa kilimo biashara cha sasa na kilimo afya

Tujadili uhalisia wa kilimo biashara cha sasa na kilimo afya

Mamlaka ya chakula na sawa KAZI ni nini kufanya Biashara au kuregulate bidhaa za chakula zimeet standards za afya KWA mlaji?
Ni vema uwaulize wahusika. Hata sigara haukatazwi na serikali kuvuta, ila wanatoa onyo kuwa ni hatari kwa afya yako huku wakichukua kodi na kuhamasisha kulima tumbaku. Mtunza afya yako si serikali, ni wewe!
 
Mkuu Gwappo...

Ahsante kwa maada hii fikirishi. Maendeleo ya wagu, ongezeko la watu duniani yameleta haya tunayaita mapinduzi ya kilimo duniani. Hapo zamani katika maeneo yetu mengi idadi ya watu ilikuwa ni ndogo saana hivi kulima kwa asili ama kwa kutumia mbegu za asili kuliweza kusaidia katika kutosheleza mahitaji husika ya watu.

Tulikuwa na mbegu za asili ambazo huzalisha kidogo , hukabiliwa na magonjwa saana,hazistahimili ukame n.k.

Ongezeko la joto duniani , kukauka kwa vyanzo vya maji ukame na mengine mengine yamepelekea kuwa na tafiti zitakazo leta mbadala wa changamoto zote hizi na kusaidia kuongeza idadi ya uzalishaji na kuepukana na changamoto za usalama wa chakula duniani.

Hata hivyo kulima kibishara kwa maana ya chakula chenye afya inawezekana tuu ... changamoto ni kuwa mtu atazalisha kidogo kwa muda mrefu na kuleta hasara katika maana ya value ya muda.

N.B.
Kilimo cha kuangalia afya ndicho kilicho bora katika kuyapa maisha yetu maana . Lakini changamoto tuliyonayo katika maendeleo yetu hayatupi nafasi nzuri katika hili
Umechambua vizuri sana Tychob na kuonesha bayana changamoto zilizopo. Lakini fikiria kama kinyesi cha ng'ombe, kuku, nk.; tungekuwa tunakusanya na kukitumia mashambani, tusingehitaji mbolea za viwandani. Na tungepata kwa bei nafuu huku tukiwapa faida wafugaji nao wakikusanya kwa wingi ili wauze badala ya kutupa ovyo.

Mbolea ya mabaki ya mimea (mulching) nayo tunatupa au kuchoma moto badala ya kuozesha ili irudi shambani kurutubisha ardhi.

Tunapaswa kubadili mtazamo wa kufikiri kwetu (change of mindset). Tunavyoona ni duni ndivyo vilivyo bora. Mtu akila bamia, mlenda au mchicha kwa viazi vitamu anaonekana amekula chakula duni kuliko aliyenunua hamburger au nyama za kwenye makopo super market!

Tunanunua kwa bei kubwa vya kuharibu miili wakati vya bei ndogo ndivyo vyenye faida kubwa mwilini.
 
Ni vema uwaulize wahusika. Hata sigara haukatazwi na serikali kuvuta, ila wanatoa onyo kuwa ni hatari kwa afya yako huku wakichukua kodi na kuhamasisha kulima tumbaku. Mtunza afya yako si serikali, ni wewe!
KWA hiyo Ina maana tunayo mamlaka isiyojali afya ya mlaji ?
Mamlaka hiyo iliwekwa na kina sisi au wawakilishi wetu si ndiyo?
Wawakilishi wetu ndiyo sisi si ndiyo?


Kutokana na ongezeko Kubwa la watu ,tukiendelea kutumia njia za asili Tunaweza timiza mahitaji ya chakula KWA kutumia njia ulizozitaja hapo juu?

Mass production inawezekana KWA mfumo huo?
 
KWA hiyo Ina maana tunayo mamlaka isiyojali afya ya mlaji ?
Mamlaka hiyo iliwekwa na kina sisi au wawakilishi wetu si ndiyo?
Wawakilishi wetu ndiyo sisi si ndiyo?


Kutokana na ongezeko Kubwa la watu ,tukiendelea kutumia njia za asili Tunaweza timiza mahitaji ya chakula KWA kutumia njia ulizozitaja hapo juu?

Mass production inawezekana KWA mfumo huo?
Unazo akili, acha baya chukua jema. Usifanye jambo kwasababu wengine wanafanya au kwasababu serikali haijakataza. Jali afya yako mwenyewe maana ndiyo mtaji wako wa kwanza kabla haujawa wa serikali.

Ukiona Simba anakuja kukuparura usisubiri serikali itangaze kumkimbia - kimbia mwenyewe!
 
Unazo akili, acha baya chukua jema. Usifanye jambo kwasababu wengine wanafanya au kwasababu serikali haijakataza. Jali afya yako mwenyewe maana ndiyo mtaji wako wa kwanza kabla haujawa wa serikali.

Ukiona Simba anakuja kukuparura usisubiri serikali itangaze kumkimbia - kimbia mwenyewe!
Tunafanya ubishi , umuch know, tunatafuta ushindi au ni tunatafuta suluhu ya Kupata chakula bora na salama?

Umeusoma mchango wangu ukauelewa?
 
Tunafanya ubishi , umuch know, tunatafuta ushindi au ni tunatafuta suluhu ya Kupata chakula bora na salama?

Umeusoma mchango wangu ukauelewa?
Ninachoandika ni ushauri tu kwa yeyote yule, una uhuru wa kuufuata au kuupuzia na hutalaumiwa. Na hakuna ubishi wala ushindani.
 
Back
Top Bottom