Tujenge utaratibu wa kusafiri na vyakula vya kula njiani

Tujenge utaratibu wa kusafiri na vyakula vya kula njiani

Sky Eclat

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2012
Posts
57,761
Reaction score
216,011
Wenye hoteli za njiani wengi hawatapenda hili bandiko. Lakini kusafiri na chakula ni muhimu hasa unapokua na watoto. Bei ya vyakula njiani ni kubwa pia ubora wake unatia mashaka.

Unakuta viazi vitamu viko kwenye karai vimepata vumbi la kutosha tu, vingine unanunua unagundua vimeanza kuoza havikua vya jana, vilibaki juzi na muuzaji anaokoa mtaji wake.

Fikiria uko na watoto, basi limesimama wote wnanataka kujisaidia, mkimaliza huduma hii, dereva ameanza kupiga honi mnatakiwa mrudi kwenye gari safari iendelee. Ukute dereva yuko kwenye ligi na dereva mwenzake wa basi lingine. Ukimfahamisha watoto hawajakula anaona unampotezea muda.

Gari linaweza kuharibika katikati ya pori.

Kama unasafiri na watoto andaa kikapu ndani weka chupa za maji, mkate, ukiweza nunua kilo ya nyama chemsha na uikaange. Matunda pia usisahau karatasi za kusafishia mikono.

Kuwa mstaarabu, mabaki ya chakula yahifadhi vizuri uyatupe sehemu stahiki.
 
Ni wazo zuri isipokuwa kwenye safari za emergency sasa.
 
Asante kwa kutukumbusha najua mengi sana mpaka tunasahauu
 
Wenye hoteli za njiani wengi hawatapenda hili bandiko. Lakini kusafiri na chakula ni muhimu hasa unapokua na watoto. Bei ya vyakula njiani ni kubwa pia ubora wake unatia mashaka. Unakuta viazi vitamu viko kwenye karai vimepata vumbi la kutosha tu, vingine unanunua unagundua vimeanza kuoza havikua vya jana, vilibaki juzi na muuzaji anaokoa mtaji wake...
Nimeyaona wiki iliyopita pale hoteli ya Mwarabu pake Mombo; tumeuziwa chips na nyama 'ndaza', nilipomuuliza konda, alikubaliana na madai yangu na kuniambia kuwa wenye hiyo hoteli wamemshika mwenye kampuni ya mabasi na wasipoingia pale huwa ni kesi na kazi inaweza kuota nyasi.

Nimejiapiza sitapanda basi lao lolote kwenda/kutoka Arusha kwa sababu ya hoteli ya Mwarabu.

Vv
 
Sehemu kubwa duniani sehemu za kula njiani bei huchangamka ndomana wengine tunazugia korosho na biskuti mpaka ufike

Ova
 
Uko sahii kabisa bibieee.....zamani anti yangu alikuwa anatoka Kanda ya ziwaa anakuja Kilimanjaro alikua anafungasha haswa,siku moja kablaa ya kuondokaa ananunua kuku wawilii,au nyama ya ngombee anakaaangaa vizuri,plus viazi au ndizi,na themothi za ujii Kama mbili maana alikua anakuja na team yake ya watoto Kama watatu,walaaaah nilikua naona shangazi anaendaa nchi gani kwani?kipindi hiyo gari ya mwanza Ni Jordan na barabara ya vumbi au upitie nairobi.now nimekua nikajua maana ya alichokuwa anafanya
 
Pale K'njaro na Rock city(kama sijakosea) tumwachie nani. Vyakula vya safari vitam bwana asikwambie mtu.
 
Wenye hoteli za njiani wengi hawatapenda hili bandiko. Lakini kusafiri na chakula ni muhimu hasa unapokua na watoto. Bei ya vyakula njiani ni kubwa pia ubora wake unatia mashaka....
Mimi kinachonisumbua na kunihuzunisha ni muda wenyewe wa kula na umbali wa uchumba dawa toka kituo kimoja kwenda kingine. Mfano mtu anatoka dodoma hadi singida ndo anachimba dawa? Vipi kuhusu wagonjwa wa na watoto???
 
Mimi kinachonisumbua na kunihuzunisha ni muda wenyewe wa kula na umbali wa uchumba dawa toka kituo kimoja kwenda kingine. Mfano mtu anatoka dodoma hadi singida ndo anachimba dawa? Vipi kuhusu wagonjwa wa na watoto???
Hapo dereva amebeti na mwenzake, ukiwa na tumbo la kuhara pole.
 
Mimi wiki hii nilisafiri Arusha na Kurudi Dar jana, kwenda na kurudi nilikula karanga na korosho tu + maji, maana hili tumbo siliamini tena [emoji23][emoji23][emoji23] tena sehemu ya kula derva katupa dakika 10
 
Wenye hoteli za njiani wengi hawatapenda hili bandiko. Lakini kusafiri na chakula ni muhimu hasa unapokua na watoto. Bei ya vyakula njiani ni kubwa pia ubora wake unatia mashaka....
jifunze kufunga, wakati wa safari, itakuepusha na mengi. Labda kama una vidonda.

Mimi safari za Dar mwanza nafungaga
 
Back
Top Bottom