Tujiandae kumpokea Mbwana Samatta muda wowote kuanzia sasa!!

Mchochezi

JF-Expert Member
Joined
Feb 29, 2012
Posts
10,962
Reaction score
7,830
Kazi kuu ya Mshambuliaji ni kufunga magoli. Mshambuliaji wa klabu ya Genk na timu ya taifa ya Tanzania, Mbwana Ally Samatta amekuwa katika fomu ya chini sana msimu huu.Samatta hafungi tena magoli kama awali, naona kama mwisho wake wa kuendelea kuvheza Genk unakaribia, kama mambo yasipobadilika muda wowote kuanzia sasa Samatta atakuwa anarejea barani Africa kutafuta timu ya kucheza ila sio Tanzania. Huu ni mtazamo tu, msijenge chuki!!
 
Hata Messi hafungi kila mechi. Badala ya kumtakia heri arudi kwenye kiwango chake wewe unatabiria kushindwa na kurudi Afrika.. Aisee hii sijui inatokana na nini...!
 
Atakuwa kapata demu sasa hivi.
 
nimeamini ile usemi wa friend yangu kwel watz hampendani badala ya kumwombea ili azid kupambana na kuangalia shida iko wapi nyie ndio mnamponda na kumwonyeshea pa kutokea duuuu acheni izo wanaeast africa sote ni ndugu. Mbona Wanyama hapewi namba kila mechi hatusemi?????
 
Miaka yake halisi na ya kwenye pasipoti inakinzana mkuu, tuwe tu wapole.
 
Hata Messi hafungi kila mechi. Badala ya kumtakia heri arudi kwenye kiwango chake wewe unatabiria kushindwa na kurudi Afrika.. Aisee hii sijui inatokana na nini...!


Unakosea, ni kweli Messi afung kila mechi ila anatoa assists za kufunga magoli na he makes the team better ila Samatta sivyo hivyo....aliyeleta mada hajakosea.
 
Hata Messi hafungi kila mechi. Badala ya kumtakia heri arudi kwenye kiwango chake wewe unatabiria kushindwa na kurudi Afrika.. Aisee hii sijui inatokana na nini...!
We jamaa hujui mpira unafananisha Messi na Samatta?

Wewe ndio walewale mnaoingia kwenye banda la mpira huku unasikilza redio
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…