Tujifunze makosa ya Kenya katika kuandika katiba mpya yetu

Tujifunze makosa ya Kenya katika kuandika katiba mpya yetu

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Kenya pamoja na kuwa na katiba mpya ila inaonekana bado kuna mambo hayakuwekwa sawa katika katiba hiyo.

Mambo kadhaa bado hayajaweza kupatiwa ufumbuzi kupitia katiba yao mpya hayo ni pamoja na;

1.Ubadhirifu mkubwa wa pesa za umma,
Nchini Kenya pesa za walipakodi bado zinafanyiwa ufisadi mkubwa sana kama sehemu nyingine za Africa kupitia miradi na tenda mbalimbali kubwa na hakuna uwajibikaji kabisa katika hili. Katiba yao haijaweza kutibu jambo ubadhirifu na ufisadi.

2.Mamlaka ya Urais bado haikuwekewa vizingiziti vya kutosha "checks and balances.
Tangu ameingia madarakani Rais Ruto amefanya mambo yanoyothibitisha hilo.
Amewafukuza kazi wakuu wa mashirika na wenyeviti wengi wa bodi za mashirika ya umma ambao waliteuliwa na mtangulizi wake Rais Uhuru,Kenyatta na anatuhimiwa kuwaweka "loyalists" wake katika nafasi hizo na nyingine nyingi hasa kutoka kabila lake la Kalenjin, hii sio afya kwa mshikamano wa nchi.

Yeye na makamu wake wamemuandama sana hadharani mtangulizi wake Kenyatta na familia yake kuhusu masuala ya kodi. Hii sio sawa, hayo mambo yalifapaswa kushughulikiwa na taasisi husika.

3.Uhamaji wa vyama kiholela kwa viongozi waliochagulia, muda mfupi baada ya Ruto kuchaguliwa wabunge wengi wa Azimio la Umoja walitimkia kwenye kambi ya Ruto, kuna tuhuma kwamba kuna biashara ya manunuzi ilifanyika na inaendelea kufanyika.

Siku tutakapoamua na kukubaliana kuwa na katiba mpya katika taifa hili ni vizuri turejee na tujifunze kutoka kwa hawa majirani zetu ambao tumekuwa tukiisifia sana katiba yao.
 
Kenya pamoja na kuwa na katiba mpya ila inaonekana bado kuna mambo hayakuwekwa sawa katika katiba hiyo.

Mambo kadhaa bado hayajaweza kupatiwa ufumbuzi kupitia katiba yao mpya hayo ni pamoja na;

1.Ubadhirifu mkubwa wa pesa za umma,
Nchini Kenya pesa za walipakodi bado zinafanyiwa ufisadi mkubwa sana kama sehemu nyingine za Africa kupitia miradi na tenda mbalimbali kubwa na hakuna uwajibikaji kabisa katika hili. Katiba yao haijaweza kutibu jambo ubadhirifu na ufisadi.

2.Mamlaka ya Urais bado haikuwekewa vizingiziti vya kutosha "checks and balances.
Tangu ameingia madarakani Rais Ruto amefanya mambo yanoyothibitisha hilo.
Amewafukuza kazi wakuu wa mashirika na wenyeviti wengi wa bodi za mashirika ya umma ambao waliteuliwa na mtangulizi wake Rais Uhuru,Kenyatta na anatuhimiwa kuwaweka "loyalists" wake katika nafasi hizo na nyingine nyingi hasa kutoka kabila lake la Kalenjin, hii sio afya kwa mshikamano wa nchi.

Yeye na makamu wake wamemuandama sana hadharani mtangulizi wake Kenyatta na familia yake kuhusu masuala ya kodi. Hii sio sawa, hayo mambo yalifapaswa kushughulikiwa na taasisi husika.

3.Uhamaji wa vyama kiholela kwa viongozi waliochagulia, muda mfupi baada ya Ruto kuchaguliwa wabunge wengi wa Azimio la Umoja walitimkia kwenye kambi ya Ruto, kuna tuhuma kwamba kuna biashara ya manunuzi ilifanyika na inaendelea kufanyika.

Siku tutakapoamua na kukubaliana kuwa na katiba mpya katika taifa hili ni vizuri turejee na tujifunze kutoka kwa hawa majirani zetu ambao tumekuwa tukiisifia sana katiba yao.
Tatizo la africa si kutokuwa na katiba ni uadilifu na utashi wa kutii katiba. Katiba ya marekani ina maneno 4,543 ikiwa ni pamoja na sahihi. Baada ya kufanyiwa ammendments 27 ndiyo ikawa na maneno 7591. Lakini pamoja na udogo wake, wamarekani wana utashi wa wazi wa kutii katiba na sheria zao.

Africa hicho kitu hakipo. Tutaandika volume and volumes za katiba. Lakini je, utashi tunao?

Kutii sheria tu za uchaguzi vyama tawala havitaki
 
Suala la ubadhirifu wa mali za umma ni la kijinai; mahakama zipo, labda kama hazina mamlaka.

Kenyata kuandamwa kwa masuala ya kikodi ni jambo sahihi tunalopaswa kuiga kwa wakenya.

Baya ninaloliona labda ni hilo la wabunge kubadilisha vyama kama nguo.
 
Haina haja ya katiba, hata Sasa hivi, Kenya bei ya chakula juu, Tanzania juu, Jana Matiangi kavamiwa na polisi, huku tumeacha.

Haina haja ya makatiba, ni kupoteza Hela tu
 
Huyo Matingi ingekuwa Katiba ya enzi za Moi sasa hivi angekuwa ameshapotea kusikojulikana au amekimbia nchi kabisa.
Haina haja ya katiba, hata Sasa hivi, Kenya bei ya chakula juu, Tanzania juu, Jana Matiangi kavamiwa na polisi, huku tumeacha.

Haina haja ya makatiba, ni kupoteza Hela tu
 
Aandamwe na vyombo sahihi bila kupewa maagizo kutoka juu, sio Rais na makamu wake. Siku zote wanasiasa wanapoingiza mikono yao katika taasisi na vyombo vya uchunguzi mambo lazima yaharibike, ndio maana vinatakiwa kuwa huru.
Suala la ubadhirifu wa mali za umma ni la kijinai; mahakama zipo, labda kama hazina mamlaka.

Kenyata kuandamwa kwa masuala ya kikodi ni jambo sahihi tunalopaswa kuiga kwa wakenya.

Baya ninaloliona labda ni hilo la wabunge kubadilisha vyama kama nguo.
 
Aandamwe na vyombo sahihi bila kupewa maagizo kutoka juu, sio Rais na makamu wake. Siku zote wanasiasa wanapoingiza mikono yao katika taasisi na vyombo vya uchunguzi mambo lazima yaharibike, ndio maana vinatakiwa kuwa huru.
Wacha awajibishwe, huwezi kuwa rais halafu hutaki kulipa kodi. Hata rais mstaafu US yanamkuta hayohayo naye analia eti wanasiasa!
 
Tatizo la africa si kutokuwa na katiba ni uadilifu na utashi wa kutii katiba. Katiba ya marekani ina maneno 4,543 ikiwa ni pamoja na sahihi. Baada ya kufanyiwa ammendments 27 ndiyo ikawa na maneno 7591. Lakini pamoja na udogo wake, wamarekani wana utashi wa wazi wa kutii katiba na sheria zao.

Africa hicho kitu hakipo. Tutaandika volume and volumes za katiba. Lakini je, utashi tunao?

Kutii sheria tu za uchaguzi vyama tawala havitaki
Kama watu hawana utashi kwa hiyari vipengele vya katiba vilazimishe watu kuwa na utashi !! Huko marekani uzalendo ni lazima ndio maana zipo sheria za kulazimishana kujiunga na jeshi ikibidi !
 
Back
Top Bottom