Tujifunze na kuiga kutoka Asia, tuachane na kasumba ya kujikomba kwa Wazungu

Tujifunze na kuiga kutoka Asia, tuachane na kasumba ya kujikomba kwa Wazungu

Sijali

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2010
Posts
2,672
Reaction score
1,814
Mwaka 1990, nusu ya raia wa Vietnam walikuwa fukara wa kutupwa zaidi yetu, wakiishi kwa nusu dola kwa siku! Leo, Vietnam kuanzia 2020 imefuta ufukara kabisa!

China, katika uhai wangu, miaka ya 60,70 ilikuwa nyuma kwa maisha ya mtu binafsi hata kuliko Tanzania! Leo, China ni ya kwanza duniani katika kila nyanja isipokuwa chache tu, na ni miaka kumi tu ijayo itaipiku Marekani.

Na ndiyo hivyo, ukitazama nchi nyingi Asia, kama India, Indonesia, Philipino nk stori ni hiyo hiyo. Ni dhahiri kabisa, uongozi wa dunia wa kiuchumi, kisiasa na kielimu utakuwa Asia. Time Magazine limekwisha tabiri kwamba kufikia mwaka 2030 asilimia 90 ya PHD za sayansi na teknolojia watakuwa Waasia!

Kwa upande mwingine, bara la Ulaya linakufa kiuchumi, kisiasa na hata kiutamaduni. Ni suala la muda tu kabla halijachukua nafasi ya tatu baada ya Asia na Amerika.

Ungedhania kuwa wataalamu wetu wa siasa wangejipanga kuanzia sasa kuelekea zaidi Asia, kama patna wa maendeleo. La hasha! Bado hawajang'amua 'transformation' hii kubwa ijayo na bado wanajikombakomba kwa Wazungu, wakiamini kuwa wanaendelea kuwa mabwana wa dunia!
 
Ondoa umaskini wako kwanza, by default nchi itakuwa tajiri. No government can make your life better in this world. No. Serikali inaweka sera Na mazingira wezeshi, sisi tunajipigania wenyewe ndani mazingira hayo wezeshi.
Kwa jicho la mbali hakuna popote Serikali ya Tanzania inamzuia mtanzania kujitafutia pesa kwa nguvu zote akiamua. Tuache malalamiko, let's fight for good life individually.
 
Ondoa umaskini wako kwanza, by default nchi itakuwa tajiri. No government can make your life better in this world. No. Serikali inaweka sera Na mazingira wezeshi, sisi tunajipigania wenyewe ndani mazingira hayo wezeshi.
Kwa jicho la mbali hakuna popote Serikali ya Tanzania inamzuia mtanzania kujitafutia pesa kwa nguvu zote akiamua. Tuache malalamiko, let's fight for good life individually.
Unajua maana ya 'tuige' wewe? China imeiga West ndiyo ikaendelea, sasa wasema nini!
 
Mwaka 1990, nusu ya raia wa Vietnam walikuwa fukara wa kutupwa zaidi yetu, wakiishi kwa nusu dola kwa siku! Leo, Vietnam kuanzia 2020 imefuta ufukara kabisa! China, katika uhai wangu, miaka ya 60,70 ilikuwa nyuma kwa maisha ya mtu binafsi hata kuliko Tanzania! Leo, China ni ya kwanza duniani katika kila nyanja isipokuwa chache tu, na ni miaka kumi tu ijayo itaipiku Marekani.
Na ndiyo hivyo, ukitazama nchi nyingi Asia, kama India, Indonesia, Philipino nk stori ni hiyo hiyo. Ni dhahiri kabisa, uongozi wa dunia wa kiuchumi, kisiasa na kielimu utakuwa Asia. Time Magazine limekwisha tabiri kwamba kufikia mwaka 2030 asilimia 90 ya PHD za sayansi na teknolojia watakuwa Waasia!
Kwa upande mwingine, bara la Ulaya linakufa kiuchumi, kisiasa na hata kiutamaduni. Ni suala la muda tu kabla halijachukua nafasi ya tatu baada ya Asia na Amerika.
Ungedhania kuwa wataalamu wetu wa siasa wangejipanga kuanzia sasa kuelekea zaidi Asia, kama patna wa maendeleo. La hasha! Bado hawajang'amua 'transformation' hii kubwa ijayo na bado wanajikombakomba kwa Wazungu, wakiamini kuwa wanaendelea kuwa mabwana wa dunia!
Hatupaswi kujitenga na watu wa Ulaya & Marekani/ magharibi [ Wazungu ] pia hatupaswi kujitenga na watu wa mashariki Asia ya mbali [ China, India, Korea, Japan, Vietnam, Singapore, Malaysia, ASEAN n.k ].

Hata mataifa ya Asia nayo haya kujitenga na wala hayajitengi na mataifa ya magharibi [ Wazungu ].

: Tunapaswa kushirikiana na mataifa yote kwa manufaa yetu kiuchumi.
 
Hatupaswi kujitenga na watu wa Ulaya & Marekani/ magharibi [ Wazungu ] pia hatupaswi kujitenga na watu wa mashariki Asia ya mbali [ China, India, Korea, Japan, Vietnam, Singapore, Malaysia, ASEAN n.k ].

Hata mataifa ya Asia nayo haya kujitenga na wala hayajitengi na mataifa ya magharibi [ Wazungu ].

: Tunapaswa kushirikiana na mataifa yote kwa manufaa yetu kiuchumi.
Nakukubali deng ...

Mjamapari( Mjamaabwpari)

Viongozi naowaheshimu na kuwakubali ...


Mao- Cultural revolution...

Deng - Kuifungua china kimataifa...

Lee kuan yew- Father of modern singapore.

Hapo ni KWA viongozi wa kimataifa
 
Asia wenyewe wameiga kwa wazungu
Japan, Singapore, Korea Kusini, Hong Kong, nchi hizi unafikiri zilitumia ujima wao wa kizaamani kufikia hapo walipo?

Au unamaanisha Waarabu
 
Hatupaswi kujitenga na watu wa Ulaya & Marekani/ magharibi [ Wazungu ] pia hatupaswi kujitenga na watu wa mashariki Asia ya mbali [ China, India, Korea, Japan, Vietnam, Singapore, Malaysia, ASEAN n.k ].

Hata mataifa ya Asia nayo haya kujitenga na wala hayajitengi na mataifa ya magharibi [ Wazungu ].

: Tunapaswa kushirikiana na mataifa yote kwa manufaa yetu kiuchumi.
Mkuu deng Wacha nikupatie zawadi siku ya leo...


"The Munger Series - Learning from Lee Kuan Yew — Investment Masters Class" The Munger Series - Learning from Lee Kuan Yew — Investment Masters Class
 
Nakukubali deng ...

Mjamapari( Mjamaabwpari)

Viongozi naowaheshimu na kuwakubali ...


Mao- Cultural revolution...

Deng - Kuifungua china kimataifa...

Lee kuan yew- Father of modern singapore.

Hapo ni KWA viongozi wa kimataifa
Upo sahihi mkuu, hao mabwana walifanya vizuri sana, naomba pia umpitie mtoto wetu wa Afrika[ Thomas Sankara ] kupitia reform za kiuchumi alizo wafanyia Burkina Faso na pia mpitie Park Chung Hee pale South Korea kupitia uchumi wa Viwanda alio ufanya.
 
Ondoa umaskini wako kwanza, by default nchi itakuwa tajiri. No government can make your life better in this world. No. Serikali inaweka sera Na mazingira wezeshi, sisi tunajipigania wenyewe ndani mazingira hayo wezeshi.
Kwa jicho la mbali hakuna popote Serikali ya Tanzania inamzuia mtanzania kujitafutia pesa kwa nguvu zote akiamua. Tuache malalamiko, let's fight for good life individually.
Asante sana, huu ujinga wa kutaka serikali ifanye kila kitu naku control uchumi ni ujinga mkubwa, na masikini wajinga ndio utakuta wana haya mawazo ya kipuuzi hivi
 
Mwaka 1990, nusu ya raia wa Vietnam walikuwa fukara wa kutupwa zaidi yetu, wakiishi kwa nusu dola kwa siku! Leo, Vietnam kuanzia 2020 imefuta ufukara kabisa! China, katika uhai wangu, miaka ya 60,70 ilikuwa nyuma kwa maisha ya mtu binafsi hata kuliko Tanzania! Leo, China ni ya kwanza duniani katika kila nyanja isipokuwa chache tu, na ni miaka kumi tu ijayo itaipiku Marekani.
Na ndiyo hivyo, ukitazama nchi nyingi Asia, kama India, Indonesia, Philipino nk stori ni hiyo hiyo. Ni dhahiri kabisa, uongozi wa dunia wa kiuchumi, kisiasa na kielimu utakuwa Asia. Time Magazine limekwisha tabiri kwamba kufikia mwaka 2030 asilimia 90 ya PHD za sayansi na teknolojia watakuwa Waasia!
Kwa upande mwingine, bara la Ulaya linakufa kiuchumi, kisiasa na hata kiutamaduni. Ni suala la muda tu kabla halijachukua nafasi ya tatu baada ya Asia na Amerika.
Ungedhania kuwa wataalamu wetu wa siasa wangejipanga kuanzia sasa kuelekea zaidi Asia, kama patna wa maendeleo. La hasha! Bado hawajang'amua 'transformation' hii kubwa ijayo na bado wanajikombakomba kwa Wazungu, wakiamini kuwa wanaendelea kuwa mabwana wa dunia!
ndoto za asubuhi huwa tamu sana....
 
Ondoa umaskini wako kwanza, by default nchi itakuwa tajiri. No government can make your life better in this world. No. Serikali inaweka sera Na mazingira wezeshi, sisi tunajipigania wenyewe ndani mazingira hayo wezeshi.
Kwa jicho la mbali hakuna popote Serikali ya Tanzania inamzuia mtanzania kujitafutia pesa kwa nguvu zote akiamua. Tuache malalamiko, let's fight for good life individually.
Unaweza kuni tofautishia kati ya China ya Chairman Mao Zedong na ya Deng Xiaoping ?
 
Kutokujiamini na ujinga pia unachangia
Unamuita fundi anakuomba nyundo
Uaminifu zero
Mnahitaji kuwa waaminifu na wachapakazi haswa
 
Ondoa umaskini wako kwanza, by default nchi itakuwa tajiri. No government can make your life better in this world. No. Serikali inaweka sera Na mazingira wezeshi, sisi tunajipigania wenyewe ndani mazingira hayo wezeshi.
Kwa jicho la mbali hakuna popote Serikali ya Tanzania inamzuia mtanzania kujitafutia pesa kwa nguvu zote akiamua. Tuache malalamiko, let's fight for good life individually.
Pamoja na ukweli kuwa mtu binafsi lazima apambane kuondoa umaskini, bado sera na maono ya serekali zina nafasi kubwa sana ktk kufuta umaskini. Chukulia mfano wa mkulima anayeshindwa kufikisha mazao yake sokoni kwa vile hakuna miundo mbinu au wakati mwingine sekekali inamzuia kuuza mazao yake. Huyu mkulima hata akiongeza bidii kiasi gani hatoboi.
Angalia kwa wenzetu wanavyolinda viwanda vyao kwa kuzuia uagiza holela wa bidhaa kutoka nje ili kulinda viwanda na ajira. Hapa kwetu soko liko huru hata kwa bidhaa hafifu toka nje. Matokeo yake hakuna ajira, maelfu ya vijana wako barabarani wakiuza mitumba na bidhaa hafifu toka China.
 
Pamoja na ukweli kuwa mtu binafsi lazima apambane kuondoa umaskini, bado sera na maono ya serekali zina nafasi kubwa sana ktk kufuta umaskini. Chukulia mfano wa mkulima anayeshindwa kufikisha mazao yake sokoni kwa vile hakuna miundo mbinu au wakati mwingine sekekali inamzuia kuuza mazao yake. Huyu mkulima hata akiongeza bidii kiasi gani hatoboi.
Angalia kwa wenzetu wanavyolinda viwanda vyao kwa kuzuia uagiza holela wa bidhaa kutoka nje ili kulinda viwanda na ajira. Hapa kwetu soko liko huru hata kwa bidhaa hafifu toka nje. Matokeo yake hakuna ajira, maelfu ya vijana wako barabarani wakiuza mitumba na bidhaa hafifu toka China.
Sahihi
 
Mwaka 1990, nusu ya raia wa Vietnam walikuwa fukara wa kutupwa zaidi yetu, wakiishi kwa nusu dola kwa siku! Leo, Vietnam kuanzia 2020 imefuta ufukara kabisa! China, katika uhai wangu, miaka ya 60,70 ilikuwa nyuma kwa maisha ya mtu binafsi hata kuliko Tanzania! Leo, China ni ya kwanza duniani katika kila nyanja isipokuwa chache tu, na ni miaka kumi tu ijayo itaipiku Marekani.
Na ndiyo hivyo, ukitazama nchi nyingi Asia, kama India, Indonesia, Philipino nk stori ni hiyo hiyo. Ni dhahiri kabisa, uongozi wa dunia wa kiuchumi, kisiasa na kielimu utakuwa Asia. Time Magazine limekwisha tabiri kwamba kufikia mwaka 2030 asilimia 90 ya PHD za sayansi na teknolojia watakuwa Waasia!
Kwa upande mwingine, bara la Ulaya linakufa kiuchumi, kisiasa na hata kiutamaduni. Ni suala la muda tu kabla halijachukua nafasi ya tatu baada ya Asia na Amerika.
Ungedhania kuwa wataalamu wetu wa siasa wangejipanga kuanzia sasa kuelekea zaidi Asia, kama patna wa maendeleo. La hasha! Bado hawajang'amua 'transformation' hii kubwa ijayo na bado wanajikombakomba kwa Wazungu, wakiamini kuwa wanaendelea kuwa mabwana wa dunia!
Kwa serikali gani? kwa katiba ipi? SAHAU milele.
 
Kuhakikisha kunakuwepo na mazingira mazuri na "fair competition" katika kufanya biashara na uwekezaji, kusimamia sheria, kukusanya kodi na kudhibiti "negative market externalities".
Kwani jukumu la serikali ni lipi katika uchumi ?
 
Uko sahihi
Pamoja na ukweli kuwa mtu binafsi lazima apambane kuondoa umaskini, bado sera na maono ya serekali zina nafasi kubwa sana ktk kufuta umaskini. Chukulia mfano wa mkulima anayeshindwa kufikisha mazao yake sokoni kwa vile hakuna miundo mbinu au wakati mwingine sekekali inamzuia kuuza mazao yake. Huyu mkulima hata akiongeza bidii kiasi gani hatoboi.
Angalia kwa wenzetu wanavyolinda viwanda vyao kwa kuzuia uagiza holela wa bidhaa kutoka nje ili kulinda viwanda na ajira. Hapa kwetu soko liko huru hata kwa bidhaa hafifu toka nje. Matokeo yake hakuna ajira, maelfu ya vijana wako barabarani wakiuza mitumba na bidhaa hafifu toka China.
 
Back
Top Bottom