Tujifunze na kuiga kutoka Asia, tuachane na kasumba ya kujikomba kwa Wazungu

Tujifunze na kuiga kutoka Asia, tuachane na kasumba ya kujikomba kwa Wazungu

Mwaka 1990, nusu ya raia wa Vietnam walikuwa fukara wa kutupwa zaidi yetu, wakiishi kwa nusu dola kwa siku! Leo, Vietnam kuanzia 2020 imefuta ufukara kabisa! China, katika uhai wangu, miaka ya 60,70 ilikuwa nyuma kwa maisha ya mtu binafsi hata kuliko Tanzania! Leo, China ni ya kwanza duniani katika kila nyanja isipokuwa chache tu, na ni miaka kumi tu ijayo itaipiku Marekani.
Na ndiyo hivyo, ukitazama nchi nyingi Asia, kama India, Indonesia, Philipino nk stori ni hiyo hiyo. Ni dhahiri kabisa, uongozi wa dunia wa kiuchumi, kisiasa na kielimu utakuwa Asia. Time Magazine limekwisha tabiri kwamba kufikia mwaka 2030 asilimia 90 ya PHD za sayansi na teknolojia watakuwa Waasia!
Kwa upande mwingine, bara la Ulaya linakufa kiuchumi, kisiasa na hata kiutamaduni. Ni suala la muda tu kabla halijachukua nafasi ya tatu baada ya Asia na Amerika.
Ungedhania kuwa wataalamu wetu wa siasa wangejipanga kuanzia sasa kuelekea zaidi Asia, kama patna wa maendeleo. La hasha! Bado hawajang'amua 'transformation' hii kubwa ijayo na bado wanajikombakomba kwa Wazungu, wakiamini kuwa wanaendelea kuwa mabwana wa dunia!
Ni kweli
Lakini Asia pia ina man power yakutosha.......ina zaidi ya watu billion 4
Wanajitosheleza kwa mengi tu
 
Ondoa umaskini wako kwanza, by default nchi itakuwa tajiri. No government can make your life better in this world. No. Serikali inaweka sera Na mazingira wezeshi, sisi tunajipigania wenyewe ndani mazingira hayo wezeshi.
Kwa jicho la mbali hakuna popote Serikali ya Tanzania inamzuia mtanzania kujitafutia pesa kwa nguvu zote akiamua. Tuache malalamiko, let's fight for good life individually.
Serikali Kazi yake hasa ni nini ? Je wakulima wanapewa ruzuku au vyama vya siasa ndivyo vinavyopewa ruzuku ?!!! Je serikali kwa kujua asilimia kubwa ya wananchi wake wanategemea kilimo je ni mipango gani inafanywa baada ya miaka 60 ya uhuru ili tusiwe tunategemea mvua katika kilimo chetu ?maana hali ya ukame na mvua zisizotabirika imekuwa ni janga kwa Nchi yetu !!? Au ni vyema watu wote tuwe ni watu wa kupiga madili ili tutajirike individualy kama ulivyoshauri ?!! ALIYESHIBA huwa hamjui mwenye njaa. !!
 
Mwaka 1990, nusu ya raia wa Vietnam walikuwa fukara wa kutupwa zaidi yetu, wakiishi kwa nusu dola kwa siku! Leo, Vietnam kuanzia 2020 imefuta ufukara kabisa! China, katika uhai wangu, miaka ya 60,70 ilikuwa nyuma kwa maisha ya mtu binafsi hata kuliko Tanzania! Leo, China ni ya kwanza duniani katika kila nyanja isipokuwa chache tu, na ni miaka kumi tu ijayo itaipiku Marekani.
Na ndiyo hivyo, ukitazama nchi nyingi Asia, kama India, Indonesia, Philipino nk stori ni hiyo hiyo. Ni dhahiri kabisa, uongozi wa dunia wa kiuchumi, kisiasa na kielimu utakuwa Asia. Time Magazine limekwisha tabiri kwamba kufikia mwaka 2030 asilimia 90 ya PHD za sayansi na teknolojia watakuwa Waasia!
Kwa upande mwingine, bara la Ulaya linakufa kiuchumi, kisiasa na hata kiutamaduni. Ni suala la muda tu kabla halijachukua nafasi ya tatu baada ya Asia na Amerika.
Ungedhania kuwa wataalamu wetu wa siasa wangejipanga kuanzia sasa kuelekea zaidi Asia, kama patna wa maendeleo. La hasha! Bado hawajang'amua 'transformation' hii kubwa ijayo na bado wanajikombakomba kwa Wazungu, wakiamini kuwa wanaendelea kuwa mabwana wa dunia!

Mpaka tutakapojitambua, ndipo tutakapotoka kwenye hili lindi la umasikini. Inasikitisha sana kuona Afrika bado ina imani kubwa sana kwamba bila nchi za magharibi, hatuwezi kufanya lolote. Tumepumbazwa akili, tunaona kila kitu kutoka magharibi ni bora.
Mfano wanasema nchi zote zilizokuwa makoloni ya ufaransa bado hazina uhuru kiuchumi. Zinanyonywa waziwazi na ufaransa. Lakini hilo, halijawahi hata siku moja kuelezea namna zinavyonyonywa, lkn pia namna ya kujitoa na unyonyaji huo.

Kuhusu kuiga nchi za Asia, huo ndiyo uwe muelekeo wa Afrika. Tukajifunze wenzetu wamefanya nini, nasi tunapaswa kufanya nini kutokana na mazingira yetu.
 
Back
Top Bottom