Tujikumbushe enzi za ufalme wa Inspector Haroun

Gangwe Mobb hao wakiwa na GWM upande wa kushoto Inspector kainamia meza anaandika na wa mbele yake Dogo Side, na upande wa kulia D-Chief kushoto na KR Mullah kulia. ....

Wakati wa tamasha la 'Mwaka Elfu Mbili' lililoandaliwa na Madunia Foundation mnamo tarehe 09/05/1999....
 
Lakinj huyo Inspector ndo alichukua nafasi ya pili baada ya Afande, huku nafasi ya 3 ikienda kwa Mandojo na Domokaya
 
Nature mbona alikuwepo katika shindano na Sitaki demu? Watu kumbukumbu zenu mnaziacha wapi?
 
Nature mbona alikuwepo katika shindano na Sitaki demu? Watu kumbukumbu zenu mnaziacha wapi?
Mmh! sikumbuki kwakweli kama nature alikuepo na kama alikuepo basi ata top5 hakuingia
 
Hahaha we jamaa una furahisha sana Amin amin nakuambia juma nature na kismat chake ajawahi fika ata nusu ya diamond sembuse inspector harun (babu) in jesus’s Voice
Hapa unamkosea Juma nature ..huwezi kufananisha zama hizi ambazo sisi mashabiki ndo tunatafuta mziki na zama za nature ambazo mziki ndo ulikuwa unatafuta mashabiki.
 
Baadae kidogo binti huyu MTANASHAATI.. ili mradi tu vina vitimie hata kama havina maana.. labda ndo sababu wakaiita rap katuni
In fact hii RAP KATUNI aliichukia sana Solo Thang, na kuwadiss sana Gangwe Mobb kwamba wanaharibu hip hop. Ukisikiliza wimbo wa Wateule unaoitwa "Tumerudi Tena" Solo kawananga sana Gangwe mobb na staili yao ya rap katuni.
 
Uko sahihi ndg. Wimbo wa kwanA wa Nature unaitwa "JINSI KIJANA".
 
unazungumzia GADO wakati kuna NGANGARI ishatoka kitambo kabla.
 
Mimi nilikua mdogo sana nilitekwa na upepo wa darubini ila nilivyopata upeo wa kupambanua mambo nikaona Prof. alistahili kupata ule ushindi...
Prof Jay ni zaidi ya wote hao, sema ushabiki tu si unajua Afande alikuja na kikosi chake kutoka Moro
 
Dah hawa jamaa wamelitoa game mbali sana lakini hawajafaidi kabisa matunda, nimewahi kumuona KR Mullar anagombea kudandia daladala la kwenda TMK pale baharini Posta nikashikwa na huruma, hawakustahili kuishi hivi. Wasanii wa dizaini hii hata Mungu akiwachukua jamii haiwapi uzito, ila hao wakina Masogange mabingwa wa kuonesha makalio watu hadi wanazimia.
 
Ya kwanza alifanya Nature na Dolo ikafanya vizuri kiasi, ilipoachiwa Remix ya Inspecta ile OG ikasahaulika kabisa. Ukisikia tu OHoo HOoo... (Sauti ya Inspekta[emoji16]) unajua nini kinafuatia.
nakumbuka ilikuwa Nature na KR sio Dolo...
 
e
Lakinj huyo Inspector ndo alichukua nafasi ya pili baada ya Afande, huku nafasi ya 3 ikienda kwa Mandojo na Domokaya

That was nonsense, ndio maana mashindano yalishindwa kuendelea
 
Mkuu acha tu yani inasikitisha sana
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…