Tujikumbushe historia ya bakwata october - december 1968 sehemu ya pili

Tujikumbushe historia ya bakwata october - december 1968 sehemu ya pili

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
21,967
Reaction score
32,074
Hata hivyo, tarehe 14 Novemba, 1968, Baraza la EAMWS la Tanzania liliitisha mkutano wajumbe kutoa mikoa yote ya Tanzania kujadili ‘’mgogoro.’’

Pamoja na waliohudhuria ni wajumbe kutoka mikoa ambayo tayari ilikuwa imekwishajitenga na EAMWS.

Mkutano huu ulifanyika katika shule ya Kiislam ya Kinondoni.

Hapajatokea katika historia ya Uislam Tanzania mkutano kama ule.

Uongozi ulikuwa unaingia katika chumba cha mkutano tayari umeshajeruhiwa vibaya sana na propaganda za magazeti ya TANU na radio ya serikali.

Katika moja ya shutuma ambazo zilikuwa zikiandama uongozi wa EAMWS ilikuwa ni matumizi mabaya ya fedha za jumuiya.

Akifungua mkutano ule Tewa aliwatahadharisha wajumbe kuwa makini katika lolote watakaloamua kwa kuwa endapo wajumbe watashindwa kuafikiana basi matokeo yake ni kuvunjika kwa EAMWS, umoja wa Waislam na mwisho ya miradi yote ya elimu pamoja na ujenzi wa Chuo Kikuu.

Hisia kali zilitawala mkutano huu na baadhi ya wajumbe wanawake walikuwa wakilia hasa pale baadhi ya wajumbe walipokuwa wakitoa michango yao katika mjadala walipokuwa wakisoma aya za Qurían Tukufu na kueleza fadhila za kupigana jihad dhidi ya madhalimu na wanafiki.

Hisia hizi kali zilitokana na ukweli kuwa wajumbe walikuwa wanafahamu kuwa wale wenzao waliokuwa wakidai kujitenga walikuwa wakitumikia Ibilis tu na wala msimamo waliokuwanao haukuwa wao wala hawakuwa wanayafanya yale kwa mapenzi ya Allah na Mtume wake.

Mwenyekiti wa mkutano Tewa Said Tewa aliahirisha mkutano hadi siku ya pili ili wajumbe wapoe na watoe mchango wakiwa katika hali ya utulivu.

Katika wajumbe ambao walisimama kidete kutetea umoja wa Waislam walikuwa Sheikh Issa Mchowera kutoka Mtwara, Bilali Rehani Waikela, Hassan Johari na Sheikh Abdallah Said kutoka Kigoma.

Mkutano uliamua kuunda Tume ya Uchunguzi ya watu saba kuchunguza chanzo cha ‘’mgogoro’’ na kisha itoe taarifa.

Mussa Kwikima kijana mwanasheria alichaguliwa kuwa katibu wa tume ile ya uchunguzi.

Wakati huo mikoa tisa ilikuwa tayari imeshajitenga na EAMWS na magazeti ya TANU yakawa tayari yamejenga ‘’mgogoro’’ ule kufikia hali ya kuonekana kuwa ni ‘’mgogoro’’ wa taifa zima ambao kila mtu anaweza kuuingilia na kusema atakalo.

Magazeti ya TANU yakawa yanaandika na kuchapisha mambo ya EAMWS kama wanavyotaka, wakizidi kutia chumvi katika ugomvi ambao tayari ulikuwa umeshaleta hofu na farka kubwa katika jamii.
 
Miaka hio wagalatia wengi walikuwa wanavaa zile kaptula wanazovaa waingereza. Wakidhani watafanana nao.
Mpk Nyerere kafundishwa kuvaa vizuri na wazee wa kiislamu
LEO wanajiona wasomi.
Kweli dunia hadaa.

Wayahudi wa pugu msianze kutuchafulia uzi.
 
Miaka hio wagalatia wengi walikuwa wanavaa zile kaptula wanazovaa waingereza. Wakidhani watafanana nao.
Mpk Nyerere kafundishwa kuvaa vizuri na wazee wa kiislamu
LEO wanajiona wasomi.
Kweli dunia hadaa.

Wayahudi wa pugu msianze kutuchafulia uzi.
Lakini bado wachafu sana, wanatembea na chenji ya toilet.
Halafu huu usomi wanaodai, mbona hamna kitu, ukiwabana wanaweweseka
Anyway, jana wakaufuta ule uzi ? kulikoni

Turudi kwenye mada..........endelea Sheikh Mo
 
Lakini bado wachafu sana, wanatembea na chenji ya toilet.
Halafu huu usomi wanaodai, mbona hamna kitu, ukiwabana wanaweweseka
Anyway, jana wakaufuta ule uzi ? kulikoni

Turudi kwenye mada..........endelea Sheikh Mo
Wagala wakiona maji yamefika puani wanaanza kulia kwa Mods uzi ufungwe.
Hoja za msingi hawana.
Kitabu Chao hawakijui.
Kuna mistari tukiwapa wanadhani tumetunga kumbe imo humo humo kwenye kitabu Chao.

Kazi kweli kweli
 
Miaka hio wagalatia wengi walikuwa wanavaa zile kaptula wanazovaa waingereza. Wakidhani watafanana nao.
Mpk Nyerere kafundishwa kuvaa vizuri na wazee wa kiislamu
LEO wanajiona wasomi.
Kweli dunia hadaa.

Wayahudi wa pugu msianze kutuchafulia uzi.
Kweli Mkuu nakubaliana na wewe. Hata aliporudi masomoni kutoka UK akafundishwa kuvaa suti na Wazee wa Pwani
 
Kismboy njoo uone wakiristo wanavyokashifu waislam
Why watanzania tunaendelea kuwa ng"ombe na tunashindwa na wenzetu wote hata kwenye majadiliano.
Sababu kuu ni kubishania upumbavu. Kuonyesha nani anajua zaidi.
Halafu tukishamaliza kubishania upumbavu hakuna yyt aliyepata faida.

Haya we chukulia waislamu wameshindwa kwenye mabishano au matusi na wakristo.
Nakuuliza nani kapata faida hapo?
Ukiwa na point ya maana weka hapa watu wapate faida.
Ukiona mtu anaandika uongo mpe ukweli.
Ukiona analeta nyodo mpe maneno yake afunge domokaya.

Lkn sio kualikana kwa LENGO LA KUBISHANA.

Tutakuwa wapumbavu mpk mwisho wa dunia.
 
Back
Top Bottom