Tujikumbushe huyu muimbaji- Sipho Mabuse

Tujikumbushe huyu muimbaji- Sipho Mabuse

Kyenju

JF-Expert Member
Joined
Jun 16, 2012
Posts
4,632
Reaction score
1,773
Sipho Mabuse alizaliwa Jijini Johannesburg- Afrika ya Kusini tarehe 2 Novemba 1951.

Alianza kazi ya Muziki mwaka 1970, akiwa na wenzake walikuwa wakiimba muziki wenye vionjo vya Kiafrika.

Lakini baada ya Ziara yao yenye mafanikio makubwa nchini Zimbabwe, walirejea nyumbani na kubadirisha jina la Kikundi chao na kukiita Harari, kuanzia hapo wakaanza kuimba muziki wenye vionjo vya Kimagharibi, kama vile funk, pop, na soul wakiimba katika lugha ya Kizulu na Kisotho.

Kwa wale mliokula chumvi kidogo kama mie katika miaka ya 1980-90 mnakumbuka jinsi huyu jamaa alivyofanya vizuri sana kati ya Wanamuziki wa Bondeni.

Aliimba nyimbo nyingi lakini kuna nyimbo ambazo zilifanya vizuri sana, kama vile:
1. Jive Soweto
2. Nelson Mandela
3. Shikika
4. Zanzibar

Kuzipata hizi nyimbo na nyingine zipatazo 20, fungua hii link.

Sipho Mabuse Lyrics, Song Meanings, Videos, Full Albums & Bios
 
Sipho Mabuse alizaliwa Jijini Johannesburg- Afrika ya Kusini tarehe 2 Novemba 1951.

Alianza kazi ya Muziki mwaka 1970, akiwa na wenzake walikuwa wakiimba muziki wenye vionjo vya Kiafrika.

Lakini baada ya Ziara yao yenye mafanikio makubwa nchini Zimbabwe, walirejea nyumbani na kubadirisha jina la Kikundi chao na kukiita Harari, kuanzia hapo wakaanza kuimba muziki wenye vionjo vya Kimagharibi, kama vile funk, pop, na soul wakiimba katika lugha ya Kizulu na Kisotho.

Kwa wale mliokula chumvi kidogo kama mie katika miaka ya 1980-90 mnakumbuka jinsi huyu jamaa alivyofanya vizuri sana kati ya Wanamuziki wa Bondeni.

Aliimba nyimbo nyingi lakini kuna nyimbo ambazo zilifanya vizuri sana, kama vile:
1. Jive Soweto
2. Nelson Mandela
3. Shikika

Kuzipata hizi nyimbo na nyingine zipatazo 20, fungua hii link.

Sipho Mabuse Lyrics, Song Meanings, Videos, Full Albums & Bios
Huyu pia ndio aliyeimba ule wimbo maarufu unaoitwa 'Zanzibar'.

Na aliweka historia kurudi kusoma shule ya secondary akiwa tayari mtu mzima.
 
Kumbuka kuna wanamziki wengi wanaitwa SIPHO
Sipho Mchunu
Sipho Bhengu
Sipho Matabhane nk.
Maana ya neno SIPHO ni zawadi. Linatokana na neno KUPHA.
 
Huyu pia ndio aliyeimba ule wimbo maarufu unaoitwa 'Zanzibar'.

Na aliweka historia kurudi kusoma shule ya secondary akiwa tayari mtu mzima.
Ndiyo alianza kusoma Secondary mwaka 2012 akiwa na miaka 60.
 
Wimbo wake wa Zanzibar huwa haukosekani kwenye playlist yangu.
 
Sipho Mabuse alizaliwa Jijini Johannesburg- Afrika ya Kusini tarehe 2 Novemba 1951.

Alianza kazi ya Muziki mwaka 1970, akiwa na wenzake walikuwa wakiimba muziki wenye vionjo vya Kiafrika.

Lakini baada ya Ziara yao yenye mafanikio makubwa nchini Zimbabwe, walirejea nyumbani na kubadirisha jina la Kikundi chao na kukiita Harari, kuanzia hapo wakaanza kuimba muziki wenye vionjo vya Kimagharibi, kama vile funk, pop, na soul wakiimba katika lugha ya Kizulu na Kisotho.

Kwa wale mliokula chumvi kidogo kama mie katika miaka ya 1980-90 mnakumbuka jinsi huyu jamaa alivyofanya vizuri sana kati ya Wanamuziki wa Bondeni.

Aliimba nyimbo nyingi lakini kuna nyimbo ambazo zilifanya vizuri sana, kama vile:
1. Jive Soweto
2. Nelson Mandela
3. Shikika
4. Zanzibaraw

Kuzipata hizi nyimbo na nyingine zipatazo 20, fungua hii link.

Sipho Mabuse Lyrics, Song Meanings, Videos, Full Albums & Bios
ok, mbona nashindwa kuzidownload sasa hizi nyimbo ?
 
Back
Top Bottom