Tujikumbushe Mashairi tuliyoyapenda shule ya msingi

Tujikumbushe Mashairi tuliyoyapenda shule ya msingi

Baba na mama salamau, nyumbani nawatumia
Siwezi kupiga simu, nipo mbali na dunia
Bila shaka mwafahamu, jela ninatumikia
Sina wa kumlaumu, niliyataka mwenyewe




Hiiii shairi naitafuta sana!!! Natamani niipate tena niirudie!! Hakika kazi ilkuwa nzurii sana...
 
Wanangu Wa faida mpo?
.
Kuna vitu vinafanya wakati Fulani mtu mzima utamani kurudi utotoni
Ingawa ni ngumu ki nadharia (mawazo) yanaweza kukurudisha na ukajikuta Una tabasamu peke yako njiani
.
Nakumbuka moja ya vitu vilivyo ni Fanya niipende shule ili kuwa ni pamoja na kukaa makundi na kusoma hadithi mbalimbali na baadae kuulizana maswali ya hadithi husika.
.
Lakini pia ile Mwalimu anakuja ghafla darasani kisha anamchagua mwanafunzi yeyote aimbe shairi na akikosea basi viboko vinamiminwa

Basi ikawa kila unaporudi home unakariri haswa mashairi ili kesho na wewe uonekane konki
Mashairi yalikua murua Sana na haya ni mfano tu
[emoji652]
"BABA NA MAMA SALAMU
nyumbani nawatumia
Siwezi kupiga simu
Niko Mbali na dunia
Bila Shaka mwafahamu
Jela Nina tumikia
Sina Wa kumlaumu niliyataka mwenyewe"
[emoji654]
"NIKIMALIZA KUSOMA
Nitafanya kazi gani
Nipende kuwa rubani
Kazi nzuri ya heshima
Nirushe ndege angani
Inifikishe salama
Nikimaliza kusoma nitafanya kazi gani"

[emoji654]

"CHITEMO MIMI MASIKINI
uvivu wangu nyumbani
Nikiwa huru njiani nakufa
Nakufa hapa kwanini
Sadiki sasa hashiba
Chakula kingi kwa baba
Nirudi tena kwa baba nakufa hapa kwanini"

Ebwana tupia nawewe shairi lako pendwa tujikumbushe zile nyakati za dhahabu kabisa
Hakika fasihi simulizi hutunza amali za jamii, tuwatengenezee watoto wetu misingi ya kupenda kujisomea vitabu itakua na manufaa maishani mwao.
 
Baba na rafiki zake, walikwenda kutembea
Wakafika kwa Mnyake, hodi wakamgomgea
Wakapata jibu lake, karibu ndani ingia
Watu wale ni wangapi, viti vile vingapi?

Wakakaribishwa viti, ukumbini kuongea
Wakajaribu kuketi, nao hawakuenea
Rafiki yao Japhet, hakupata pa kukaa
Watu wale ni wangapi, viti vile ni vingapi?

Wakaona afadhali, wakae wawiliwili
Kila kiti kuchangia, kwa hii njia ya pili
Kiti kimoja kikabakia
Watu wale ni wangapi, na viti vile vingapi?
 
Baba na mama salamau, nyumbani nawatumia
Siwezi kupiga simu, nipo mbali na dunia
Bila shaka mwafahamu, jela ninatumikia
Sina wa kumlaumu, niliyataka mwenyewe




Hiiii shairi naitafuta sana!!! Natamani niipate tena niirudie!! Hakika kazi ilkuwa nzurii sana...
Baba na mama salamu, nyumbani nawatumia,
Siwezi kupiga simu, nipo mbali na dunia,
Bila shaka mwafahamu, jela ninatumikia,
Sina wa kumlaumu, niliyataka mwenyewe.

Vipi hapa nimefika, bila shaka mnajua,
Nitakaa kwa miaka, gereza likinilea,
Tayari nimeshachoka, tabu zinanisumbua,
Sina wa kumlaumu, niliyataka mwenyewe.

Nilipofika mjini, nadhani nilikosea,
Nikaingia kundini, watu nisiowajua,
Wakanikalisha chini, elimu kunipatia,
Sina wa kumlaumu, niliyataka mwenyewe.

Tukaingia sokoni, wakaniongoza njia,
Nikaenda kwa imani, wao watashambulia,
Nikiwekwa hatarini, wao watasaidia,
Sina wa kumlaumu, niliyataka mwenyewe.

Hatua nikahesabu, mbili tatu nikafika,
Fedha bila kuhesabu, haraka nikanyakua,
Mambo yaliponisibu, wenzangu wakakimbia,
Sina wa kumlaumu, niliyataka mwenyewe.

Meno saba yalinitoka, pale bila kukawia,
Kwa hakimu nikafika, shitaka kanisomea,
Hatimaye katamka, jela nitatumikia,
Sina wa kumlaumu, niliyataka mwenyewe.

Haikimbii misimu, jela ukitumikia,
Naishi kama sanamu, sina la kufurahia,
Najihisi marehemu, kucha kutwa ninalia,
Sina wa kumlaumu, niliyataka mwenyewe,

Ndugu nisalimieni, wote mnaowalea,
Karamu andalieni, nyumbani nikirejea,
Sheria ziheshimuni, mimi nimeshuhudia,
Sina wa kumlaumu, niliyataka mwenyewe.
 
Back
Top Bottom