Tujikumbushe, ni kitu gani kimewahi kukutoa ushamba!?

Tujikumbushe, ni kitu gani kimewahi kukutoa ushamba!?

Naingia benki mara ya kwanza baada ya kufungua mlango na kuingia naona mlango unarudi wenyewe sasa nikaogopa usije kujibamiza kwasababu ni wa kioo nkaushika na kuuanza kuupeleka taratibu .

Mlinzi ndo akanambia hauna shida we achia tu
Ahahahaha
 
Mara ya kwanza kuendesha gari nilikuwa natumia miguu miwili kucheza Na automatic transmission wa kulia una accelerate wa kushoto una break[emoji23][emoji23][emoji23] kweli ushamba mzigo
Cha ajabu kwny car racing trainings wanafundisha kutumia miguu 2 kwny automatic car kwa usalama zaidi.
 
nimeenda posta kutuma barua ilikuwa kazi siku ile nawaza naidumbukiza ki namna gani? kwa urefu ama upana.

nikaona isiwe shida nikamfata mtu mmoja kumuuliza mzee hii barua naidumbukiza vp? kwa upana ama urefu alicheka saanaaaa yule mzee akanambia vyovyote vile.
haaaah aiseee tupo weng complicators
 
Back
Top Bottom