Tujikumbushe Taifa Stars ya 1980s na miamba ya soka Afrika

Tujikumbushe Taifa Stars ya 1980s na miamba ya soka Afrika

Kumbe mambo mbotela kashafariki.
R.I.P

Viol...... naomba nisahihishe na nifute usemi wangu wa awali..... 'LEONARD MAMBO MBOTELA HAJAFARIKI YUPO HAI'. SAMAHANI WADAU KWA KULETA TAARIFA AMBAZO HAZIKUWA SAHIHI!!!!!!
 
Viol...... naomba nisahihishe na nifute usemi wangu wa awali..... 'LEONARD MAMBO MBOTELA HAJAFARIKI YUPO HAI'. SAMAHANI WADAU KWA KULETA TAARIFA AMBAZO HAZIKUWA SAHIHI!!!!!!

Pamoja mkuu,maana huyu jamaa nilimsikiliza mwaka Jana tu,sasa nikashangaa gafla imekwaje hata sikusikia kwenye media.


Pamoja mkuu
 
haya bwana naona wewe una ubishi wa kiulaya ulaya. tukitumia vigezo vya mafanikio ya individual players hata leo wapo ambao klabu kubwa za Africa zimewanunua kutoka tz sasa tuseme timu yataifa imekuwa imara? kwanza hii heading inapotosha eti MIAMBA YA SOKA AFRIKA!!! kwa lipi walilofanya .kujifariji tu

You are some how right by your heading interpretation, but the heading is not as you claim to be!

Vv
 
Wanabodi, nawaomba radhi wenzetu ambao mko chini ya miaka 40 maana hamuwafahamu sana wachezaji hao, lakini kwa kuwa JF ni kisima cha maarifa, mtaweza kupata historia ya miaka hiyo.

Nakumbuka Taifa Stars ya mwaka 1980, ndio pekee ambayo iliyofika mbali zaidi ktk michuano ya AFCON.

Tukumbushane wachezaji wa kikosi hicho, na ambacho hakijawahi kutokea kwa maana ya kufika mbali ktk mashindano hayo.

Baadhi ya wachezaji hao ni:-
1. Juma Pondamali (Mensah)
2. Leopard Mukebezi (Tasso)
3.
4. Leodgar Tenga (T Captain)
5. Jella Mtagwa
6. Mohammed Rishard (Adolf)
7.
8.
9. Augustino Peter (Peter Tino)
10. Mohammed Salim
11. Thuwein Ali

Wakongwe wenzangu, Baba Enock na wengine wachezaji tukumbushane niliowasahau.

Vv



Hii ilikuwa kabla hawajaanza bongo fleva (uchawi) kwani walijali sana vipaji vya wachezaji si mvuto wa nguvu za giza. Siku hizi kila mchezaji ni mbongo fleva (fake/mchawi) na ndiyo maana hawafundishiki/hawakocheki. Mtu anaona bora aroge ili apande ndege na kwenda kubadirishana jezi na wachezaji wa Misri, akirudi anajisifia kuwa alimpa mchezaji wa Misri jezi yake. Rais Mwinyi was dead right kuwa Taifa Stars ni kichwa cha mwenda wazimu.
 
View attachment 260444

Majina ya wachezaji wanaotajwa kwenye wimbo wa Taifa Stars

Iddi Pazi
Kiwelo Mussa
Said George
Athumani Maulidi
Athumani Chama
Ahmed Amasha
Ramadhani Lenny
Mohamed Adolf
Octaviani Mrope
Makumbi Juma
Peter Tino
Charles Borniface
Lila Shomari
Hillary Hemed
Selestine Mbunga
Zamoyoni Mogela

Abdul Wakati Juma
Joel Bendera

Hao wawili wa mwisho nadhani walikuwa makocha

Umenikumbusha mbali; huyo ni Freddie Ndala Kasheba (Supreme) akiwa na Orchestra Safari Sound.

Hicho kikosi cha Stars ni cha miaka ya katikati ya 1980.

Wachezaji na Timu zao ni: Idd Pazi 'father', Kiwelu Mussa 'Super Kiwelu', Athumani Maulid 'Big man', Ramadhani Lenny Maufi 'Abega', Lilla Shomari, Zamoyoni Mogella 'Golden Boy' (Simba SC); Said George, na Hillal Hemed (Coastal Union), Athumani Juma 'Chama', Ahmed Amasha, Makumbi Juma 'Bongabonga', Charles Boniface Mkwasa 'Master', (Yanga SC); Mohammed Rishard 'Adolf', na Peter Tino (Pan Africa), Octavian Mrope, na Celestine 'Sikinde' Mbunga (Majimaji). Abdul Wakati Juma alikuwa kiungo mahiri kutoka Small Simba ya Zanzibar.

Vv
 
Umenikumbusha mbali; huyo ni Freddie Ndala Kasheba (Supreme) akiwa na Orchestra Safari Sound.

Hicho kikosi cha Stars ni cha miaka ya katikati ya 1980.

Wachezaji na Timu zao ni: Idd Pazi 'father', Kiwelu Mussa 'Super Kiwelu', Athumani Maulid 'Big man', Ramadhani Lenny Maufi 'Abega', Lilla Shomari, Zamoyoni Mogella 'Golden Boy' (Simba SC); Said George, na Hillal Hemed (Coastal Union), Athumani Juma 'Chama', Ahmed Amasha, Makumbi Juma 'Bongabonga', Charles Boniface Mkwasa 'Master', (Yanga SC); Mohammed Rishard 'Adolf', na Peter Tino (Pan Africa), Octavian Mrope, na Celestine 'Sikinde' Mbunga (Majimaji). Abdul Wakati Juma alikuwa kiungo mahiri kutoka Small Simba ya Zanzibar.

Vv

Umenikumbusha mbali sana, hiki kikosi kama sikosei ilikuwa 1984, nakumbuka tulicheza na Sudan hapa Dar wakatufunga tuliporudiana Sudan tukashinda, man of the Match akiwa Idd Pazi na ndio kisa cha El-hilal kumsajili mwaka huo. Kwenye benchi upande wa Golini alikuwa Ramadhani Korosheni wa KMKM, jamaa nilikuwa sina imani naye!
 
huwa najiuliza hawa mnaowasifu walishirii mara ngapi michuano ya mataifa huru Afrika? mimi naona ni yaleyale hakuna lolote

Hata mimi nashangaa. Eti "miamba ya Afrika". Na hao Misri wajiite nani kama sisi ni miamba? Tatizo letu Tanzania ni kuwa tuna "low expectations" kwenye kila kitu ndio maana tunaona eti kwenda kwenye AFCON na kutolewa kwenye hatua za awali tena miaka 35 iliyopita ni mafanikio. Shame on us!
 
Zamoyoni Mogella alikuwepo kweli mwaka 1980?
 
Nico Njohole alikuja baadaye pamoja na Ahmed Amasha, Athumani Juma Chama, na Yusufu Ismail Bana. Daud Salum na Kajole sikumbuki kama waliwahi kuwa ktk first eleven ya T Stars.

Kumbukumbu yangu Stars ya 1981iliyopigwa na Harambee Stars Uwanja wa Taif ilikuwa na:Hamis Kinye,Yusuf Bana, Ahmed Amasha, Athumani, Juma Chama, Jella Mtagwa, Nico Njohole, Peter Tino.

Harambee Stars ilikuwa
Mahamoud Abas (Kenya One), Hussein Heri, Josephat Mulira, Bob Ogolla, Wilberforce Mulamba Francis Kadenge, Peter Otieno 'Basanga' na wengine.

Vv
Ongezea Mogela na Juma Burhani
 
Back
Top Bottom