CHAI CHUNGU
JF-Expert Member
- Feb 20, 2012
- 7,113
- 933
Huyo jamaa yuko hai na nnadhani anaishi maeneo ya UKONGA,maana mara nyingi nakutana nae maeneo ya Banana-Uk.Nimemkumbuka Malima Ndelema, huyu alikuwa bingwa wa kipindi cha ngoma za asili za makabila mbalimbali, sijui yu hai bado au sijui yu wapi sasa huyu mtu.
Ni watu waliokuwa wanakupa sababu na kukulazimisha kusikiliza radio tofauti kabisa na sasa!
Saa nne asubuhi ilikuwepo taarifa ya habari kama sikosei,saa kumi alasiri pia ilikuwepo<hata kifo cha sokoine kilitangazwa wakati huo,saa moja usiku habari kutoka sauti ya tz zanzibar
Watangazaji wazuri waliobaki TBC ni, Shaban Kissu, Sued Mwinyi, Agnes Mbapu na Kingalame. Walio wengi vimeo wanajifanya wajuaji sana wawapo hewani. Hakuna nidhamu kama iliyokuwepo enzi za akina Nyaisanga. Wananiuzi sana wanapotumia maneno kama Mwalyego 'ameweza' kufeli masomo.4 au Tino (aliweza) kukosa penati!!!
Hiki ni kikosi cha first 11 ya Radio One.
Waliokaa kutoka Kushoto ni Charles Hilary kwa sasa yuko BBC-London
Mikidadi Mahamod (Brother) sasa ni Mkurugenzi wa Radio Uhuru, Mzungu Mike Ross, na Uncle J. Nyaisangah.
Waliosimama toka kushoto, Deo Mshigeni yuko US, Monica Mfumia yuko UK, Florah Nducha ni Mkuu wa UN Radio New York, Vicky Msina, ni PRO wa BOT, Aboubakar Liongo yuko DW-Radio ya Ujerumani, Lilian Mbaga sasa ni Mkurugenzi wa TGNP, Sunday Shomari yuko VOA na Taji Liundi sasa ni Meneja wa PRT ya TBC.
Nimemkumbuka Malima Ndelema, huyu alikuwa bingwa wa kipindi cha ngoma za asili za makabila mbalimbali, sijui yu hai bado au sijui yu wapi sasa huyu mtu.
Ni watu waliokuwa wanakupa sababu na kukulazimisha kusikiliza radio tofauti kabisa na sasa!
Nimemkumbuka Hassan Mgumba kama sijakosea jina na kipindi chake cha matukio ya wiki
enzi hizo kwa sisi wa mpakani tunaipata RTD usiku pekee tena kwenye shortwave
Tulitegemea zaidi raidio za Kenya.
Kuna mwingine anaitwa Mrekoni alikuwa na kipindi chake kizuri cha karibu mgeni au mgeni wetu alifariki majuzi
He was talented.
Pascal unaweza kujua kama Angalieni Mpendu tunae? Na kuna kile kipindi cha 'Hisia na Muziki' kilikuwa poa sana
Hawanihusu nilikuwa hata sijazaliwa
Mama Debora Mwenda
Unakumbuka zile hadithi? jumamosi ikifika saa nane mchana watoto wote tuko kwenye radio, na mashuleni tulikuwa na club za mama na mwana
ben kiko bado yu hai,na mwanae ni swaiba wangu sana,na ben kiko mwenyewe yupo tabora
Wanabodi,
Baada ya Kifo cha Mtangazaji Nguli nchini, Uncle J. Nyaisanga, naomba kuchukua fursa hii, kufanya reflection ndogo ya Watangazaji wa RTD waliotangulia mbele ya haki. Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.
Naomba nisizungumzie kulitowatoa duniani, wala hatima ya familia zao walizoziacha huku nyuma maana sio tuu nitazidi kuogopa, bali pia tutazidi kuumia!. Just imagine, kijitaasisi kidogo kama RTD chenye ofisi yake pale BH-Pugu Road kupoteza idadi kubwa hivi ya watumishi wake (tena hawa ninaowataja ni Watangazaji tuu!, achilia watumishi wengine!. Sii bure!, ila lazima tukubali ni kazi ya Mungu, na kazi ya Mungu haina makosa!.
Hii list sio walikufa lini ni random, nikiwakumbuka wengine nitawaongeza!
Tukianzia na
- David Wakati
- Abdul Masudi (Jawewa)
- Eli Mbotto
- Stephen Mlatie
- Siwatu Luanda
- Salama Mfamao
- Salim Seif Nkamba (Mjomba)
- Michael Katembo
- Nelly Kidella
- Halima Mchuka,
- Omar Jongo
- Tumboi Tamimu Risasi
- Mohamed Ng'ombo
- Abisai Stephen (Uronu)
- Stephen Lymo.
- Nadhir Mayoka
- Juma Ngodae
- Rukia Machumu
- Karim Besta
- Henrick Michael Libuda
- Idrissa Sadalah
- Bati Kombwa
- Iddi Rashid Mchatta
- Dominic Chilambo
- Hassan Mkumba
- Khadija Said
- Ally Saleh
- Kwegier Munthali
- Leonard Mtawa
Jee unawakumbuka?, unakumbuka vipindi vyao?!, unawakumbuka kwa lipi?!.
Pia sio vibaya kuwaulizia wale watangazaji wa siku nyingi ambao hatujui walipo, ili kama nao wametangulia tuyaingize majina yao.
RIP All the Fallen Heroes wa Tasnia ya Utangazaji Tanzania!,
Pascal.
nakumbuka KBC kulikua na dada mmoja hadija ali ktk salaam nilikua napenda.
Sio Chaguo la msikilizaji, bali kilikuwa kinaitwa Ombi lako, na pia hakikuwa siku zote, siku zingine tulikuwa tunatupiwa mashairi (Malenga wetu),
CC: jazba
YANGA wamevaa jezi za rangi ya kijani na bukta za njano hawa simba wametia UZI nikisema UZI nafikili mmeshanielewa huyo CHARLES HILARY akitangaza mpira SIMBA na YANGAChilambo...chilambo...unaniskia..?..nakuskia Charles..?hapa Uwanja wa Taifa kumekucha Zamoyon Mogela anawainua wapenzi wa Simba...Simba 1 Maji Maji toka Songea hawajapata kitu ....haya Chilambo endelea..!! asante sana Charles hapa Mwanza mambo bado si Pamba wala Ushirika toka moshi waliojipatia bao..lala laal laaa goooooo!!!wakati napokea toka kwako Charles mshambuliaji wa Pamba John Makelele alipata krosi safi sana toka kwa Hamza Mponda anaukwamisha mpira wavuni Pamba 1 Ushirika hawajapata kitu....Daaah ni mengi sana ya kukumbuka sijui kama zile enzi za RTD zitarudi.
Duh umenikumbusha mbali, kile kipindi cha mama na mwana nilikuwa sikosi; kulikua na hadithi za kusisimua sana, mfano UA JEKUNDU (ambapo kuna stori ya msichana aliyependwa na zimwi lililokuwa na bonge za jumba zuri msituni etc etc..ilikuwa inasisimua enzi hizo za utoto
Acha uongo kama wewe ukiwa unaisikiliza hii redio 24/7 huwezi kuandika ushuzi kama huo uliouandika...
nidhamu ndo msingi wa TBC.
Na Still kuna watu kama Acheli Shilewa, Masoud Masoud, Aloisia Maneno, Al anisa Shida Masamba na wengine weengi wanafanya vizuri still.
Pia kuna chipukizi kwa mfano Betty Tesha Mwinuka anafanya vizuuri mno kiasi kwamba hutachoka kumsikiliza akiwa anatangaza...
Njoo na uharo sasa...maana huo ushuzi haujabamba
..Wakuu, Kuna huyu Dada mmoja mtangazaji jina limenitoka kidogo ambaye alifariki kama sio mwaka jana ni juzi tena alikuwa amekwenda kazini na Akaanguka huko na kufariki! alikuwa anaitwa nani vile...??