Tujikumbushe watangazaji wa zamani wa Redio na TV

Nimemkumbuka Malima Ndelema, huyu alikuwa bingwa wa kipindi cha ngoma za asili za makabila mbalimbali, sijui yu hai bado au sijui yu wapi sasa huyu mtu.

Ni watu waliokuwa wanakupa sababu na kukulazimisha kusikiliza radio tofauti kabisa na sasa!
Huyo jamaa yuko hai na nnadhani anaishi maeneo ya UKONGA,maana mara nyingi nakutana nae maeneo ya Banana-Uk.
Kwasasa anarusha kipindi cha "YAKALE NI DHAHABU"
 
Saa nne asubuhi ilikuwepo taarifa ya habari kama sikosei,saa kumi alasiri pia ilikuwepo<hata kifo cha sokoine kilitangazwa wakati huo,saa moja usiku habari kutoka sauti ya tz zanzibar

...Kuanzia saa Mbili asubuhi had Saa Tano kamili RTD ilikuwa inarusha vipindi vya Masomo ya shule za Msingi.Kumbuka 'A Thousand Miles to Tanga'. Kuanzia Saa Tano Kamili hadi Saa Sita ilikuwa ni Kipindi cha Wakati wa Kazi. Saa Sita Kamili hadi Saa Saba ilikuwa ni kipindi cha Salmu cha Mchana Mwema na Saa Saba Kamili Taarifa ya Habari.

Baada ya Hapo, Vipindi ambavyo vingefuata vilitegemea Siku gani ya Wiki lakini vingekuwa ni Pamoja na 'Karibu RTD', 'Mgeni wa Wiki' 'Baraza/Ukumbi wa akina Mama' nk.

Hizi taarifa za Habari za Saa Nne na Saa Kumi zilikuja baadae Sana Mkuu.Taarifa ya Habari Kutoka Visiwani ilikuwa ni Saa 12 Jioni, Nadhani.


Taarifa za Kwanza kabisa za Kifo cha Sokoine hazikuwa kwenye Taarifa ya Habari ya Saa Kumi bali Matangazo ya Kawaida yalisimamishwa na Ikulu inakunganishwa moja kwa moja hewani na ndipo Tukamsikia Mzee wetu Nyerere akitangaza kwa Masikitiko Kifo cha Sokoine.

 


Acha uongo kama wewe ukiwa unaisikiliza hii redio 24/7 huwezi kuandika ushuzi kama huo uliouandika...
nidhamu ndo msingi wa TBC.
Na Still kuna watu kama Acheli Shilewa, Masoud Masoud, Aloisia Maneno, Al anisa Shida Masamba na wengine weengi wanafanya vizuri still.
Pia kuna chipukizi kwa mfano Betty Tesha Mwinuka anafanya vizuuri mno kiasi kwamba hutachoka kumsikiliza akiwa anatangaza...

Njoo na uharo sasa...maana huo ushuzi haujabamba
 


Aboubakar Liongo hayupo Ujerumani tena...
 
Nimemkumbuka Malima Ndelema, huyu alikuwa bingwa wa kipindi cha ngoma za asili za makabila mbalimbali, sijui yu hai bado au sijui yu wapi sasa huyu mtu.

Ni watu waliokuwa wanakupa sababu na kukulazimisha kusikiliza radio tofauti kabisa na sasa!


Still yupo TBC mpaka leo...
 


Ni Hassan Mkumba...sio Mgumba
 
Mama Debora Mwenda
Unakumbuka zile hadithi? jumamosi ikifika saa nane mchana watoto wote tuko kwenye radio, na mashuleni tulikuwa na club za mama na mwana

Nakumbuka sana kipindi kiliitwa mama na mwana....na hadith kama ADILI NA NDUGUZE...
I wish i could turn back the hand of time
 

Sarah Dumba, sijui yuko wapi?
 
Sio Chaguo la msikilizaji, bali kilikuwa kinaitwa Ombi lako, na pia hakikuwa siku zote, siku zingine tulikuwa tunatupiwa mashairi (Malenga wetu),

CC: jazba

Acha uongo Kipindi Cha chaguo la msikilizaji kilikuwepo tena kama sikosei saa nane mchana siku ya jumamosi
 
YANGA wamevaa jezi za rangi ya kijani na bukta za njano hawa simba wametia UZI nikisema UZI nafikili mmeshanielewa huyo CHARLES HILARY akitangaza mpira SIMBA na YANGA
 


kiukweli radio tz kipindi hicho ilikuwa radio bana sio ss ivi.. hii mama na mwana ilikuwa kiboko aisee, nakumbuka kipindi hicho nilikuwa nasoma madrasa ambapo jumamosi na jumapili tulikuwa tunaenda asubuhi na jioni, sasa siku ya jumamosi ilikuwa ni lazima nichelewe kwenda madrasa mchana maana hadi kwanza nisikilize mama na mwana....YAANI ilikuwa ni tamu hatari...nakumbuka ustadh wetu alikuwa mkali kupita kiasi yaani ukichelewa madrasa hata dakika tano ni fimbo lakini siku ya jumamosi wanafunzi wengi tulijitolea kuchapwa na ustadh kwa kuchelewa kuliko kukosa mama na mwana.......yaani sitasahau..

sijui siku hizi watoto wanafurahia nini jamani, ivi wana cha kukumbuka ukubwani kweli zaidi ya facebuku?..dunia imechange sana
 


...Ni Asheli Chilewa kama sikosei.
Mkuu unafanya kazi huko nini?
Mbona umepaniki mno Brother/Sister? :smile-big:
Maana kama unafanya kazi huko halafu majibu yenyewe ndiyo haya, Mkuu atakuwa amedhibitisha alichosema.
Naamini pointi yako ineweza kueleweka tu bila hayo maneno yanayokarahisha!

 
..Wakuu, Kuna huyu Dada mmoja mtangazaji jina limenitoka kidogo ambaye alifariki kama sio mwaka jana ni juzi tena alikuwa amekwenda kazini na Akaanguka huko na kufariki! alikuwa anaitwa nani vile...??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…