mwanawao
JF-Expert Member
- Aug 18, 2010
- 3,192
- 5,743
Wadau kwenye nchi kila siku bank zimekuwa zikiongezeka kila siku. Hali hii ni nzuri maana inaongeza ushindani na kumfanya mteja kupata huduma nzuri zaidi tofauti na bank ilivyokuwa chache. Kwa mfano hakuna mtu anayependa kwenda kwenye bank zenye utitiri mwingi wa watu maana kama unataka kupata huduma lazima itakuchukua kupoteza karibia siku nzima ukiwa bank. Hakuna anayependa kupoteza muda mwingi namana hii kwa siku. Cha ajabu zaidi utakuwa ukipokea majibu ya kiburi kutoka kwa wahudumu ya kutokumtosheleza/kumridhisha mteja pale unapohitaji huduma kutoka kwao.
Katika hali kama hii watu tunakimbilia sehemu ambazo tunaweza kupata huduma nzuri na kuhudumiwa kwa haraka. Ila kuna jambo lingine ambalo linaniogopesha kwenye huu utitiri wa bank. Ikitokea bank IKIFILISIKA au KUUNGUA MOTO, Je, kuna uwezekano wa mteja kupata hela yake aliyohifadhi katika bank hiyo?
Wakuu naomba tusaidiane kupeana taarifa juu hili ili wakati wa kuchagua bank ya kuhifadhi madafu yetu tuwe makini zaidi.
Katika hali kama hii watu tunakimbilia sehemu ambazo tunaweza kupata huduma nzuri na kuhudumiwa kwa haraka. Ila kuna jambo lingine ambalo linaniogopesha kwenye huu utitiri wa bank. Ikitokea bank IKIFILISIKA au KUUNGUA MOTO, Je, kuna uwezekano wa mteja kupata hela yake aliyohifadhi katika bank hiyo?
Wakuu naomba tusaidiane kupeana taarifa juu hili ili wakati wa kuchagua bank ya kuhifadhi madafu yetu tuwe makini zaidi.